Timu ya Kaizer Chiefs yamsajili Kotei

Hauko timamu wewe, kama unaweza ukalinganisha kaizer chiefs na Simba basi ndio mana Taifa Stars inacheza vile ilivyocheza juzi na kufungwa
Simba ni quarter finalists wa klabu bingwa Africa, Kaizer Chiefs hawashiriki kombe lolote la kimataifa mwaka huu. Malengo hapo lazima yatakuwa tofauti. Kwa kusema hivyo sina maana ya kuibeza Kaizer Chiefs, ni moja kati ya klabu bora kabisa SA na ina facilities nzuri sana.

Ila ukweli unabaki pale pale Kotei ana mapungufu sana kwenye upigaji wa pasi, hasa pasi ndefu, ufanisi wake ni mdogo sana, na kwa level ya Simba na walipo kwa sasa anakuwa anakosa kitu cha msingi sana katika uchezaji.
 
Ha ha ha sina neno zaidi ya kusubiri results za mbrazil na msudani
 
Kotei ndio mlimchagua kiungo bora akiwashinda Mkude,Chama,Haruna,ilikuwaje mchezaji mbovu ndio anakuwa kiungo bora ?
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli. Kotei ni bonge la mchezaji ambaye muda mfupi Simba tutajuta kumuacha. Anakaba vizuri sana, ni kiraka anacheza nafasi zaidi ya tatu uwanjani ana mapafu ya mbwa, ameshazoea mfumo wa Simba pamoja na kucheza kwenye viwanja vibovu mikoani. Sasa huyo Mkude wenu ni mzuri akiwa na mpira tu na vipasi vyake vya square kwenye kupora mipira ambayo ndio sifa ya kiungo mkabaji Mkude yupo chini ukilinganisha na Kotei.

Kotei ni aina ya wachezaji ambao ni mashujaa wasioimbwa kwa sababu wao hawana mbwembwe/udambwidambwi zaidi ya kufanya kazi yao kwa ufanisi uwanjani vizuri ndio maana leo mashabiki maandazi wanaona Kotei kuachwa ni sawa tu.

Simba kufika robo fainali ni baada ya wachezaji wengi kukaa pamoja miaka miwili na zaidi tangu usajili wa 2016/2017. Ilipaswa kuongeza wachezaji kwa uangalifu bila kuvunja uti wa mgongo wa timu. Hata kama ni maingizo mapya yangeingia taratibu ndani ya miaka miwili au mitatu. Lakini la ajabu leo wachezaji muhimu Okwi, Juuko, Kotei na Niyozima wanasemekana wanaoondoka kwa pamoja. Je kocha na viongozi wanaelewa kuwa mpaka timu ipate muunganiko wa wachezaji wapya na wa zamani inachukuwa muda?
 
Unajua sisi wapenze wa soka Tz tuna changamoto kubwa sana! Kuna wakati ni lazima tuwe tunazungumzia soka katika uhalisia wake bila kujikita katika ushabiki wa Simba na Yanga! Huu ni upofu wa fikra kama kila kitu tunakichambua katika mizania ya Simba na Yanga!
Binafsi licha ya mahaba niliyo nayo kwa Simba ila usajili uanafanyika sasa unanipa mashaka!
Ni ngumu kuamini kuwa kocha alikuwa hamtaki Kotei ili hali alikuwa anacheza kwa ufanisi katika mechi nyingi (zaidi ya 90) Nakumbuka katika baadhi ya Mechi za Mwisho Kotei alitolewa dk ya 80 hadi Mtangazaji wa Redio alikiri kuwa hajawi kuona Baba Mchungaji Kotei akitolewa nje!
Kotei amefanya kazi kubwa Simba hakustahili kuachwa bali kuuzwa kwa faida!
Hivi hawa Wabrazil ikitokea wameshindwa(Mungu epusha mbali) tutasema nini kumwacha Kiungo Bora aende hivihivi.Hii inataka kutokea kama kipindi kile OMOG alitaka kummaliza Mkude1 au kama ambavyo tumemmaliza Juuko!
Kuna watu wanabisha bure usajili inaofanya Simba safari hii ni kamari! Ila Mungu ni Mwema!
 
Kotei ndio mlimchagua kiungo bora akiwashinda Mkude,Chama,Haruna,ilikuwaje mchezaji mbovu ndio anakuwa kiungo bora ?
Unalinganisha machungwa na maandazi, na pia waliochagua ni wachezaji wenyewe, sio kocha.
 
Usajili ni kama wewe unavyofanya mipango yako, inaweza ikaonekana mizuri lakini isikufikishe kule unakotaka, lakini hitaji la kuwa na mipango linabaki palepale.

Simba wangeweza kumbakisha Kotei na pengine asingefanya vizuri msimu unaokuja kwa sababu mbalimbali kwa sababu tu he is human. Tuwaache viongozi wa Simba wafanye kazi yao ya kukisuka kikosi.
 
haya wote tunasubiri
 
Wanadai jamaa alishacheza na wakina Neymar, Cassemiro na Coutinho, inawatosha sana hiyo sifa mkuu 😃.
Hapana, hiyo ni added advantage, kilichowafurahisha Simba ni record yake (statistics). Na hiyo inatumika kila mahali duniani.
 
Hapana, hiyo ni added advantage, kilichowafurahisha Simba ni record yake (statistics). Na hiyo inatumika kila mahali duniani.
Lete record yake mkuu, maana hao jamaa aliocheza nao wako mbali sana kimafanikio.
 
Kashata game na Algeria nikaona ni muda sasa wa kutengeneza vijana wetu. .poor performance wakamtoa 45 minutes. .
 
Hapana, hiyo ni added advantage, kilichowafurahisha Simba ni record yake (statistics). Na hiyo inatumika kila mahali duniani.
Record ya kucheza ligi ya India ??
Aje kucheza viwanja kama Mkwakwani,Namfua Singida
 
Lete record yake mkuu, maana hao jamaa aliocheza nao wako mbali sana kimafanikio.
Hata uki-Google unapata profile yote, siku hizi kila kitu kipo kiganjani huhitaji kwenda library.
 
Mkuu pamoja na usajili mpya, haruna na okwi ni watu wanaotakiwa kubaki ili tufanye zaidi ya msimu ulioisha.
 
Record ya kucheza ligi ya India ??
Aje kucheza viwanja kama Mkwakwani,Namfua Singida
Huyo mchezaji amekuja Simba pia ana malengo yake, na malengo yake sio kucheza Mkwakwani tu bali ni kuonekana duniani atakapocheza kwenye champions league ambapo kuna viwanja vizuri na bora zaidi.
Tunao wachezaji wengi sana na wazuri wanaoweza kucheza kwenye viwanja vya vumbi na kupata matokeo, ndio maana tumemsajili beki wa Singida United na Lipuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…