Tiziano Crudeli mtangazaji kichaa wa mpira

Hawa ac milan wanaopigwa had na sassuolo?
Mkuu inaonekana umeanza kushabikia mpira miaka ya karibuni. Ac milan ndio timu ya pili kwa mafanikio kwa michuano ya yote ya ulaya ukiachana na michuano ya nchini italy. Ikiongozwa na madrid yenye jumla ya makombe 19, ac milan imechukua makombe 17 ya ulaya. Siasa na ukata ndio iliyoiharibia timu.
 
Hata Notigham Forest alicheza mechi 50 bila kufungwa ila Leo yuko wap??

Imebaki story
 
Duh, kweli milan imebadilika. Yaani hapo hakuna nimjuaye zaidi ya donnaruma na niang.
Hahaaaa mkuu inakuaje unawajua akina donna na niang alafu akina suso huwafahamu??
Achana na hao watoto wa juzi walioanza kuangalia mpira sababu ya betting,

Millan inarudi mkuu usihofu kwa hilo ni upepo tu ulipita mwakani tunarudi rasmi kukichafua ulaya.
forzamillan
 
Game ni ngumu kweli, na ni muhimu sana maana kwa sasa tuna point sawa na roma, na game inayofuata wanapiga na juve. Juve pia sina uhakika kama atapata matokeo weekend hii ugenini kwa torino ya mihajlovic.
Kikosi kipo hivyo kweli mkuu, isipokua hapo tu kwa antonelli nimeona de sciglio ndo ataanza. Pia tutammiss sana kucka j3.
Nlitamani sana kuona niang asugue benchi, na pale mbele akae bona, lapa na suso, hiyo ingetufanya kua na makali sana mbele, ila ndo hivyo ishu itakua nani wa kucheza LM maana sosa ni chenga tu, na bertolaci sina uhakika kama yupo fiti tayari.
 
Tena mkuu madrid washkuru sana uefa walizochkua mara mbili hivi karibuni, ila tulikua mbele yao na milan ndo tulikua the most successful club in europe, na ya pili kidunia nyuma ya al ahly in terms of international trophies
 
Binafsi naumia sana juu ya mino raiola kua ndo agent wa Bona na Dona. Hawa ni watu muhimu sana kwa milan ya sasa, ila raiola simuamini hata kidogo. Nimeona galliani anakutana na raiola kabla ya alhamisi au alhamisi yenyewe kuongelea kuhusu kumuongezea mkataba Bona mpaka 2020. Ntakua na amani sana hilo likifanikiwa. Forza milan
 

Mkuu donnarouma namfahamu kwa sababu sisi madrid tunamfuatilia kwa karibu sana kutaka kumnyakua, na huyo niang ni kwa sababu ni muafrica. Kiufupi niliacha kufuatilia milan baada ya kupoteza muelekeo na kuanza kuwekeza wakina Poli na elsharaawy baada ya wakina Kaka', seedorf, ambrosini, Gatusso nk kumaliza muda wao wa kuitumikia. Bila shaka generation ya wakina pilro chini ya Don Carlo Anceloti ilikuwa best kabisa na sidhani kama itakuja tokea tena ndani ya sansirro
 
Bila shaka generation ya wakina pilro chini ya Don Carlo Anceloti ilikuwa best kabisa na sidhani kama itakuja tokea tena ndani ya sansirro

Mkuu kizazi bora kabisa kuwahi kutokea milan kilikua chini ya arigo sachi, kikiwa na watu kama van basten, gullit, rijkaard, tasoti, ancelloti, costacurta, maldini, baresi, donadoni, albetini na legends wengine kibao. Kizazi hicho ndo kilifanikiwa kuchukua european cup mara mbili mfululizo(89 na 90) kabla haijabadilishwa jina
 
Roma inafungika mkuu, japokua hatuna history nzuri na uwanja wao miaka ya hivi karibuni lakini nina imani paletta anauwezo wa kumficha vzr tu dzeko, kulikua na habari kwamba strootman hatacheza ila naona hukumu yake wame i-cancell hivo atakuwepo,

Wasi wasi wangu ni upande wa midfielders, hapa ndio patakapo amua huu mchezo tuombe suso aje awe na siku nzuri siku hyo lakini upande wa backline yetu nina imani nayo.

Kuhusu yule kibonge raiola kuwa agents wa bona na donna hii nayo sio nzuri ukiangalia madrid wanamnyemelea donna +uhusiano wake na madrid, but naamini donna hawezi akaondoka kwa sasa san siro bado anahitaji muda mwingi sana wa kujifunza.
 
Umenena vyema sana mkuu Legeza Mwendo
 
Roma wanafungika game yao na atalanta wamefungwa kizembe sana japo walikuwa wanaongoza goli moja. Niang siku game likimkalia vizuri anatulia ila mara nyingi anakuwa mapepe sana hatulii akafanya maamuzi mazuri. Ni kuomba awe na game nzuri maana hamna namna lazima atachezeshwa tu.
 
Hahahaaaaaa mimi huwa nachizika lakini Mzee kanizidi aiseee
Nimecheka sana goal la Thiago Silva kusawazisha dhidi ya Barcelona
Kawakumbatia watu wote
[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Wataliano wengi vichaa wa soka
kuna mmoja nimetafuta clip yake sijaiona
alipagawa mno hadi ikawa gumzo clip yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…