Timu zilizokuwa zinapeleka ofa mezani Yanga SC sasa zitakwenda Simba SC kuwania saini ya Saidoo Ntibazonkiza

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425

Timu kubwa kama Kaizer Cheaf na nyingine zilizokuwa zinashusha ofa kwa Fistoni Kalala Mayele lazima zitakwenda kugonga hodi kwenye milango ya Simba SC.

Kutokana na kiwango cha Saidoo Ntibazonkiza Maestro kabisa lazima Simba SC walambe OFA nono kutoka kwa mshambuliaji mwenye jumla ya magoli kumi na tano(15).

NALIA NGWENA nitasikitika sana endapo kiungo Maestro Saidoo Ntibazonkiza kukosa timu nje ya nchi.

Nawasilisha hoja.
 
Japo Mimi ni Simba 🦁 ila saido kufunga Gori tano Kwa timu dhaifu ya Police 🚓 Tanzania siungi mkono hoja yako....
Hizo Gori angezifunga kwenye timu zenye ushindani sio vibonde wa NBC PREMIER LEAGUE

Saido ni mchezaji pekee mkweli hajadanganya UMRI wake (36) years 😊😊😊😊😊😊😊
 
NAKAZIA
 
Hamuamini Mayele ananyang'anywa tonge mdomoni ila mnasahau Saidoo alitupia 3 mechi ya kwanza tu alipojiunga na Simba. Mechi ya mwisho kabla hii ya Polisi alitoa assist kama sikosei 2 au 3 zile goli za Sakho zilitokea kwake.

Binafsi nilikuwa sipendezwi na jinsi alivyokuwa anapoteza mipira sana katika mechi nyingi ila mechi yake ya kwanza alipojiunga na Simba na hizi mbili za mwisho ameonyesha kiwango kikubwa sana. Takwimu zake zinatisha na nadhani anakwenda kuwa mfungaji bora na pia mchezaji bora msimu huu. Takwimu binafsi zinambeba.
 
Hujui unachoongea mkuu, saido ana miaka mingapi
 
saido ataendelea kuwa simba awanyandue humuhumu,huko nje mpelekeni mayele
 
Sawa lakini hayo makapu ya magoli Kwa mechi Moja ni noumer....

Mechi ya Jana haikua ya ushindani mkali na ndio maana akaweza kutupia goli tano....
 
CV ya Saido ni kubwa mno, ukilinganisha na Mayele au mchezaji yeyote NBC league. Saido kwenye umri wa miaka 36 sasa hivi anamalizia football career yake Tanzania. Akitoka hapa kwetu atarejea kwao Burundi. Ameshacheza ligi kubwa duniani ikiwemo ligi kuu Ufaransa, amecheza UEFA champions league, amecheza uarabuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…