Titus Amigu: Maneno uchawi au mchawi kwa dhana za Kiafrika hayastahili kuwamo kwenye Biblia

Asante sana kwa hilo. Hata mimi kwa kusikiliza mafundisho yake redioni nimeona hilo kwamba anaona kuwa uchawi hauna uhalisia yaani haupo na yanayotendeka ni ujanja ujanja tu au mazingaombwe. Mazingaombwe ni tofauti sana na uchawi, japo yapo mazingaombwe yanayofanywa kwa msaada wa nguvu za giza.

Nilikuwa mkoa flani padre mmoja kijana sana akiwa na miezi michache ya upadre akahubiri na kukemea sana wote wanaoamini katika uwepo wa uchawi. Alikuwa akisema; watu wanalala kwenye hizi nyumba zetu zilizojaa panya halafu wanaamka asubuhi wametafunwa miguu au wana chale mwilini zinazotokana na kuumwa na panya halafu wanasema ni wanga wamewachanja chale. Akiongea mengi na watu niliokaa nao benchi la nyuma walikuwa wakicheka na kusema huyu padre hajui kitu, hayajamkuta, amekulia wapi?

Mapadre wengi pia hawaamini uwepo halisi wa shetani na kazi zake. Wanafikiri shetani ni kielelezo tu kinachotumika kuelezea uovu. Na wengi wa mapadre hufikiri kuwa Mungu ni nadharia tu. Niishie hapo kwa sasa.
 
Naweza nikaipataje?
 
Unakuta hilo lipadri ndio CHAWI KONKODI

Hapo anazuga tu
 
Natoa rai kwa wana JF wenzangu, yanapotokea maandiko kama haya ambayo yanahitaji "critical thinking" basi tuwe critical thinkers kweli na tuache uvivu wa kusoma na kutafakari. Inashangaza baadhi ya comments mpaka unajiuliza anaetoa comment amesoma kweli andiko lote akalielewa na kulitafakari? Mfano mdogo tu hivi kupitia andiko hili ni kweli Fr. Titus hakubali kwamba uchawi upo? Tuache uvivu wa kusoma, naamini JF ni darasa, tukilitumia vizuri linatuelimisha.
 
Ukiacha vitabu vyake, Kuna mada zake kadhaa kule facebook ameeleza vizuri sana na mengi sana kuhusu huu tunaoita uchawi, matukio yanayofahamika kuwa ni uchawi, magonjwa mbalimbali yanayofikiriwa na kuwa ni uchawi. Amechambua mengi sana kule waweza ingia huko ukajifunza
 
Tembelea catholic bookshops hasa kubwa unaweza kuipata.

Mimi niliwahi kuiona pale st joseph cathedral bookshop dsm. Na catholic bookshop ya mwanza pale jirani kanisa kuu nadhani wanayo.
Ahsante nitafanya hivyo
 
Kuna msemo Wahenga walisema '' Kusoma kwingi huondoa Maarifa'. Hawa Ma-Padre wamesoma sana theories za Theology, Phylosophy na Psychology... Sasa huwa kuna wakati wanajisahau kutenganisha kati ya Dunia (uhalisia wake) na Theories za Darasani kuhusu Mwanadamu. Mie sipingi kila kitu kuhusu usomi, ila kuna wakati inafika inabidi ufahamu uhalisia wa Dunia unayoishi kisha ufahamu mipaka ya nadharia na uhalisia wa Dunia.
 
Waafrika tunapenda shortcut kwa kila kitu, ndio maana hatuishi kudanganywa danganywa.
 
Mtume Petro alikuwa hajasoma hajui kusoma wala kuandika lakini ndie alikuwa papa wa kwanza wa kanisa

Huyo father Amigu na falsafa yake na midigrii kibao ya falsafa na theolojia kaishia upadri tu
Inasemekana anawekewa vikwazo asiwe padri kwasababu alizaliwa Msumbiji,ilhali elimu yake yote kaipatia Tanzania na ameongoza vema taasisi zote alizokabidhiwa kuziendesha.Nadhani ni roho mbaya tu.
 
Ujuaji mwingi huondoa maarifa, na ajabu zaidi kuna Watu wameshamwamini kirahisi rahisi tu, Shetani ana mbinu nyingi kuuhadaa ulimwengu, Mungu atujalie uzima na hekima kuepukana na hawa Manabii wa uwongo.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Umemaliza kiusahihi sana.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Kuna mtu yoyote aliyewahi kumuona MSUKULE?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…