TIGO wamenitapeli? Hakikai sitokubali.

TIGO wamenitapeli? Hakikai sitokubali.

makilo

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2015
Posts
2,620
Reaction score
5,260
Kheri ya ijumaa kuu kwa wote.
Siku ya tarehe 23 mwezi wa 3,nilifanya malipo kwa njia ya mtandao nililipa ticket ya bus Dar to Mwanza.

Malipo yangu hayakufanikiwa nikawasiliana na huduma kwa wateja wakaniambia kuna tatizo la kimtandao kwa hiyo fedha zangu zitarudishwa baada ya siku 3.

Kila baada ya siku tatu nikawa nawakumbusha ikaanza story ya masaa 24 nitarudishiwa changu, nikaona niende Makao Makuu Makumbusho nikaambiwa wameshachukua taarifa zangu hivyo nitarudishiwa baada ya saa 24.

Nimekaa siku 2 nimewapigia wanasema mbona huku tumeshakurudishia? Jamani jamani jamani TIGO wamekuwa na huduma mbovu mbovu mno.

Nikarudi Tena makao makuu wakaniambia niwawie radhi pesa yangu bado inaonekana ipo kwao nikae baada ya siku 3 itakuwa mikononi mwangu. Juzi jumatano nikawapigia kuuliza Mana siku 3 zimekata nikaambiwa masaa 24 nisubiri nikabakia kucheka tu.

Leo nawapigia simu kwa number Yao ya 100 inapokelewa ila upande wangu si sikii chochote wamenipiga "MUTE" maana nikitumia simu ya mtu mwingine wanapatikana vizuri tu.

Wakuu nahitaji changu jasho langu sio vyema likapotea kirahisi rahisi.
 
Kheri ya ijumaa kuu kwa wote.
Siku ya tareh 23 mwezi wa 3,nilifanya malipo kwa njia ya mtandao nililipa ticket ya buss dar to mwanza.

Malipo yangu hayakufanikiwa nikawasiriana na huduma kwa wateja wakaniambia kunatatizo la kimtandao kwahiyo fedha zangu zitarudishwa baada ya siku 3.
Kila baada ya siku tatu nikawa nawakumbusha ikaanza story ya masaa 24 nitarudishiwa changu,nikaona niende makao makuu makumbusho nikaambiwa wamesha chukua taarifa zangu hivyo nitarudishiwa baada ya masaa 24.

Nimekaa siku 2 nimewapigia wanasema mbona huku tumeshakuludishia? Jaman jaman jaman TIGO wamekuwa na huduma mbovu mbovu mnooo.
Nikarudi Tena makao makuu wakaniambia niwawie radhi pesa yangu Bado inaonekana ipo kwao nikae baada ya siku 3 itakuwa mikononi mwangu.juzi juma 5 nikawapigia kuuliza Mana siku 3 zimekata nikaambiwa masaa 24 nisubili nikabakia kucheka tu.leo nawapigia simu kwa number Yao ya 100 inapokelewa ila upande wangu si sikii chochote wamenipiga "MUTE" maana nikitumia simu ya mtu mwingine wanapatikana vizuli tu.

Wakuu nahitaji changu jasho langu sio vyema likapotea ki rahisi rahisi.
Utaipata lakini kwa shida sana maana imeshapigwa hiyo..
 
Hivi huwa wanaipiga makao makuu au Hawa Hawa tunao ongea nao?
Customer Care imekuwa out sourced .. Nadhani walichukua Wakenya na iko Nairobi.. Hivyo hata ukifika pale HQ hakuna msaada mkubwa utapata
 
MAMBO MENGINE YA KUJITAKIA KABISA. BADO HATUJAFIKIA KIUFANISI KUFANYA MAMBO MENGI KWA NJIA YA DIJITARI, SIKU NYINGINE KAKATE STENDI MKUU
 
Customer Care imekuwa out sourced .. Nadhani walichukua Wakenya na iko Nairobi.. Hivyo hata ukifika pale HQ hakuna msaada mkubwa utapata
Mkuu mshana nimeifuatilia Sana hii pesa mpaka Ile Hali ya uvumilivu inafika kikomo.
Kama nitafika mpaka HQ kwa Mara nyingine Tena inamana naenda kuambulia masaa 24 Tena au 72 Kama mwanzo?
 
Back
Top Bottom