TikTok “inayotishia usalama wa taifa” yageuka kuwa chombo kizuri cha kushindania uchaguzi nchini Marekani

TikTok “inayotishia usalama wa taifa” yageuka kuwa chombo kizuri cha kushindania uchaguzi nchini Marekani

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
VCG111485321049.jpg
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Marekani, rais wa zamani wa nchi hiyo Donald Trump amefungua akaunti ya TikTok, ili kuwavutia wapiga kura vijana, na kufanya maandalizi kwa ajili ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Novemba mwaka huu nchini humo. Kabla ya hapo, Rais wa sasa Joe Biden pia alifungua akaunti ya TikTok mapema mwezi Februari mwaka huu.

TikTok ni mtandao wa kijamii wa video unaomilikiwa na Kampuni ya Bytedance ya China. Kutokana na teknolojia yake ya hali ya juu, mtandao huo umewavutia watumiaji milioni 170 nchini Marekani katika miaka michache iliyopita, ambayo ni nusu ya idadi ya watu nchini humo. Aidha, mwaka jana pato la TikTok nchini Marekani lilizidi dola bilioni 16 za Kimarekani. Baada ya hapo, baadhi ya wanasiasa wa Marekani waliinua fimbo yao, wakidai kwamba TikTok ina data nyingi za watumiaji, na “inatishia usalama wa taifa”, hivyo ni lazima “hatua kali” zichukuliwe. Lakini TikTok imeeleza kwamba inafuata sheria zote za Marekani, na kuahidi kuhakikisha usalama wa data, na hata inakubali kujiweka chini ya uchunguzi mkali wa serikali ya Marekani. Hata hivyo Marekani haitaki kuisamehe, na hadi sasa imetoa amri ya kuipiga marufuku mara mbili.

Wakati serikali ya Marekani inapiga kampeni ya kuimaliza TikTok, wanasiasa wa nchi hiyo wamefungua akaunti zao kwenye mtadano huo bila ya kusita, kwani wanajua TikTok ni chombo kizuri cha kuwavutia wapiga kura katika uchaguzi.

Habari zinasema kwenye video ya kwanza iliyotolewa na Trump baada ya kufungua akaunti kwenye TikTok, Mkurugenzi Mtendaji wa Michezo ya Fainali ya Mapigano (UFC), Dana White, ambaye aliandamana na Trump, alisema: “Rais sasa anatumia TikTok.” “Ni heshima yangu.” Trump akajibu. Licha yake, Kamati yake Kisiasa “Make America Great Again” pia imejiunga na TikTok, ili kumsaidia kuwavutia wapiga kura vijana.

Hata hivyo, wakati Trump alipokuwa madarakani, aliitendea vibaya mtandao huo wa TikTok. Mwaka 2020, alisaini amri ya kuipiga marufuku TikTok, lakini mwishowe alishtakiwa na TikTok, na kufuta amri hiyo kutokana na hukumu ya mahakama.

Kama Trump, Rais Biden pia anaipenda na kuitendea vibaya TikTok. Alifungua rasmi akaunti ya TikTok Februari lakini miezi miwili baadaye, alisaini rasmi muswada wa kulazimisha ByteDance kuacha TikTok, ama sivyo, TikTok itapigwa marufuku kabisa nchini Marekani.

Marekani inadai kuwa inaheshimu uhuru wa kutoa maoni, na ni soko huria zaidi duniani. Lakini katika suala la TikTok ambayo ni APP halali iliyoanzishwa kwa kufuata sheria na utaratibu wa nchi hiyo, imeacha maadili yote, na kufanya kama jambazi anayetaka kuiba kitu kizuri cha watu wengine.
 
China piga kazi.

Tuko pamoja, tunawaunga mkono

Ila hebu na nyinyi watendeeni haki Waislamu wa Uighur. Kuna baadhi ya mambo mnawakandamiza sana. Kwa mfano uhuru wao wa kuabudu mnauminya.

Mkiweza kuwatendea haki Waislamu wa Uighur mtaheshimika katika ulimwengu wa waislamu duniani, ila mkiendelea kuwaminya hamtapata heshima ambayo mnastahili.
 
China piga kazi.

Tuko pamoja, tunawaunga mkono

Ila hebu na nyinyi watendeeni haki Waislamu wa Uighur. Kuna baadhi ya mambo mnawakandamiza sana. Kwa mfano uhuru wao wa kuabudu mnauminya.

Mkiweza kuwatendea haki Waislamu wa Uighur mtaheshimika katika ulimwengu wa waislamu duniani, ila mkiendelea kuwaminya hamtapata heshima ambayo mnastahili.

Umewahi kujiuliza kwa nini wanazungumziwa sana Uyghurs pekee na vyombo vya habari na sio waislam wengine waliopo China ?
 
Umewahi kujiuliza kwa nini wanazungumziwa sana Uyghurs pekee na vyombo vya habari na sio waislam wengine waliopo China ?
Kwa sababu ni Jimbo linatoleta chokocho za kutaka kujitenga na china kupitia asili yao, dini inatumiwa kama pazia tu kuficha makusudi na harakati zao za kisiasa. Uyghurs ni Wachina wenye asili ya Uturuki, hadi Sasa hawakubali kuwa sehemu ya China hivyo wanataka kuunda taifa lao. Ni kama ilivyokuwa Chechniya huko urusi, wakurdi huko Iraq na Uturuki, (na hivi punde wazanzibari hapa Tanzania, ingawa harakati za wazanzibari ni hafifu ukilinganisha na hao wengine niliowataja).
 
Tik tok ni muhanga tu katika vita ya kiuchumi baina ya US and China, but the good news ni kwamba kwa level tik tok waliyofikia, ni ngumu kuizuia.
TikTok imepigwa ban na kuzuiwa karibu dunia nzima.

Kama unafikiri kutoizuia ni good news, jiulize ni kwa sababu gani TikTok inayotumika kimataifa ukienda China huipati bila VPN?

Yaani, aliyeunda TikTok yeye mwenyewe hataki itumike nyumbani kwake. Unafikiri ni kwa sababu gani?

Na hilo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
 
TikTok imepigwa ban na kuzuiwa karibu dunia nzima.

Kama unafikiri kutoizuia ni good news, jiulize ni kwa sababu gani TikTok inayotumika kimataifa ukienda China huipati bila VPN?

Yaani, aliyeunda TikTok yeye mwenyewe hataki itumike nyumbani kwake. Unafikiri ni kwa sababu gani?

Na hilo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
Leta ushahidi hapa ya kuwa Tik Tok haitumiki China bila VPN kwanza.
 
Leta ushahidi hapa ya kuwa Tik Tok haitumiki China bila VPN kwanza.
TikTok haijawahi kuruhusiwa kabisa kutumika China [bara]. Hong Kong, ilipigwa ban mwaka 2020. Wachina wanatumia Douyin ambayo inafanana na TikTok, ila ipo chini ya udhibiti mkali wa serikali.

Turejee kwenye swali: Unafikiri ni kwa sababu gani TikTok haipatikani nchini China?

tktk.png

 
TikTok imepigwa ban na kuzuiwa karibu dunia nzima.

Kama unafikiri kutoizuia ni good news, jiulize ni kwa sababu gani TikTok inayotumika kimataifa ukienda China huipati bila VPN?

Yaani, aliyeunda TikTok yeye mwenyewe hataki itumike nyumbani kwake. Unafikiri ni kwa sababu gani?

Na hilo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
Douyin ndio hiyo hiyo TikTok ilianza Douyin mainland China ndio ikafuata TikTok world wide
 
Douyin ndio hiyo hiyo TikTok ilianza Douyin mainland China ndio ikafuata TikTok world wide
Douyin na TikTok ni za kampuni moja na zinafanana kimuonekano lakini ni tofauti kimuundo na hazishirikiani kwenye data na maudhui.

Mfano: uki-search kwenye Douyin maudhui ama accounts zilizopo TikTok hutozipata kwenye Douyin na kinyume chake ni vivyo hivyo kwa sababu hazishirikiani kwenye suala la user data.

Huo utofauti wa kimuundo unazifanya ziwe apps mbili tofauti ama zilizotengana.

Kuna mdau amesema hapo kwamba "TikTok ni muhanga tu katika vita ya kiuchumi". Swali langu; ni kwa sababu gani TikTok inayopatikana kimataifa haipatikani nchini China?

Hilo nalo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
 
Douyin na TikTok ni za kampuni moja na zinafanana kimuonekano lakini ni tofauti kimuundo na hazishirikiani kwenye data na maudhui.

Mfano: uki-search kwenye Douyin maudhui ama accounts zilizopo TikTok hutozipata kwenye Douyin na kinyume chake ni vivyo hivyo kwa sababu hazishirikiani kwenye suala la user data.

Huo utofauti wa kimuundo unazifanya ziwe apps mbili tofauti ama zilizotengana.

Kuna mdau amesema hapo kwamba "TikTok ni muhanga tu katika vita ya kiuchumi". Swali langu; ni kwa sababu gani TikTok inayopatikana kimataifa haipatikani nchini China?

Hilo nalo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
Asante kwa elimu hii
 
Kwa sababu ni Jimbo linatoleta chokocho za kutaka kujitenga na china kupitia asili yao, dini inatumiwa kama pazia tu kuficha makusudi na harakati zao za kisiasa. Uyghurs ni Wachina wenye asili ya Uturuki, hadi Sasa hawakubali kuwa sehemu ya China hivyo wanataka kuunda taifa lao. Ni kama ilivyokuwa Chechniya huko urusi, wakurdi huko Iraq na Uturuki, (na hivi punde wazanzibari hapa Tanzania, ingawa harakati za wazanzibari ni hafifu ukilinganisha na hao wengine niliowataja).
.....alafu wakishajitenga wataanza kutumiwa na maadui wa china kuleta chokochoko china!
 
Douyin na TikTok ni za kampuni moja na zinafanana kimuonekano lakini ni tofauti kimuundo na hazishirikiani kwenye data na maudhui.

Mfano: uki-search kwenye Douyin maudhui ama accounts zilizopo TikTok hutozipata kwenye Douyin na kinyume chake ni vivyo hivyo kwa sababu hazishirikiani kwenye suala la user data.

Huo utofauti wa kimuundo unazifanya ziwe apps mbili tofauti ama zilizotengana.

Kuna mdau amesema hapo kwamba "TikTok ni muhanga tu katika vita ya kiuchumi". Swali langu; ni kwa sababu gani TikTok inayopatikana kimataifa haipatikani nchini China?

Hilo nalo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
Utofauti wa Douyin na TikTok ni suala la kisheria zaidi la serikali ya China ni sio utofauti wa kimuundo Douyin imekuwapo China ni muda mrefu sana unless unataka sheria za China zi apply kwenye TikTok sijui huo uhuru wa content kama utapatikana tena TikTok.

China walifanya jambo la maana sana sheria zao wakaacha zitumike huko huko Beijing sisi wengine tutaamuliwa na sheria zetu na kipi tunataka kukiona na kipi hatutaki kukiona na sio sheria za serikali za China zituchaguliwe.
 
Douyin na TikTok ni za kampuni moja na zinafanana kimuonekano lakini ni tofauti kimuundo na hazishirikiani kwenye data na maudhui.

Mfano: uki-search kwenye Douyin maudhui ama accounts zilizopo TikTok hutozipata kwenye Douyin na kinyume chake ni vivyo hivyo kwa sababu hazishirikiani kwenye suala la user data.

Huo utofauti wa kimuundo unazifanya ziwe apps mbili tofauti ama zilizotengana.

Kuna mdau amesema hapo kwamba "TikTok ni muhanga tu katika vita ya kiuchumi". Swali langu; ni kwa sababu gani TikTok inayopatikana kimataifa haipatikani nchini China?

Hilo nalo ni kwa sababu ya vita ya kiuchumi kati ya US na China?
Vita ya kiuchumi inakuja pale marekani wanapo lazimisha wauziwe huo mtandao maana vitu vyote walivyotaka kutoka kwa TikTok walipewa ikiwemo uhifadhi wa data hapo hapo U.S
 
Back
Top Bottom