Tofauti kati ya X-rays, MRI na Ultra sound.

jf user

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2018
Posts
777
Reaction score
623
Habari wakuu.
Naomba kujua tofauti kati ha hivi vitu MRI, X-rays, Ultra sound na CT Scan interms of-
1/Cost
2/Ubora wa picha "Clear image"
3/Effect kwenye mwili wa binadamu mfano mionzi ya X-rays na madhara ya MRI na Ultra sound.
4/Upatikanaji hapa kwenye hospitali zetu na za binafsi pia sio mbaya mkaziorodhesha zote ili iwe rahisi kupata huduma kwa watu walio sehemu mbalimbali za nchi.
5/Uhitaji wa wataalamu.
 
Reactions: Uda
Ubora, gharama na upatikanaji wake.
Ghari zaidi ujue ndio bora zaidi na ndio adimu haswaa.
Sasa wewe fuatilia kuanzia hapo
 
1. X ray na ultrasound sehemu nyingi hazitofautiani sana gharama, na nafuu kuliko MRI. Hospitali nyingi za serikali haizidi elfu 30.

2. Hakuna suala la ubora wa picha maana kila kimoja kina fanya kazi kwa namna yake. Ila MRI inauwezo mkubwa wa kuchunguza hata kasoro ndogo ndogo sana ambazo ultrasond inaweza isizioneshe.

3. Miozi ijukikane tu kuwa si salama kwa binadamu, lakini madhara yake si makubwa hasa kwa ultrasound na MRI, X ray zenyewe ndio si nzuri kupiga mara kwa mara hata maeneo ya kichwa na kifua pasipo ulazima wa kufanya hivyo.

4. X ray na ultrasound zinafanyika karibu vituo vyote vya afya vyenye hazi ya hispitali. MRI nazo zinapatikana kwa baadhi ya hospitali kubwa kubwa, Aga Khan utapata huduma, ile ya Mkapa dodoma utapata huduma, hata Muhimbili pia
 
Gharama kwa MRI ni kubwa kiasi, hata muhimbili tu si chini ya laki 5 kwa wasitumia bima, sijui kama zimepanda au kushuka
 

3. ultrasound na MRI hazitoi Mionzi.
 
Shukrani mkuu nadhani MRI ndio bora Zaidi.
 
X Ray n hatar Kwa afya yako Pia n bei ndogo Pia inapatikana hospital nying
 
Ukitaka kupata uzoefu wa kuwa kwenye jeneza utaupata kwenye MRI

Hicho kipimo ni kwa vile tu ni ugonjwa hauna namna ila kinaogopesha
 
3. ultrasound na MRI hazitoi Mionzi.
Ni sawa mkuu. Inatumia mawimbi ya sauti na mwangwi, sema ndio hivyo humu unaweza ukatoa maelezo ya ndani ndani kidogo kumbe ndio mtu akapotea kabisa asielewe kitu. Ndio maana majibu ni ya general sana tena juu juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…