Thread Ya Vitu / Mambo uliyochelewa Kufahamu!

Thread Ya Vitu / Mambo uliyochelewa Kufahamu!

Kibuje

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2018
Posts
292
Reaction score
286
Katika maisha kuna mambo ambayo tunahisi tunayajua / tuko sahihi kuamini hivyo mpaka pale inapotokea unafahamu kwamba unavyoamini sio sawa. Yapo mengi kama vile kuamini -

> Mtu akikuruka miguu utakuwa mfupi hadi pale atakaporudia kukuruka.
> Kutumia sukari nyingi, (eg: kwenye chai / juisi) kunasababisha kisukari.
> Uking'atwa na mbwa, kupona ni mpaka unyonye maziwa ya shangazi yako.
> Mama mjamzito kula mayai itasabisha kuzaa mtoto mwizi n.k

Yapo mambo mengi ambayo wengi wetu tumechelewa kuyajua na tukiachana na hayo hapo juu, mimi binafsi imenichukua muda mrefu sana kufahamu kama muhogo hauoti kwenye mti wa kisamvu. Nilikuwa najua muhogo na kisamvu ni product ya mti mmoja! Kitu kingine, ni kwamba sikuwa najua wimbo wa 'Dillema' ulioimbwa na Nelly na Kelly ulikuwa ni wimbo unaohusu 'cheating kwenye mapenzi'. 🤣

Wewe binafsi ni kitu gani ambacho unahisi umechelewa kukijua / kujua ukweli wake?
 
Tunda alilokula Adam hawa nilikua nikiuliza ni tunda gani bila kupata majibu but now ni mwaka wa sita tu tangu nilijue hili.
Hilo mpaka leo linanichanganya, ni tunda lipi hilo mkuu?
 
nilijua utu uzima dawa, kumbe kwenye mapenzi atakuwa mgonjwa wa kulazwa ICU
 
Alifanya matusi na nyoka kisha na adam kwa lugha nyepes nyoka alimbikiri hawa ana Adam akapita alipotoka kupita nyoka ila lugha za mafumbo za vitabu vya Dini kama biblia vimefumba hapa
Duuh! kwahiyo nyoka alikulaje mzigo sasa, na dudu ya nyoka ipo kwa wapi?!
 
Back
Top Bottom