Tofauti kati ya mhuni na mhalifu

Tofauti kati ya mhuni na mhalifu

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2021
Posts
630
Reaction score
1,262
Watu wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mhuni na mhalifu na kuleta mkanganyiko pale wanapotaka kufahamu tofauti ya watu hawa wawili.

Mhuni ni mtu yeyote aliyeamua kwenda kinyume na maadaili mema au utamaduni huku mhalifu ni mtu yeyote aliyevunja sheria.

Mhuni anakosa maadili mema na kufanya mambo yanayokinzana na tamaduni za watu anaoishi nao iwe jamii au nchi kwa ujumla.

Mhuni anaweza kuwa anatumia mihadarati, kauli chafu, anavaa mavazi yasiyo na staha, mitindo mibovu ya urembo wa mwili wake, mtu muongo, mtu anayejihusisha na ushoga au usagaji kwa kuridhia mwenyewe, kwa ujumla mtu asiye mcha Mungu

Mhalifu yeye anafanya makosa yaliyokatazwa katika sheria iliyowekwa ikiwemo wizi, uuaji, ubakaji, utakatishaji wa fedha, biashara haramu, udhalilishaji kwa njia yeyote ile, na mengineyo.

Mhuni anaweza asiwe mhalifu hii inatokea pale anapokosa maadili kama kutokwenda kwenye ibada, mitindo mibovu ya mavazi, kukosa heshima, uvivu, uchafu wa mwili na mazingira yanayomzunguka lakini havunji sheria za nchi.

Mhalifu anaweza asiwe mhuni hii inatokea pale mhalifu huyu kuwa na maadili yanayopendeza jamii yake au nchi yake anapokuwa mbele za watu lakini anatekeleza uhalifu kwa njia ya siri sana na watu wasimtambue kuwa ni mhalifu.

Ni rahisi sana kumtambua mhuni kuliko mhalifu kwasababu mhuni anaonekana kuwa amekosa maadili lakini mhalifu anaweza asitambulike kwa haraka ikiwa anavunja sheria akiwa peke yake au kwa siri.
 
Washaanza kutetea panya road
 
Mkuu nadhani wewe ndio huelewi mhuni na mhalifu ni mtu mmoja.

Ili uwe mhuni unapaswa ufanye uhalifu.

Kwa kukusaidia tuu,
Yote uliyoyasema kwenye uhuni mfano ushoga, kutumia mihadarati, usagaji, matusi n.km vyote hivyo ni uvunjifu wa sheria, hivyo ni uhalifu.

Kumtukana mtu ni kuvunja sheria hivyo ni uhalifu.
Kutoka na Wake za watu ni kosa kisheria, ni uhalifu.

Ukishaambiwa wewe ni mhuni jua tayari kuwa wewe ni mhalifu yaani unaweza kuvunja sheria.

Kufuata sheria ndio maadili yenyewe, sasa ukivunja sheria ndio Uhuni wenyewe.

Kwa Sisi tunaojichanganya na wahuni tunajua wahuni ndio wahalifu wenyewe.
 
Mkuu nadhani wewe ndio huelewi mhuni na mhalifu ni mtu mmoja.

Ili uwe mhuni unapaswa ufanye uhalifu.

Kwa kukusaidia tuu,
Yote uliyoyasema kwenye uhuni mfano ushoga, kutumia mihadarati, usagaji, matusi n.km vyote hivyo ni uvunjifu wa sheria, hivyo ni uhalifu.

Kumtukana mtu ni kuvunja sheria hivyo ni uhalifu.
Kutoka na Wake za watu ni kosa kisheria, ni uhalifu.

Ukishaambiwa wewe ni mhuni jua tayari kuwa wewe ni mhalifu yaani unaweza kuvunja sheria.

Kufuata sheria ndio maadili yenyewe, sasa ukivunja sheria ndio Uhuni wenyewe.

Kwa Sisi tunaojichanganya na wahuni tunajua wahuni ndio wahalifu wenyewe.
Nakazia!
 
Watu wengi wanashindwa kutofautisha kati ya mhuni na mhalifu na kuleta mkanganyiko pale wanapotaka kufahamu tofauti ya watu hawa wawili...
Yatosha asee nasema yatosha watu sasa hivi wanabadilishwa jinsia na kaka zao wanakuwa rojo na legelege kama wapemba siyo wahuni ama wahalifi. Watanzania jinsia zetu zimevurugwa.
 
Hivi ujui kama kutumia miadarati na kutusi watu ni kuvunja sheria. Ukiwa muhuni lazima utakua muhalifu tu.
 
Hivi ujui kama kutumia miadarati na kutusi watu ni kuvunja sheria. Ukiwa muhuni lazima utakua muhalifu tu.

Utashangaa aliyetoa hoja anadegree.

Anashindwa kuelewa kuwa Neno mhuni lipo Kupunguza makali ya neno Mhalifu.
Kama vile Mdangaji Kupunguza ukali wa neno Malaya.

Ili uwe Mhuni itakupasa uvunje sheria Fulani
 
Mkuu nadhani wewe ndio huelewi mhuni na mhalifu ni mtu mmoja.

Ili uwe mhuni unapaswa ufanye uhalifu.

Kwa kukusaidia tuu,
Yote uliyoyasema kwenye uhuni mfano ushoga, kutumia mihadarati, usagaji, matusi n.km vyote hivyo ni uvunjifu wa sheria, hivyo ni uhalifu.

Kumtukana mtu ni kuvunja sheria hivyo ni uhalifu.
Kutoka na Wake za watu ni kosa kisheria, ni uhalifu.

Ukishaambiwa wewe ni mhuni jua tayari kuwa wewe ni mhalifu yaani unaweza kuvunja sheria.

Kufuata sheria ndio maadili yenyewe, sasa ukivunja sheria ndio Uhuni wenyewe.

Kwa Sisi tunaojichanganya na wahuni tunajua wahuni ndio wahalifu wenyewe.
Najikuta nacheka mkuu
 
Muhuni na muhalifu wote ni wavunjaji sheria na wanapaswa kudhibitiwa na kuadhibiwa...
 
Mkuu nadhani wewe ndio huelewi mhuni na mhalifu ni mtu mmoja.

Ili uwe mhuni unapaswa ufanye uhalifu.

Kwa kukusaidia tuu,
Yote uliyoyasema kwenye uhuni mfano ushoga, kutumia mihadarati, usagaji, matusi n.km vyote hivyo ni uvunjifu wa sheria, hivyo ni uhalifu.

Kumtukana mtu ni kuvunja sheria hivyo ni uhalifu.
Kutoka na Wake za watu ni kosa kisheria, ni uhalifu.

Ukishaambiwa wewe ni mhuni jua tayari kuwa wewe ni mhalifu yaani unaweza kuvunja sheria.

Kufuata sheria ndio maadili yenyewe, sasa ukivunja sheria ndio Uhuni wenyewe.

Kwa Sisi tunaojichanganya na wahuni tunajua wahuni ndio wahalifu wenyewe.
 
Utashangaa aliyetoa hoja anadegree.

Anashindwa kuelewa kuwa Neno mhuni lipo Kupunguza makali ya neno Mhalifu.
Kama vile Mdangaji Kupunguza ukali wa neno Malaya.

Ili uwe Mhuni itakupasa uvunje sheria Fulani
Nakubaliana na wewe kabisa
 
Back
Top Bottom