Tiba ya kuondoa virusi vya ukimwi mwilini baada ya kulala na mwathirika haraka!

Tiba ya kuondoa virusi vya ukimwi mwilini baada ya kulala na mwathirika haraka!

tunatakiwa tuwe makini maana wa bongo tukijua tu kuna PEP basi tutajirusha kama nini kwenye ngono haswa kwa kipindi hiki cha maadili zero kwenye ndoa, jamii
 
nakaa karibu na mount ukombozi hospital siku hizi nitakua situmii condom
 
Dk. Cku moja nilifanya mapenzi na msichana m1, baada ya cku moja mkojo ulikuwa unauma saana,, ni nini hicho??
 
AlhamduliLlah, sina HIV wala UKIMWI kwa hiyo sina sababu ya kuitumia, ila kuna walioitumia nawafahamu na nimeona walivyofanikiwa.

Tembelea hiyo tovuti ujionee mwenyewe.
mi sina bwana nitembelee ya nini...
 
Post Exposure Prophylaxis (PEP) ni moja ya njia za kuzuia maambukizi kwa watu ambao hawana virusi vya UKIMWI wasiwe navyo. Mara nyingi inatumika kwa wahanga wa kubakwa na wafanyakazi wa afya ambao wanaweza kujidunga,kujikwaruza au kumwagikiwa na maji maji yanayotoka kwa mgonjwa alieathirika. Historia ya PEP ilianza na dawa mbili na sasa ni dawa tatu ambazo zinatumiwa kwa siku 28 baada ya tukio. Inapendekezwa kuwa mtu aliyekuwa exposed apimwe na kuanzishiwa hayo madawa ndani ya masaa 72 bada ya tukio.
Kuhusu effectiveness ya huu mpango bado haujaweza kufanyiwa uchunguzi wa kutosha kuweza kuthibitishwa kuwa hauna matatizo. Kwa wale wanaokfanya ngono zembe sina uhakika kwa wanaweza wakajihami kwa PEP.

Hii ni kweli.
Ila utakua ujinga wa Hali ya juu, Kua uende ukatafute virusi kwa makusudi huku ukitegemea PEP.
Kwanza Kama tunavyojua dawa zote ni sumu, halafu dozi yake ni 28 days, that means ule dawa asubuhi na jioni kwa mda wa wiki nne mfululizo.
Pili hakuna garantii Kua ukitumia PEP basi ndo uko salama, hii ni PROPHYLAXIS sio chanjo.
Tatu hizo dawa zinazotumika kwenye PEP ni ARV zile zile wanazotumia ndugu Zetu wanaoishi Na VVU, Zina maudhi madogo Na makubwa.
Nne zinanunuliwa ghali kwa hiyo hakuna Dr. Anayejua maadili ya kazi yake atakae kupa wewe dawa uchezee kila siku.
Mi ningeshauri tuchukue tahadhari Na kujikinga kuliko kutegemea PEP.
shukran.
ImageUploadedByJamiiForums1373194276.582077.jpg
 
Nimekusoma mkuu, jambo la muhimu sana kuchukua tahadhari, na isitoshe hakuna researcher yeyote aliyethibitsha kuwa PEP inatoa kinga 100%.
 
Smile ni kweli kwamba PEP husaidia kuzuia maambukizi ya HIV shortly after contact. kuna siku moja nilikuwa nina deal na damu kwenye utafiti wangu. what happened wakati namfanyia pricking client wangu akatikisa kidole ile niddle ili mchoma yeye na mimi kwa wakati mmoja.

mbaya zaid the client alikuwa +HIV, basi nilichokifanya punde i washed the place kwa maji ya bomba yanayotiririka for about 15 mints huku nikiwa nakibinya damu iendelee kutoka. kisha nikatumia PEP nilipo test after 3 days nikawa safe na nikarudia baada ya wiki ya ni siku 7 still nikamshukuru Mungu.

sasa huko kwenye kusex nako pia husaidia manake itawaahi wadudu kabla hawajajiincubate kwenye ini.
huwezi kuwa positive in such short time. no antibodies already formed. lazima ucheki baada ya miezi 3 hadi 6. ndiyo PEEP husaidia kuzuia HJIV.
 
It's true,NGO's nyingi huwa wana hizo dawa na wafanyakazi huwa wanaambiwa in case kama umebakwa uende kwa custodian wa hizo dawa within 24hours ili akupatie umeze kwani zinazuia maambukizi ya ukimwi.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Sio ngo tu HOSPITAL zote zinazotoa dawa za ARV zinakuwepo.hizo ni dawa common za ARV zinatumika kwa waathirika wa virusi siku zote nazo ni zidovudine+lamivudine au kwa jina moja rahis..COMBIVIR ...so ukienda unajieleza km ukiwa unafit unapewa..sio umelala na mtu siku 5 zishapita ndo unaenda
 
Back
Top Bottom