TLS yalitaka Jeshi la Polisi kuwatia nguvuni waliohusika na kitendo cha udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kilichotokea Yombo Dovya

TLS yalitaka Jeshi la Polisi kuwatia nguvuni waliohusika na kitendo cha udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kilichotokea Yombo Dovya

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
242
Reaction score
1,141
GUNvAZgXkAACugl.jpg
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii na taarifa maalum kwa Umma kutoka kwa Jeshi la Polisi Tanzania juu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mwanamke anayesemekana anaishi eneo la Yombo Dovya Jijini Dar es Salaam akifanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia na kundi la Wanaume huku wakirekodi video ya vitendo vile viovu. Tukio hilo sio tu ni kinyume na sheria za nchi yetu lakini pia ni kinyume na maadili na utamaduni wetu kama Watanzania.

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinalaani kitendo hiki kiovu na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki za kisheria na kuhakikisha wahalifu wote walio tenda kitendo kile na waliowezesha kutendwa kwa kitendo kile kiovu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani mara moja ili haki iweze kutendeka.

Aidha TLS inapinga vitendo vyote vya kikatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya usalama na haki jinai katika kuhakikisha wahalifu hao wanafikishwa katika mamlaka sahihi za haki ili kujibu mashitaka yao. TLS pia kupitia kifungu cha 4 (e) cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002) inaendelea kufuatilia mwenendo wa suala hili kwa ukaribu zaidi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na vinavyosimamia haki jinai ili kuhakikisha hatua stahiki kwa waliohusika zinachukuliwa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.

Kila binadamu anastahili heshima, haki na usawa katika jamii yetu. TLS inatoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote ile ikiwemo kuacha mara moja kusambaza video zinazohusu tukio hili ili kulinda haki ya mhanga.

Tanzania bila udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia inawezekana!

Pia soma=> Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa mande na wanaume watatu
 
Safi sana TLS.

Taarifa za awali kwamba hao WAHUNI ni Wajeda(JWTZ) waliajiriwa 2023.

TLS tunaomba mfatilie kwa makini tusije tukapigwa adakadabra kama za Joshua Mulundi(Mtu feki aliyemteka ulimboka).

Waliombaka huyo Binti ni wanajeshi na hata huyo mmoja amevaa vest ya jeshi(Maana raia walikatazwa kuvaa).

Kama yule msanii aliyechoma picha yake aliyemchora Mama kizimkazi alikamatwa fasta ,basi nina imani haifiki jioni polisi watupe taarifa kuwadaka hao Wajeda Wahuni.

Binti ahojiwe amtaje mwanamme aliyetembea nae ambaye ni mme wa Mjeshi(Afande Kaptain) then kaptain aunganishe na hao wahuni aliowatuma.

Sura zinaonekana wazi nilitarajia JWTZ wawafukuze kazi haraka iwezekanavyo wasiwachoshe polisi kuanza kufatilia wakati JWTZ wanawajua hao WAHUNI.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii na taarifa maalum kwa Umma kutoka kwa Jeshi la Polisi Tanzania juu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mwanamke anayesemekana anaishi eneo la Yombo Dovya Jijini Dar es Salaam akifanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia na kundi la Wanaume huku wakirekodi video ya vitendo vile viovu. Tukio hilo sio tu ni kinyume na sheria za nchi yetu lakini pia ni kinyume na maadili na utamaduni wetu kama Watanzania.

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinalaani kitendo hiki kiovu na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki za kisheria na kuhakikisha wahalifu wote walio tenda kitendo kile na waliowezesha kutendwa kwa kitendo kile kiovu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani mara moja ili haki iweze kutendeka.

Aidha TLS inapinga vitendo vyote vya kikatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya usalama na haki jinai katika kuhakikisha wahalifu hao wanafikishwa katika mamlaka sahihi za haki ili kujibu mashitaka yao. TLS pia kupitia kifungu cha 4 (e) cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002) inaendelea kufuatilia mwenendo wa suala hili kwa ukaribu zaidi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na vinavyosimamia haki jinai ili kuhakikisha hatua stahiki kwa waliohusika zinachukuliwa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.

Kila binadamu anastahili heshima, haki na usawa katika jamii yetu. TLS inatoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote ile ikiwemo kuacha mara moja kusambaza video zinazohusu tukio hili ili kulinda haki ya mhanga.

Tanzania bila udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia inawezekana!

Pia soma=> Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa mande na wanaume watatu
Hiyo mke w jamaa aliyewatuma hana akili kabisa,sasa mumewe ndo demu wake jamaa asipoachana na hiyo kama anapiga kavukavu,kukiwa na gonjwa la zinaa atanusurika?Watu wangu waangamia kwa kukosa maarifa! Duuh Mungu tunusuru.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii na taarifa maalum kwa Umma kutoka kwa Jeshi la Polisi Tanzania juu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mwanamke anayesemekana anaishi eneo la Yombo Dovya Jijini Dar es Salaam akifanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia na kundi la Wanaume huku wakirekodi video ya vitendo vile viovu. Tukio hilo sio tu ni kinyume na sheria za nchi yetu lakini pia ni kinyume na maadili na utamaduni wetu kama Watanzania.

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinalaani kitendo hiki kiovu na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki za kisheria na kuhakikisha wahalifu wote walio tenda kitendo kile na waliowezesha kutendwa kwa kitendo kile kiovu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani mara moja ili haki iweze kutendeka.

Aidha TLS inapinga vitendo vyote vya kikatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya usalama na haki jinai katika kuhakikisha wahalifu hao wanafikishwa katika mamlaka sahihi za haki ili kujibu mashitaka yao. TLS pia kupitia kifungu cha 4 (e) cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002) inaendelea kufuatilia mwenendo wa suala hili kwa ukaribu zaidi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na vinavyosimamia haki jinai ili kuhakikisha hatua stahiki kwa waliohusika zinachukuliwa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.

Kila binadamu anastahili heshima, haki na usawa katika jamii yetu. TLS inatoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote ile ikiwemo kuacha mara moja kusambaza video zinazohusu tukio hili ili kulinda haki ya mhanga.

Tanzania bila udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia inawezekana!

Pia soma=> Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa mande na wanaume watatu
Ila wanasheria wana lugha za konakona sana hiyo yote kujifanya wao hawajaiona hiyo connection badala yake ile tarifa ya Polisi ndiyo imewahabarisha ya kile kilichotokea.
Nadhani wangenyooka tu kwa kusema "Baada ya kuangalia ile connection hakika hatujafurahishwa na ule unyama aliotendewa binti anayeonekana kwenye connection ile na tunaliomba Jeshi la Polisi lichukue hatua madhubuti dhidi ya wahusika ikiwemo kufikishwa mahakamani".
Mbona wanajamii sisi ni waelewa tu wala hatutawalaumu maana tutajua hawajaangalia connection kwa nia mbaya bali kumsaidia victim aweze kupata haki yake.
 
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii na taarifa maalum kwa Umma kutoka kwa Jeshi la Polisi Tanzania juu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mwanamke anayesemekana anaishi eneo la Yombo Dovya Jijini Dar es Salaam akifanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia na kundi la Wanaume huku wakirekodi video ya vitendo vile viovu. Tukio hilo sio tu ni kinyume na sheria za nchi yetu lakini pia ni kinyume na maadili na utamaduni wetu kama Watanzania.

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinalaani kitendo hiki kiovu na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki za kisheria na kuhakikisha wahalifu wote walio tenda kitendo kile na waliowezesha kutendwa kwa kitendo kile kiovu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani mara moja ili haki iweze kutendeka.

Aidha TLS inapinga vitendo vyote vya kikatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya usalama na haki jinai katika kuhakikisha wahalifu hao wanafikishwa katika mamlaka sahihi za haki ili kujibu mashitaka yao. TLS pia kupitia kifungu cha 4 (e) cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002) inaendelea kufuatilia mwenendo wa suala hili kwa ukaribu zaidi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na vinavyosimamia haki jinai ili kuhakikisha hatua stahiki kwa waliohusika zinachukuliwa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.

Kila binadamu anastahili heshima, haki na usawa katika jamii yetu. TLS inatoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote ile ikiwemo kuacha mara moja kusambaza video zinazohusu tukio hili ili kulinda haki ya mhanga.

Tanzania bila udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia inawezekana!

Pia soma=> Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa mande na wanaume watatu
Ni mwanzo mzuri kwa TLS ya Bw. Mwabukusi.

Ila pia uangazie na Suala la janga la Watu kutekwa na kutoweka (Forced disappearence) ambalo limeshika kasi sana hivi sasa hapa Tanzania.
 
Wakamatwe hao mafala na fala mwenzao aliyewatuma, ushahidi ni connection kesi week moja week yapili wapigwe umeme, 30yrs.

Kama kweli wajeda basi jeshi lichunguze nidhamu za askari wake.
 
Safi sana TLS.

Taarifa za awali kwamba hao WAHUNI ni Wajeda(JWTZ) waliajiriwa 2023.

TLS tunaomba mfatilie kwa makini tusije tukapigwa adakadabra kama za Joshua Mulundi(Mtu feki aliyemteka ulimboka).

Waliombaka huyo Binti ni wanajeshi na hata huyo mmoja amevaa vest ya jeshi(Maana raia walikatazwa kuvaa).

Kama yule msanii aliyechoma picha yake aliyemchora Mama kizimkazi alikamatwa fasta ,basi nina imani haifiki jioni polisi watupe taarifa kuwadaka hao Wajeda Wahuni.

Binti ahojiwe amtaje mwanamme aliyetembea nae ambaye ni mme wa Mjeshi(Afande Kaptain) then kaptain aunganishe na hao wahuni aliowatuma.

Sura zinaonekana wazi nilitarajia JWTZ wawafukuze kazi haraka iwezekanavyo wasiwachoshe polisi kuanza kufatilia wakati JWTZ wanawajua hao WAHUNI.
Hii video SASHA atakuwa keshaiona tusubiri tuone atachukua hatua Gani.
 
Subiri sasa wakishakamatwa miongoni mwa wanachama wa TLS a watakuwa wanasheria wao
Siyo kosa maana ndiyo kazi ya wakili. Hata ukiua kama huna uwezo wa kuweka wakili wako ssrikali inakupa wakili wa kukutetea bure
 
Back
Top Bottom