Tigo Bussiness waboresha bando zao, ujazo mkubwa, gharama nafuu

Last Seen

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
229
Reaction score
566
Tigo wameboresha Vifurushi vyao vya malipo ya baada kama ifuatavyo.

DATA ONLY
15K......15GB
30K......35GB
40K.......48GB
60K.......72GB
100k........120GB

COMBO
15K........10GB + dakika 400
30K........25GB +Dakika 1000
40K.......35GB + Dakika 2000
60K........55GB + Dakika 3000
100K......100GB + Dakika 6000

Ili Kujiunga unapaswa kuwa na viambatanisho vifuatavyo.
  • TIN number
  • Kitambulisho/Leseni
  • Leseni hai ya biashara
Security Deposit
Pia, Kabla hujaungwa na huduma utapaswa kulipia security deposit ambayo ni thamani halisi ya pesa ambayo utakuwa unalipia kila mwisho wa mwezi. Mfano; Ukihitaji bando la 30k, Utapaswa kulipia 30k kama security deposit.Hii security deposit itakuwa kama ulinzi tu na haitatumika popote, Ikitokea ukasitisha huduma na miezi yote ulilipia huduma hii pesa utarudishiwa kwenye Tigopesa yako.

Jinsi ya kulipia security deposit
1. Bonyeza Menu ya Tigopesa *150*01#

2. Kisha chagua namba '4' Lipa bili

3. Chagua namba '2' Kupata majina ya kampuni

4. Namba '6' TIGO bisiness

5. Kisha bonyeza namba '2' security deposit

6. Weka Kumbukumbu namba ambayo ni namba yako ya simu unayoitumia kwa Tigo B2B.

7. Kiasi unacholipia.

8. PIN

9. Thibitisha na Tuma.

Jinsi ya kulipia gharama za huduma baada ya matumizi (Mwisho wa mwezi)
Utapaswa kulipia huduma kila mwisho wa mwezi kupitia Tigopesa yako, na utakuwa na siku za ziada kumi na tano kukamilisha deni lako.

KUJIUNGA
Ukihitaji kujiunga nitumie viambatanisho nilivoeleza awali (leseni hai ya biashara,TIN na Kitambulisho cha NIDA) kupitia email hii lastseen@duck.com

NB
Sijaweka namba za simu kwa sababu baadhi ya wateja hawapendi kutambulika ID zao, email inakuwa rahisi zaidi.


Kama una swali au Kuna mahali hujaelewa unaweza kuuliza nitakujibu hapa.

Mshana Jr johnthebaptist GENTAMYCINE Raphael Thedomiri Medecin Watu8 zwenge ndaba Lavit je parle Msanii Bueno




 
Hii toka lini mm mbona wameniwekea tr1 ila nimekuta kifurushi cha siku zote
 
Ntapita pale tigo kupata huduma.sema hapa kipengele ni leseni ndio tatizo
 
Lete ushahidi wa text, mtu kajiunga kapata hizo BANDO.!

Hata hio Posta uliyoweka hapo juu, Tigo hawaitambui.
Fatilia kwanza mkuu!.
Babu hizo hazipatikani kwenye menu ya tigo.

Hizo ni ofisini tu
 
Hii haujiungi zinaingia zenyewe kila tarehe moja wa kila mwezi ni postpaid
 
Mtatoana roho[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Namshtua mkuu, Maana watu watamfata watalipia, halafu hawatopata wanachokitaka, Mwisho sio mzuri!!
Yah! Najua Mkuu, ila mpya ni hizo japo hazijawa updated kwenye mfumo.
 
Hii ni yangu ime top Jana . Mbona bado ipo vile vile. Au hayo maboresho yameanza Leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…