Tibaijuka Kumvaa Masilingi?

Something serious must have happened on this river to change its course to Tibaijuka kumvaa Migiro.
This is JF! lest we change its identity to Home of Great Flip - Floppers

- Usijali sana ndugu yangu unajua JF huwa ina watu wanye akili nyingi sana ila kwa wale tuliopo hapa kwa muda mrefu huwa tunaelewa haraka sana, thanks though!

Respect.
You should know by now kinachokwepwa ni nini, Bwa! ha! ha! ha! ndio JF hii na sisi tunakomaa nao tu!

FMEs!
 
sasa hii thread ipelekwe kwenye Celebrities na ibadilishwe kichwa cha habari.

Maoni yangu.

With minimal resources wich is always the case , intense pressure and challenges Tibaijuka can perform and deliver better than Migiro.

Tibaijuka kama akiupata ubunge nina hakika watampunguza makali kwa kumuingiza kwenye system ( Uwaziri)
 
Katika zama hizi, yeyote anayegombea kupitia CCM hata akiwa na rekodi nzuri kiasi gani bado akienda Bungeni hawezi kuwa effective ukilinganisha na Mbunge aliyeingia mjengoni kwa kupitia upinzania.

Tatizo la Ubunge wa kupitia CCM haumpi nafasi Mbunge kujadili hoja kwa kuangalia maslahi ya Taifa, badala yake hoja zinajadiliwa kwa kuangalia maslahi ya chama na serikali.

Wengi tunaweza kuwaona wana rekodi nzuri za utendaji lakini once wakiingia mjengoni huwasikii kujadili hoja zenye maslahi ya Taifa. Na wakiamua kujadili basi watakuwa wana wanauma (ng'ata) na kupuliza. Kinachotakiwa kwa sasa ni kuuma (kung'ata) bila kupuliza.

Mbunge anasimama Bungeni anakosoa hoja kwa vingele zaidi ya 10, akimaliza kukosoa anasema anaunga mkono HOJA kwa asilimia 100! Hivi mtu anaungaje mkono hoja yenye mapungufu kibao?

Tutashangilia leo kwamba Mama Tibaijuka anagombea kupitia CCM na kumpigia debe, akichagulia na kuingia mjengoni anafumba mdomo ama anaanza kuuma na kupuliza. Tunahitaji Bunge lisilo na majority ili wabunge wakiunga mkono hoja, basi iwe ni hoja iliyojitosheleza na kama ina mapungufu basi yawe ni kidogo.
 
Labda nilitoka nje niliposema Tibaijuka hafai kuwa Rais kwa sasa.Ok wakuu ili tusipelekwe kwa celebrities wacha turudi kwenye mstari.
Vipi wakulu wa Muleba patatosha huko akija na mama Tibaijuka kuomba dhamana ya kuwawakilisha???
 
- Kuweka sawa ishu, ni kwamba Mama Migiro kiprotokali sasa hawezi tena kugombea ubunge, wala kuwa Waziri tena, isipokuwa Waziri Mkuu, au Rais tu wa jamhuri.

Respect.


FMEs!
 
-Mama Tibaijuka nampenda kwa kitu kimoja,ana uwezo wa kujenga hoja za kisomi.Anafaa sana hasa katika hoja za kulijenga taifa.Maslingi kwanza hata enzi za mkapa alikua waziri mwingine wa ajabu kweli,nikikumbuka lile sakata lake la uuzaji wa hoteli ya kilimanjarao na hoja za dharau alizokua anatoa siwezi mtofautisha na Mramba
 
Mkuu hapa mimi sikubaliani na wewe.CCM itatawala mpaka mwisho wa dunia?come on,give me a break.
 
Ni kweli kabisa anahitajika nyumbani lakini hawezi narudia hawezi kuleta mabadiliko yoyote akiwa ndani ya sisiemu. Nasema honestly kwamba hata yeye analijua hilo, labda kama anakuja kujishikiza ili apate mkate wake wa siku. Na kama ni hilo hataleta mabadiliko yoyote yale.
Anakumbuka vizuri kesi ya Bawata ilivyomtesa sana hadi kukimbia siasa za nyumbani.
Kwani leo siasa hizo za sisiemu zimebadilika?
 

Keil,
Samahani hapo juu uandike kwa maslahi ya watanzania wachache maana ukichunguza utaona wala si maslahi ya chama ila maslahi ya watu wachache plus watawala wetu
 
Kwa kuanzia tu nimesikia Tibaijuka yuko busy anajenga shule kule Bukoba ya wasichana ya A level na kufundisha pia wasichana waliofeli pia nao wapate nafasi kurudia mitihani ya O level.
Nimeambiwa school fees yake itakawa ndogo sana ingawa sijajua ni udogo kwa kivipi.
Nimeagiza jamaa yangu anichukulie fomu nijue gharama na nitawahabarisha hapa.
Shule inaanza mwezi ujao nadhani.
Sijui nimoja ya pilika pilika za kampeni au ni kwa sababu mama huyu ni kichwa sana?
 
Huyu mama is very critical toka wakati ule alipoanza kuanzisha jukwaa la wanawake Tanzania na hivyo kuna kipindi alikuwa anapata maneno mengi toka UN na kumtaka atoke kwenye nafasi yake ila kama ni kweli tunamkaribisha kwenye siasa za kibongo
 
- Kuweka sawa ishu, ni kwamba Mama Migiro kiprotokali sasa hawezi tena kugombea ubunge, wala kuwa Waziri tena, isipokuwa Waziri Mkuu, au Rais tu wa jamhuri.

Respect.


FMEs!

Mkuu FMES, ni vizuri kuelewa kwamba ktk kuwania nafasi za kisiasa, protokali huwekwa kando wakati mwingine ... ndiyo maana unakuta mtu kama marehemu mzee Rashid Kawawa aliwahi kuwa waziri wa kawaida, baada ya kuwa waziri mkuu; vivyo hivyo kwa CD Msuya.
 

- Ahsante mkuu ila facts zinaendelea kua facts, kwamba Mama Migiro yuko juu sana kulinganisha na Tibaijuka, I mean kuanzia na:

Mwalimu University, Mbunge, Waziri, na sasa Naibu Katibu wa Umoja wa Mataifa eti hapa bongo na huko nje kuna mbongo wa kumlinganisha na huyu Mama ni nani huyo mwenye CV nzito kama hii? So far simuoni! Pole sana mkuu ila hizi ni facts,

- Tibaijuka ana safari ndefu sana mpaka kumfikia Mama Migiro, maana sasa anahitaji kuwa mbunge, halafu awe Waziri ndio labda watamuona wakubwa huko UN, wewe huoni ni safari ndefu sana hii kwa Mama Tibaijuka, au?

Respect.


FMEs!
 

Nafikiri ndiyo ubaya na uzuri wa cheo cha Mama Migiro. Kama ni jeshini ningelisema ana KOROKORO. Kwa Tanzania, kazi itakayokuwa sawa kwake ni Rais au PM. Ila hili aote tu maana sidhani eti Kikwete ampishe kwenye Urais. Pia Lowassa na Rostam Azziz wampitishe ashike U-PM.

Mama Tiba yeye anaweza kwenda kuanzia huko kwenye Ubunge. Akaanza kuonyesha makali yake na mwaka 2015 akagombea Urais na kuwa Rais wa Kwanza mwakamke East Africa. Migiro kusema arudi na agombee Urais ni kushindwa moja kwa moja. Labda iwe ni chaguo la CCM, CCJ au Chadema.

Anyway, sina imani sana na viongozi wengi waliokuwa na Mkapa.
 

Ni dharau kubwa sana kumlinganisha Mama Tibaijuka na Mama Migiro,ni sawa na kumlinganisha Nyerere na JK!

Mama Migiro kawahi kuwa waziri hadi wa mambo ya nje na sasa Naibu katibu mkuu wa UN,utamlinganisha vipi na Mama Tibaijuka ambaye hata nafasi yake ya Habitat kule Nairobi ni kitengo kidogo sana ndani ya UN tena akashindwa kukiongoza kwa ufasaha hadi wafanyakazi wake wakagoma na kuandamana kwa mabango wakiomba UN imuondoe ?
 

- Ahsante sana mkuu, tupo pamoja sana hapo kwenye red line, aanzie ambako Mama Migiro alipita siku nyingi sana zamani, na ndicho hasa tunachokisema..

Respect.


FMEs!
 

- Mkuu so far tumekua na heshima sana kutokwenda hiyo avenue ya Tibaijuka na self-destructions za huko Nairobi zilizosababisha investigations nzito sana toka UN HQ, tulifkiri sio lazima sana kupitia huko maana Mbunge, Waziri, na Naibu Katibu Mkuu wa UN, sijui unamlinganishaje na kiongozi wa kitengo kidogo cha UN kilichoko Africa,

- Ndio maana tunasema kipenda roho bwana hula hata nyama mbichi! hatujaongelea majivuno yake wala vibweka vyake vya kujifanya Mungu mtu, ndio maana tunashangaaa!

Respect.


FMEs!
 
Ni dharau kubwa sana kumlinganisha Mama Tibaijuka na Mama Migiro,ni sawa na kumlinganisha Nyerere na JK!

Mbona JK kajenga UDOM? Kamleta Drogba. Kajenga uwanja wa Taifa. Anajenga kiwanja cha ndege cha kimataifa Bagamoyo na Bandari na kuongeza mkoa mpya Tanzania?

Bado amalizie vitu vichache tu:
1. Ayauwe mashirika ya Reli na ATCL kwani yamekuwa mzigo mkubwa kwa taifa. Mungu bariki Reli imeshabebwa na maji na maji hayohayo yameimalizia ndege yetu ya mwisho ya ATCL.
2. Avunje Muungano, kero kubwa kabisa kwa nchi yetu.

Baada ya hapo tunaanza upya kabisa tukiwa weupe.......
 

I dont mean to be discriminative or stereotyping but the painted line can even make her political ambitions on hold..Thats why im amazed na folks wanaompa a wide chance huyu mama kuwa Rais.Siasa ina watu wake jamani na ndiyo ushangae kwanini Rais akaja kuwa Kikwete na siyo Mwandosya au Marehemu Professor Shayo(RIP)?Hivi ushawahi kujiuliza kwanini kauli ya tupate mgombea anayekubalika na kuuzika kirahisi ni maarufu sana katika siasa?
Nway bora tusiende huko manake tunaweza tukaharibu kabisa.Mama Tibaijuka u have my honor and i really respect and appreciate all ur efforts kufanya hii dunia iwe mahali salama kwa binadamu na kama umeamua kweli basi wish u all the best in ur political career though u dont seem to enjoy politics all that much!
 

Hayo niliyoainisha ndiyo siasa za Bongo na siku zote ndio yametufikisha hapa tulipo na tukiyaendekeza hatuendi mbali na tulipo leo.
Tutabaki kupiga makitaimu hapa jf tukilalama kila siku. Nililiona wazi 2005 na nikawambia rafiki zangu waliokuwa karibu na mimi, na leo wananiita nabii.
Kwa taarifa nani anaweza kutueleza JK aliuzika kwa sifa zipi za maana? Kabla ya kuwa rais alifanya lipi la kumzidi kwa mfano mama Tibaijuka au huyo Rose kiasi cha kununulika?
Tukienda kwa misifa kama anayotoa fmes hapa nawambia tutaishia kufuga wakina EL na RA kibao tu.
Wacha ninyamaze hapa nisije rushiwa vijembe mimi. Migiro ni mzuri na Tibaijuka mzuri na wote wanafaa kwa uongozi. Lakini kwa virus aliye sisiemu hawawezi kufanya lolote la maana kwa nchi hii maana imedhihirika kama wasemavyo wao Chama kina wenyewe na hao wenyewe ndio wanatuamulia watanzania twende wapi hata kama hatutaki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…