Tips ndogondogo za usalama uwapo nyumbani kwako

Tips ndogondogo za usalama uwapo nyumbani kwako

Braza Kede

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2012
Posts
3,840
Reaction score
6,844
Katika uzi huu tupia dondoo mbalimbali za kiusalama za kuzingatia katika mazingira ya nyumbani.

- Usilale na mitungi ya gesi ndani, tafuta sehemu nje ya nyumba uweke huko.

-Usiache nyaya za umeme zikiwa uchi, si salama.

- Weka vitu vyenye ncha kali kama visu, misumari, spoke, mbao au mabati yaliyotumika n.k kunakohusika, mfano kisu kikae jikoni, gereji au stoo.

- Hakikisha kuna mlango wa dharura unaokuwezesha kutoka kwenye matukio ya dharura kama moto, wizi nk.

- Hakikisha watoto wadogo (kama wapo) wanakuwa na uangalizi wa mtu mzima au mwenye uelewa kuweza kufuatilia nyendo zao na kuwaepusha na mienendo hatarishi.

- Hakikisha unakuwa na uelewa wa watu wanaofika hapo nyumbani kwako. Kumbuka kuwa mara nyingi wezi/majambazi wanakuwa sio watu wa mbali bali ni watu wanaopafahamu hapo kwako na aghalabu wanaweza kuwa wanashinda hapo kwako.

-Hakikisha unawafahamu wanaofanya kazi mbalimbali hapo kwako na kujiridhisha ninwatu safi. Hawa ni kama mafundi ujenzi, mafundi TV, mafundi wa matenki, mafundi bomba n.k.

- Kama kuna mashimo makubwa yaliyo wazi hakikisha yanazibwa ili watu wasitumbukie humo au kuwa mazalia au maficho ya wadudu hatarishi kama nyoka, mijusi n.k.

Tuendeleze kupeana tips wakuu....
 
Sio nyumba ya kupanga, hivi vyumba vya kupanga uweke mtungi wa gesi nje, hata ukitoa ile ya kuwashia. Wahuni watakuja na vyao,

Kwa nyumba binafsi inakuwa rahisi sana, mtu anakuwa anaandaa mazingira rafiki
 
Sio nyumba ya kupanga, hivi vyumba vya kupanga uweke mtungi wa gesi nje, hata ukitoa ile ya kuwashia. Wahuni watakuja na vyao,

Kwa nyumba binafsi inakuwa rahisi sana, mtu anakuwa anaandaa mazingira rafiki
Hata nyumba yako binafsi mitungi ya Gas ijengewe kijumba au container, jua na mvua si rafiki pia.
 
Hata nyumba yako binafsi mitungi ya Gas ijengewe kijumba au container, jua na mvua si rafiki pia.
Kabisa, tena itakiwa iwe nje ya nyumba unayoishi.

Pia ujenzi uwe wa tofauti kidogo hasa kwenye jiko
 
Usalama wa kwanza ni chakula, hakikisha una chakula cha kutosha kwenye stoo yako, hili ni muhimu sana. Jingine(Kwa wenye nyumba zao) hakikisha una maji ya kutosha kwenye Tanks zako za maji halafu pia hakikisha una maji ya kisima, hakikisha pia una idea kuhusu umeme mfano kufunga soketi za umeme, kujua main switch Nini nk. Kwa usalama wako na familia yako hakikisha una pesa benki, kwenye laini za simu na nyumbani pia kuwe na chimbo lako la kuweka pesa na mwisho hakikisha nyumba yako hasa ndani kumepangika vizuri sana na kusiwe na makorokoro mengi. Zingatia haya utakuja kunishukuru pakitokea Sintofahamu kadhaa.
 
Usalama wa kwanza ni chakula, hakikisha una chakula cha kutosha kwenye stoo yako, hili ni muhimu sana. Jingine(Kwa wenye nyumba zao) hakikisha una maji ya kutosha kwenye Tanks zako za maji halafu pia hakikisha una maji ya kisima, hakikisha pia una idea kuhusu umeme mfano kufunga soketi za umeme, kujua main switch Nini nk. Kwa usalama wako na familia yako hakikisha una pesa benki, kwenye laini za simu na nyumbani pia kuwe na chimbo lako la kuweka pesa na mwisho hakikisha nyumba yako hasa ndani kumepangika vizuri sana na kusiwe na makorokoro mengi. Zingatia haya utakuja kunishukuru pakitokea Sintofahamu kadhaa.
Sisi wa chumba kimoja ndoo za maji, jiko la mkaa humohumo,



ngoja tuchill tusubiri yatukute
 
Back
Top Bottom