THRDC: Maamuzi ya Rais Trump kusitisha misaada yamekuja ghafla na yanakiuka makubaliano ya mikataba

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kufuatia uamuzi wa Rais wa Marekani Donald Trump ( Executive Orders) kuzuia fedha zote za misaada zilizokuwa zinatolewa na serikali ya Marekani kupitia baadhi ya taasisi zake ikiwemo taasisi ya misaada ya Marekani ( United States Agency for Development – US-AID), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeeleza kuwa uamuzi huo umekuja ghafla.

Ambapo wameeleza kwamba kitendo cha kuzuiwa kwa fedha ambazo zilikuwa zimeshaingizwa kwenye utekelezaji ni kukiuka misingi ya utawala bora,

Aidha amesema kuwa katika utafiti wa awali wanebaini uwepo wa athari za uamuzi huo katika sekta mbalimbali nchini ikiwemo asasi za kiraia (CSOs).

Kupitia tamko ambalo limetolewa na THRDC pamoja East African Human Rights Institute leo February 10, 2025 wameeleza yafuatayo.







 
Alaa! Kumbe ni kweli hilo limewagusa wengi etie? Sasa tulieni basi dawa iwaingie; la sivyo mkimchokonoa atakaza zaidi mshindwe kupumua.
 
Mnapenda msaada saada nyinyi sijui kabila gani ww mbona si ni boda boda tunaishi uza gari lako nunua boda tafuta riziki
 
Wezi nyie mshazoea kutumbua mifedha yao
Pesa zitakuja ila kwa usimamizi maalum,ruling nyie mavitambi makubwa

Ova
Yeah. Kama huwezi kujiongoza, basi uwe tayari kuongozwa. Usipokubali na ukashupaza shingo utaachwa hapo. Umenikumbusha mbali mkuu. Majuzi kati hapo ilikuwa fedha ya ufadhili (magari yao yalisajiliwa TX.....). Huwezi kununua hata mafuta (Diezel au Petrol) bila idhini ya mfadhili na ni kwenye vituo vilivyoainishwa. (Identified petrol Stations) Matengenezo (Maintenance) ni kwenye garage zilizoidhinishwa. Fedha ya matumizi lazima uiandikie mpango kazi kwa mfumo walioutaka wao e.g. DANIDA wao walikuwa ni lazima utumie LFA.
Upigaji ulikuwepo sikatai lakini sio kama ilivyo sasa ktk kiwango cha "ni kufuru" ck hizi.
 
Hawa fish walipowachiwa pesa tu wazisimamie pia wakawa wanazila wanazipeleka kwenye matumizi yao mingine
Miradi mingi waliyokuwa wanasimamia wenyewe ma tx ilikuwa inaenda viZuri na ilikamilika
Kama DANIDA walivyokuwa wanasimamia project ya maji mbeya mjini wakati ule mradi ulienda vzr....
Tramp akaze hapo hapo na ikiwezekana azidishe

Ova
 
Exactly. Mswahili abakie ni wa kutumwa tu tena kwa maelekezo maalum. Fedha na usimamizi waachiwe wenyewe maTx. Kwani mswahili hilo limemshinda. Ujanja-ujanja na maneno meeeeengi lakini utekelezaji kitu Tangible kionekane imekuwa ni zero mtoto wa sifuri kazi ni kujidai kila siku eti tumesoma, tuna degree (ya google)tuna mat...ko (ya Uturuki)na upuuzi kama huo.
 
Wezi nyie mshazoea kutumbua mifedha yao
Pesa zitakuja ila kwa usimamizi maalum,ruling nyie mavitambi makubwa

Ova
Tena wajinga kweli kweli. Wamezoea vya bure. Watu wanauawa kila siku na wengine wanawekwa rumande kihuni bila dhamana kwa shinikizo kutoka Kizimkazi wao wako kimya, halafu wanakuja kulilia vya watu. Waambie hawa watawala wetu wanaishi kifahari kuliko hata hao wafadhili waache matumizi ya kifahari.
 
Yaani inasikitisha kabisa tena unakuta hicho kitaasisi kimekaa vikao kabisa nawakalipana posho.

Mwishoni mwa kikao wakatoa waraka mrefu wakiwalaumu na kulilia pesa za watu.

📌📌📌Afrika na Uafrika ni laaanaaa!!!
 

Mikopo siyo Sadaka, lakini Misaada ni Sadaka.
 
Hakuna kabisa nidhamu ya hali ya juu katika Matumizi ya Fedha za Kodi za Wananchi.
 

Attachments

  • 5771391-6b7300c48c43013b94b420cc6e416c60.mp4
    8.3 MB
Washawashtukia

Ova
 
Chafya imepigwa US ila kero yake imefika mpaka kazuramimba huko ndanindani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…