TikTok yapewa muda hadi Januari 19, 2025 iwe imeuza hisa zake kwa mwekezaji wa Marekani au ifungiwe

TikTok yapewa muda hadi Januari 19, 2025 iwe imeuza hisa zake kwa mwekezaji wa Marekani au ifungiwe

Mahakama ya Rufaa ya D.C. imetangaza uamuzi wa kuunga mkono sheria inayotaka ByteDance, kampuni mama ya TikTok kutoka China, kuuza hisa zake za programu hiyo ifikapo Januari 19, 2025, la sivyo itakabiliwa na marufuku kote Marekani.
View attachment 3171068
Sheria hiyo, inayojulikana kama Protecting Americans from Foreign Adversary Controlled Applications Act, imeelezwa kuwa imelenga moja kwa moja kulinda usalama wa taifa.

Hata hivyo, TikTok imepinga hatua hiyo, ikidai inakiuka haki ya Kifungu cha Kwanza cha Katiba ya Marekani (First Amendment).

Mahakama, kwa upande wake, imesisitiza kuwa ushahidi wa serikali ya Marekani kuhusu hatari za kiusalama una uzito mkubwa, ikizingatia ushawishi wa programu hiyo duniani na uwezekano wa matumizi mabaya.

Soma, Pia: Bunge la Marekani lapitisha Muswada wa Sheria ya kuifungia TikTok
==
The U.S. Court of Appeals for the D.C. Circuit has upheld a law requiring TikTok's Chinese parent company, ByteDance, to sell its stake in the app by January 19, 2025, or face a nationwide ban.

The decision supports the Protecting Americans from Foreign Adversary Controlled Applications Act, which the court deemed narrowly tailored to address national security risks.

While TikTok argues the law infringes on First Amendment rights, the ruling emphasised the app's global reach and potential for misuse, citing the U.S. government's persuasive evidence.
Hapo usa anataka mmiliki awe usa citizen ili wakitaka taarifa flan kweye ujasusi wazipate ila china sio mjinga hivyo.
 
Ni mtandao pekee ambao Zayuni hajauweka mkononi. Sasa anatumia machinery ya serikali ya Marekani ambayo iko viganjani mwake kuuweka mkononi.
Hii ndo komment ya maana kabisa kwenye hii thread watu wanalichukulia hilo kwa wepesi sana ila mtandao wenye watumiaji wengi halafu usa hana access nao hilo ni bom kwake
 
Mtandao wa hovyo, lkn Marekan nayenyewe iache soko huria liamue, au waanzishe TikTok yao nasio kufungia mitandao. Hivi Tz ikifungia watsp, X, insta wakasema sio salama kwa nchi yetu itakua sawa?.
Jombaa mfano gani huo, Tz mnaamuliwa tu
 
Wakati wenzetu wanapigania USALAMA wa nchi yao. Hapa kwetu serikali inapambana kudukua mawasiliano ya raia wake ili kulinda usalama wa taifa
Ukipata muda nenda Google then search Edward Snowden.
 
Back
Top Bottom