TMDA: Ukitumia antibiotiki na usipokojoa mkojo wenye harufu, jua hiyo ni bandia

TMDA: Ukitumia antibiotiki na usipokojoa mkojo wenye harufu, jua hiyo ni bandia

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba Nchini (TMDA), Bw. Adam Fimbo ametoa rai kwa jamii kutambua dawa zote za antibiotiki (Antibiotic) endapo watazitumia kwamba ni lazima iwe na matokeo ikiwemo harufu katika mkojo wa mtumiaji baada ya kutumia.

tmmma.jpg

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba Nchini (TMDA), Bw. Adam Fimbo
Bw. Fimbo ametoa rai hiyo wakati wa akifungua rasmi mafunzo ya siku nne kwa wakaguzi wapya yanayofanyika Kibaha, Mkoani Pwani ambapo alibainisha kuwa TMDA, ina utaratibu wa mafunzo hayo ya mara kwa mara kwa ajili ya kuwajengea uwezo wakaguzi ilikuzuia mianya ya kuingiza dawa bandia ama zisizo na ubora kwa matumizi ya binadamu.

“Kama hutasikia harufu katika dawa hiyo ujue hakuna dawa humo, kinyesi kisipokuwa cheusi ujue hamna dawa humo ndani ya hiyo dawa. Kila dawa inamatokeo yake baada ya kutumia lakini isipotoa matokeo husika ujue dawa hiyo ni bandia hivyo inatakiwa hatua kuchukuliwa haraka,” Alisema Fimbo

Pia Fimbo ameitaka Jamii kuwa watambuzi kwenye kuzingatia dawa halisi ama bandia huku akisema kuwa dawa zote zilizosajiliwa nakukaguliwa na TMDA zinatakiwa kuwa na namba za TMDA za usajili ili kuwahakikishia watumiaji ubora na viwango vilivyokusudiwa katika matumizi.

“Dawa zilizosajiliwa na TMDA zina nembo inayoanzia na TZ na nembo ya dawa inayoanzia na TZA ambapo kila unapoangalia lebo ya dawa utaona namba hizo ambazo zitakuhakikishia kwamba dawa hiyo imesajiliwa na TMDA,” Alisema Fimbo

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa TMDA, anayeshughulikia dawa na vifaa tiba Dkt. Yonah Mwalwisi amesema mamlaka hiyo inatumia mbinu na mifumo mbali mbali inayosaidia kudhibiti ubora katika soko la nchi kwa kuhakikisha linapata vitendanishi na vifaa vyenye ubora, salama na vyenye ufanisi unaotakiwa.

EATV
 
Huyu Mkurugenzi dah.! Ina maana anataka kuaminisha umma kuwa dawa zote lazima ziwe Excreted na Figo?!
 
Mkurugenzi hapo ameferi
Antibiotic nyingne hasa dawa za kumeza matokeo ya harufu huja pengne baada ya siku 2 ndo huweza kuhisi harufu ya dawa
Tofauti na sindano ambapo ndio hutoa matokeo ya harufu kwa halaka

Sasa km hvyo dah ! Utajuwa ugomvi na maduka ya dawa

Mm naona hizi pharmacy kuwe na kipengele kigumu ili kuweza kufungua ili kuepusha maduka madawa uchwala ambayo ndio yanaongoza kwa kuuza dawa feki

Mana siku hizi U.T.I ndio imekuwa biashara marelia sio deal tena
So antibiotic zinauzika km chugu
 
dah hatari najiuliza wale walioambiwa kama haunusi harufu ni corana nahisi kwa ss hadi rangi hawawezi kutofautisha hko walipo.
 
Ali copy na ku paste huu hana mpya kabisaaa hata kidogo....
 
Nianze kwanza kwa kusema SI KWELI KWAMBA kila Dawa au kila Antibiotic mtu akitumia basi itatoa Harufu ambayo ni noticeable kwenye mkojo. Yapo baadhi ya makundi ya Antibiotics yenye viambata vya Penicillins na Cephalosporins , ambayo hujumuisha dawa kama Amoxicillin, Ampiclox, Cefalexin , Cefadroxil n.k ambapo kwa hizi unaweza pata Harufu kwenye mkojo ikiwa ni pamoja na jasho wakati mwingine. Lakini pia yapo makundi mengine ambapo sio rahisi kuhisi harufu kwenye mkojo au jasho. Japo unaweza ona mkojo au kinyesi kibadilika rangi. So sio KWELI kwamba Dawa isipotoa Harufu basi ni Fake. Hapo nadhani DG ameghafilika.
 
Wenye vyoo vya Shimo kama kule shuleni kwetu kuna automatic harufu inakuwaje... Huyu Mkurugenzi inaelekea hujichunguliaga kwa mpalange...

Hii reserch kaiachia live ni sawa na tathmini kesi ya Takwimu ya utawala wa katiri ingemhusu
 
Back
Top Bottom