Timu zilizoongoza kwa mapato ya mlangoni 2020/21 Vpl na Fdl hizi hapa

Kubali tu mashabiki wa Simba wanashughulika na Yanga zaidi kuliko mashabiki wa Yanga kushughulika na Simba..kitaalam hii inaitwaje?
Haa wapi,Simba tuko bize na kuongeza mikataba minono kwenye club yetu.juzi tumeongeza dili la Air Tanzania na jana Emirates Aluminium & Glass Co.Ltd.
 
Simba lazima alikuwa na mapato mengi sababu ya CAFCL
 
Duh akili za Kibashite hizi
 
Takwimu hizi zinatia shaka si kwa timu moja tu bali kwa timu zote. Mfano, mashabiki 141,681 wa Yanga kwa mechi 19 za nyumbani ni sawa na wastani wa mashabiki 7457 kwa kila mechi, na mashabiki138,518 wa Simba kwa mechi 19 za nyumbani ni sawa na wastani wa mashabiki 7290 kwa kila mechi. Je, wastani huu ndio hali halisi ya mahudhurio ya mashabiki pale Kwa Mkapa au Uhuru? Hilo swali nawaachia

 
ukiacha mechi ya simba na yanga ambayo mara nyingi huingiza mashabiki wengi, mechi zingine ni mara chache sana hizi timu (yanga na simba) kuzidisha mashabiki 7000 katika mechi zao.
 
Watoto wa juzi wameaminishwa Simba ndio timu kubwa TZ, record zinawakataa wanakaza vichwa.
 
Kama vipi mzee Bakhresa afumue pale azam complex aanzishe kiwanda hata cha juice.

Ila nadhani changamoto ya azam fc ni kucheza kila mechi yao ya ligi usiku. Hii inamkosesha wahudhuriaji wengi azam complex.
 
Simba ndio iliyoingiza pesa nyingi msimu uliopita kwa Mkapa.

Ligi ya TPL yanga walituzidi Tsh, millioni 57 tu.

Hapo pesa za kiingilio cha mechi za Simba za Club Bingwa Afrika kuanzia hatua ya mtoano hadi makundi hadi robo fainali haijawekwa.
Hebu mtuwekee na hizo tuone nani kaingiza pesa nyingi kwa Mkapa msimu uliopita.

Hii ndio Simba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…