Luqman mohamedy
JF-Expert Member
- Jul 24, 2016
- 899
- 1,231
TLP KUUNGANA NA CCM
Halmashauri Kuu ya Chama cha TLP imesisitiza kuwa chama hicho hakitasimamisha mgombea wa nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, badala yake chama hicho kitamuunga Mkono Mgombea wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli pindi atakapopitishwa na Chama Chake.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho Augustino Lyatonga Mrema amesema maamuzi ya halmashauri kuu ya TLP yanafuatia chama hicho kuridhishwa na mwenendo wa utawala wa Serikali ya awamu ya Tano.
MAONI YANGU
Maamuzi ya TLP kumuunga mkono JPM kwenye uchaguzi wa 2020 inaweza kuwa na faida kubwa kwa TLP yenyewe kuliko hata CCM.
Sidhani na siamini kama CCM inahitaji kura chache za wanachama wa TLP, bali ninachodhani TLP wanahitaji nguvu na anagalau majimbo mawili matatu kwa nguvu ya CCM.
Hii ndio siasa bwana, ukikaza mashindano mwenzio anajenga muungano anakupiga bao.
Kama naona 2020 kwa mara nyingine TLP chama kilichokuwa mfu kinapata angalau kata na majimbo mawili.
Ukiona huna nguvu wewe ungana na mwenye nguvu baadae utapata nguvu.
UKAWA kuna tamaa kubwa muungano wao ni wa Kinafiki
Sina chama najaribu kuchambua muelekeo tu, usinicopy vibaya.