TMDA: Ukivuta sigara hadharani faini Tsh. 200,000 au jela miezi 6

TMDA: Ukivuta sigara hadharani faini Tsh. 200,000 au jela miezi 6

Fegi hazina faida yoyote,napambana Sana kuachana na hii kitu nadhani kukwepa miezi 6 au kufokolewa 200,000 ni Bora kuachana nazo tu.
Kiburudisho gani KERO kwa wengine?
 
Kama ndio hivyo kwa nini wasipige marufuku kilimo cha tumbaku.
 
Kama ndio hivyo kwa nini wasipige marufuku kilimo cha tumbaku.
Hujakatazwa kuvuta ila vuta kistaarabu. Kuna watu sio wastaarabu na masigara yao wanavuta pasipo kuangalia wapo maeneo gani
 
Waondoe hicho kipengele cha au jela miezi sita na iwe au kunyongwa hadi kufa.

Na yule anayekamata mvutani akimfikisha tu kituoni apewe 50k pale pale hata kabla mtuhumiwa hajatozwa hizo 200k halafu uone kama watu wataendekeza kukera wengine kwa sitarehe zao.
 
Sawa.

Tufanyieni tu kama tarura


Ila wavuta sigara mnakera kweli kweli
 
Wenzetu wametenga smoking area

Bongo wamefanya hivyo au ndy wanatengeneza style ya kujipigia hela

Ova
 
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imesema ni kosa kisheria kuvuta sigara hadharani au kwenye maeneo ya mikusanyiko na atakayebainika kufanya hivyo atatozwa faini ya Tsh. 200,000 au kutumikia adhabu ya kifungo cha miezi sita jela.

Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TMDA, Gloria Matemu aliyasema hayo Aprili 9, 2022 katika Soko Kuu la Kariakoo, wakati wa kampeni ya kutoa elimu katika maeneo ya mikusanyo kuhusu madhara ya kutumia tumbaku na adhabu zake.

Alisema TMDA imepewa jukumu la kudhibiti matumizi ya tumbaku kwa lengo la kutoa elimu kuhusu matakwa ya sheria namba 121 kuanzia Aprili 30, 2022.

"Ukibainika unavuta tumbaku hadharani au katika mikusanyiko utatozwa faini ya Sh 200,000 au kutumikia adhabu ya miezi sita jela," alisema.

Hivyo, aliwataka wamiliki wa kumbi za starehe na masoko kutenga maeneo maalum ya kuvutia sigara kwa sababu watu wengi wanaathirika kutokana na watu wachache wanaovuta sigara.

Matemu alisema TMDA imefanya kampeni ya siku tano ya kutembelea kwenye maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu kama vituo vya mabasi na masoko, ili kuwaelimisha kuhusu madhara na namna sheria inavyofanya kazi.

Alisema kampeni hiyo imesaidia kufikisha elimu kwa wakazi wa Manispaa ya llala na lengo kuu ni kuwafikia Watanzania wote wafahamu kuhusu jukumu hilo la TMDA katika kudhibiti matumizi ya tumbaku ili kupunguza madhara yatokanayo na uvutaji huo.

Mkaguzi wa TMDA, Kanda ya Mashariki, Jafari Tolo alisema takwa la sheria ni kuzuia uvutaji wa sigara kwenye mikusanyiko ya watu na wamiliki wa maeneo yanayokusanya maeneo maalum ya wanaovuta kuvuta bila kuathiri wasiovuta.

Alisema pia maeneo yenye mikusanyiko kunapaswa kufungwa vifaa vya kubaini endapo kuna mtu anavuta sigara katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Ofisa Afya wa Soko la Kisutu, Aron Matei aliishukuru TMDA kwa elimu waliyotoa na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari kuhusu uvutaji wa sigara katika maeneo yasiyo rasmi.


Source: Nipashe
wavutie wapi sasa
 
Dah.....wabongo wanajichanganya kweli....sugars siyo bangi Wala sex....Kuna tofauti kati ya hadhara....na hadharani....hadhara ni sehemu yenye mikusanyiko ya watu Kama masokoni, vituo vya Basi, kumbi za starehe nk.....na hadharani ni sehemu yoyote ambayo mtu anaonekana na mtu mwingine...hata ukikaa barazani kwako uko hadharani.....ukiwa shamba kwako nk.....tutafautishe kati ya maeneo ya umma.....maeneo ya wazi.....na maeneo binafsi....bila hivyo tamko hili Ni upuuzi🤣🤣🤣🤣🤣
 
Dah.....wabongo wanajichanganya kweli....sugars siyo bangi Wala sex....Kuna tofauti kati ya hadhara....na hadharani....hadhara ni sehemu yenye mikusanyiko ya watu Kama masokoni, vituo vya Basi, kumbi za starehe nk.....na hadharani ni sehemu yoyote ambayo mtu anaonekana na mtu mwingine...hata ukikaa barazani kwako uko hadharani.....ukiwa shamba kwako nk.....tutafautishe kati ya maeneo ya umma.....maeneo ya wazi.....na maeneo binafsi....bila hivyo tamko hili Ni upuuzi🤣🤣🤣🤣🤣
loswahili ni kibantu
 
Back
Top Bottom