Tigo Kuweni wastaarabu

Johnsecond

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2010
Posts
1,076
Reaction score
211
Kwa nini tigo mnatutoza pesa huduma kwa wateja? Mimi ni mteja wenu nikitaka kuongea na mtoa huduma wenu lazima nilipe tsh 50 mbona ni uonevu huo? Au mnataka tusiombe msaada huduma kwa wateja?
 
Kweli wana tabia mbaya mie nashangaa iweje watoze pesa ya huduma kwa mteja?? Yaani hawa Tigo wameharibikiwa kweli siku hizi wamekuwa weeeeziiii weziiii tu mambo zao hovyo kabisa. Usiombe ukakopa hiyo sijui mia sijui mia mbili zao hizo msg utakazopata utajuta kwanini ulikopa kwakweli wajirekebishe Tigo mnapoteza customers wenu
 
Nilikuwa mteja loyal customer wa Tigo, ulikuwa mtandao wangu wa kwanza lakini kwa sasa nimetokea kuichukia sana tigo natamani hata kuitupa line yangu ya tigo ili nisitamani hata kuitumia. Kwanza wanakata kiasi kikubwa ukilinganisha na wanachotangaza, pili kila huduma unayotaka kwao wanakata pesa eg ukimtumia hata mzazi wako pesa wanakata asilimia 0.3% ya pesa uliotuma. Hii inamaana wanakuchaji mara mbili, sielewi kwa nini wanikate wakati nimenunua credit ambayo naweza kuitumia kwa jinsi ninavyotaka. Tigo acheni kutafuta pesa kwa nguvu namna hiyo muwajali na wateja wenu..nashauri makato haya wayaweke kwenye matangazo yao ili mteja awe amejiandaa kuliko kama ilivyo sasa...wazo langu kwa TIGO.
 

Taarifa: Wanakata asilimia 3% sio 0.3% kama ulivyosema. Mwisho wa taarifa.
 
mimi nawapenda ila kama wataendelea hivi watanipoteza mimi na jamaa zangu wote!
 
Jamaa sio wastaarabu, nilienda Sumbawanga nikakuta mawakala wote wa tigo pesa wanalalamika kuwa hawalipwi stahili zao na tigo na wanasema kuwa tigo ni wahuni, na kwa sasa ukienda sumbawanga kutafuta Tigo pesa hutopata mahala popote. Kila kitu wanakata pesa ndo maana jina la tigo linamaana mbaya sana mitaani, hahahhahaha. Ukiwa huna tsh50 huwezi wasiliana na mtoa huduma wao hata kama tatizo wamelisababisha wenyewe. Kwa nini msiwafuate tritel?
 
Watanzania tunaibiwa sana hasa kwenye huduma za kibenki na mitandao ya simu.
 
Lakini sitaki kulaumu sana huu ni wakati wenu tigo kujipanga na ku-win market yaliyolalamikiwa yafanyieni kazi mtaonesha ukomavu wa kibiashara na msiyafanyie kazi kimya kimya bali watu wote waelewe.
 
Sometime even us we have to Think, What is Tshs.50.00 kama umepata huduma nzuri? au usipate kwa Tshs. 50?
 
Mawasiliano shida hadi upige kama mara nne au tano ndio mtu anapatikana!!!!!!! na hiyo huduma ya wimbo wa anayekupigia ndiyo inaboa vibaya mno, wewe unaomba wimbo mmoja mtu akikupigia mara mbili au tatu atakuta nyimbo kibao ambazo hukuziomba na mbaya zaidi hata huzipendi, mfano wewe dini flani utasikia wimbo wa dini nyingine ambao hukuuomba! sijui tigo inaelekea wapi, wengine sisi ni wateja tangu inaitwa mobitel, ikaja buzz then tigo bado tumo tu, watatupoteza muda si mrefu hawa
 
Hawa jamaa hata huduma ya tigo niwezeshe, kwa mbwembwe itakuja meseji "umekopeshwa Tsh 1,200.00 naweza kupiga au kutuma sms kwenye mtandao wowote" hii ni huduma kwa wateja maalum, lakini ukitakakuangalia salio haionyeshi kuwa salio lako ni pamoja na hicho kiduchu walichokuongezea! Kama simu ilikuwa na shilingi 10/= salio litaonyeshwa hilo hilo! Hawaonyeshi kiasi walichoongeza! Aidha kuna wakati nilishinda Tsh 500,000.00 huo usumbufu wake sina hamu! Pesa nilipewa bila kusaini popote!! Hao ndio tiGO.... Mtandao unaopendwa saana na vijana hasa Intellectuals!!
 
And more worse uki2ma sms,iende isiende lazma ukatwe.Alafu hiv lazma ukope amount waliokupangia?kama ukikopa kutokana na shida zako,kwnn usiweze kumpgia wa mtandao tofauti?huu mkopo?wizi?riba 10%? Watz tujitazame upya!
 
Tigo Kimeooo! Mambo iko Airtel... Wanakuja kasi subirini muone! mtakufa kibudu na tigo yenu nyie tigo. Mliweza kuliteka soko sasa mmebweteka.
 
Sometime even us we have to Think, What is Tshs.50.00 kama umepata huduma nzuri? au usipate kwa Tshs. 50?
No bora lakini tigo ndio wanaoongoza kwa huduma kwa wateja zilizo mbaya harafu wanakulipisha.
 
Voda wanakupa nafasi nadhani tano kwa mwezi kuongea na mtoa huduma zaidi ya hapo unalipia pia. Lakini ni bora yao mpaka mara tano kama hujasolve tatizo lako ina maana uende kwao physically
 
Sometime even us we have to Think, What is Tshs.50.00 kama umepata huduma nzuri? au usipate kwa Tshs. 50?

Sio hivyo, ndugu. Wanakata kabla hata hujaunganishwa na mhudumu!! Kibaya zaidi, unaweza kusuburi kwa muda mrefu sana hadi unaweza kukata tamaa -- pesa imeliwa, huduma hujapata!!
 
Hakika hawa jamaa wezi sana, mi leo nimeamka simu yangu haiko hewani, nimepita kwa mtoa huduma wao ananiambia eti line yangu emexpire natakiwa ku -renew. Gharama za ku-renew ni shiling 500, nikamuuliza yule bwana inaamaana mnaniuzia line kwa lazima? hakuwa na jibu, kilichiniudhi zaidi ni pale aliponiamabia kuwa kumbukumbu zangu zote kwenye ile line yangu sitaweza kuzipata tena, huu ni upuuzi uliozidi kipimo, sina hamu nao tena
 
Karibuni AIRTEL, mimi nipo huku tangu 2005 na sijawahi kujuta. Hamieni, waambie na majirani wote wahamie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…