TIME IS A MYTH IT DOESN'T EXIST

hitler2006

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2014
Posts
489
Reaction score
454
wadau kwa muda nimekua nikijiuliza mini maana ya muda..
nani alipanga sec,min,and hours nakosa jibu kabisa..
kwa mtazamo wangu...mpangilio wa nini cha kufanya ndo ulileta uwepo wa intervals kati ya tukio moja na jingine ...na hiyo interval ndo huitwa muda....BILA KUWEPO MATUKIO YENYE KUPEANA NAFASI HAKUNA MUDA kwa hiyo MTU anayekaa bila kufanya kazi hapotezi muda kwa sababu hakuna tukio naada ya tukio analofanya..KARIBUNI KWA MAONI ZAIDI
 
Naona inakufunza kuwa mwanafalsafa, hongera!
Swali lako la kwanza: ungekuwa umesoma Physics ingesaidia kukupa majibu kuhusu atomic time au hata astronomical time. Lakin si mbaya unamlengo sawa na akina Lamport kwenye theory zao za Logical Time
 
Huwezi kuumiliki muda.
 
Usichanganye saa na muda,
saa inapima muda,muda ni dhana,hayo manambanamba ni man made tu yasikuchanganye.
Muda ni dhana halisi na ipo.
muda ni uwepo na uwepo unatengenezwa na nafasi(space),nikisema space nieleweke hivi ni sehemu/eneo ambapo kitu kinaweza ku-exist au kitendo kinaweza kutokea(is the place where something can exist and action can happen).
na kwenye space ndio unaweza kupima muda/muda upo.. hivyo the way space still is the way time exist so muda ni uwepo.
nimejibu kwa uelewa wangu na hii dhana huwa inapingana na hiyo ya kusema kama hakuna matukio ya kupeana nafasi basi hakuna muda! kwanini..?
kwasababu muda ni uwepo hata kabla ya hayo matukio kutokea muda/uwepo upo kabla.
na kwa hii dhana muda hauendi mbele wala kurudi nyuma hili nimeshawahi kulizungumzia humuhumu.
 
Kuna tofauti kati ya saa na muda
Saa inaundwa na dakika na sec ila muda ni past present and future muda ulikuwepo ila saa ililetwa tu ili kudetermine muda
 
Ni kweli una hoja, umefikiria nje ya box, hiyo inaitwa hypothesis unachopaswa ni kuiongezea nyama, kuipa hoja zilizoshiba. Kama huna kitu cha kufanya haupotezi muda, ila muda unaenda tu bila ya wewe kufanya kitu. Ni sahii kabisa watu wasio na kitu cha kufanya muda kwao ni very irrelevant, hawaufuati na hawashughuliki nao. Kimsingi wako huru sana na wanafurahia maisha bila yakuwa na fedha (hawazezi kupata fedha bila ya kufanya kazi na kufuata muda labda u-bet). Mara nyingine najiuliza maswali mengi sana, huwa nahisi maisha ya kutafuta fedha yametuweka utumwani, tumekua watumwa na maisha yetu wenyewe. Hii nakubaliana na Dalai Lama kama ninavyo quote hapa chini:

“Man. Because he sacrifices his health in order to make money.
Then he sacrifices money to recuperate his health.
And then he is so anxious about the future that he does not enjoy the present;
the result being that he does not live in the present or the future;
he lives as if he is never going to die, and then dies having never really lived.”
 
Naona inakufunza kuwa mwanafalsafa, hongera!
Swali lako la kwanza: ungekuwa umesoma Physics ingesaidia kukupa majibu kuhusu atomic time au hata astronomical time. Lakin si mbaya unamlengo sawa na akina Lamport kwenye theory zao za Logical Time
Mkuu utofauti kati ya atomic time na astronomical time ni upi?
 
Muda unapatikana pakiwa na mabadiliko tu. Mabadiliko yakisimama na muda haupo. Ukiweza ku experience uwepo "being" katika hii dunia basi hata muda utaona ni uongo. Ili kuweza kuendana na changes ndio maana akili ikatengeneza muda. Nini tofauti kati ya alhamisi na jumapili? Can u feel it leo ni tarehe 15 au 21? Can u feel leo ni jumanne? Ukifugiwa ndani unconscious for 2 days then unatoka huna kumbukumbu ya muda unaweza kusema muda huo ni saa ngapi na ni siku gani?
Ni hayo tu........

Nisije kuenda mbali
 
Unapo kaa tu bila kufanya kazi hupoteza muda mwingi tu
maana katika mwili wako kuna matukio ya kukua kwa chembe chembe hai.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…