Pre GE2025 Tofauti ya Daftari la Kudumu la Wapigakura na Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa

Pre GE2025 Tofauti ya Daftari la Kudumu la Wapigakura na Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kwa ufahamu tu:

Tofauti kati ya Daftari la Kudumu la Wapigakura na Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa

Daftari la Kudumu linasimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya Kumchagua Diwani, Mbunge na Rais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.

Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa linasimamiwa na Ofisi ya Rais - TAMISEMI na ni kwa ajili ya Uchaguzi wa Wenyeviti wa Vijiji, Wajumbe, Wenyeviti wa Vitongoji na Wenyeviti wa Mitaa.

Daftari la Wapigakura wa Serikali za Mitaa litaanza kuandikishwa kuanzia tarehe 11 - 20/10/2024

Uandikishaji utafanyika kwenye Ofisi Vitongoji na Mitaa au kwenye Majengo ya Umma ya maeneo hayo na vituo vitafunguliwa kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na mbili Jioni

Zoezi hili ni kwa Tanzania Bara na litafanyika kwa muda wa siku 10.

NB: Kila mtu anajiandikisha katika eneo analoishi yaani Kitongoji/Mtaa wake.

Snapinsta.app_462619786_18347708266193701_7173077663418115474_n_1080.jpg


Chanzo: TAMISEMI

Pia soma ~ Rais Samia kuzindua uandikishaji wa Wapiga Kura wa Serikali za Mitaa Oktoba 11, 2024 - Dodoma
 
Lakini si kila mwananchi atapata kadi ya mpiga kura bila kujari anajiandikisha kwenye daftari lipi!!?
 
CHADEMA HAWATAKI VIJANA WAJIANDIKISHE, JE WANAWAOGOPA KWENYE UCHAGUZI?

Sauti za Chadema sasa zinapaza malalamiko yasiyo na mashiko, wakidai kwamba Tume ya Uchaguzi (NEC) inaandikisha wanafunzi kwa lengo la kuwaandaa kupigia kura CCM. Ukweli ni kwamba, kila kijana mwenye miaka 18 ana haki ya kikatiba kujiandikisha na kupiga kura.

Hii siyo mbinu ya kisiasa bali ni utekelezaji wa sheria, kwani vijana waliozaliwa mwaka 2006, wakiwemo wa umri wa miaka 17 mwaka huu, watafikisha miaka 18 ifikapo mwakani. Je, Chadema wanataka kuwanyima haki zao kikatiba?

Chadema wanatakiwa kuelewa kuwa kila aliyeandikishwa ameonesha kitambulisho kinachoonesha umri wake halali. Kuibua tuhuma za "kuandikisha watoto" bila kutoa ushahidi wa vitambulisho ni mbinu ya kisiasa ya kutengeneza mazingira ya kujiondoa mapema au kutafuta kisingizio endapo watashindwa tena mwakani. Tumeona mbinu kama hizi mara kadhaa—wakishindwa, hukimbilia kusema "tulibambikiwa."

Nani anaweza kuwazuia vijana wenye ari na shauku ya kushiriki kikamilifu katika uchaguzi? Hili si swali la wafuasi wa CCM bali ni ishara ya hofu ndani ya Chadema, wakijua kuwa kizazi cha sasa kinatambua haki zake na hakitadanganywa kirahisi. Wanapojaribu kupinga ushiriki wa vijana, wanaonesha wazi kuwa hawataki sauti za kizazi kipya zisikike.

Kwa kifupi, malalamiko ya Chadema si hoja ya msingi bali mbinu ya kuwatisha vijana na kuwapotezea imani katika mchakato wa uchaguzi. Uchaguzi si mchezo wa kuigiza bali ni nafasi ya kila raia, awe kijana au mzee, kuamua hatma ya taifa kupitia sanduku la kura.

Kama Chadema wana hofu ya kushindwa, basi wanapaswa kujipanga na kuja na sera bora badala ya kutengeneza visingizio visivyo na msingi.
 
Tunashindwa kuunganisha ,taarifa za nida,sensa na NEC,TIN NUMBER,NA PSSSF ?
 
Serikali za mitaa zitakuwa na kura nyingi kuliko Uchaguzi Mkuu.... Msiniulize Kwa Nini.... Amekuja kiongozi mmoja ana kidaftari kina majina shazi.... Waandikwe .... Kuna kiongozi wa chama kingine wamashikana Masharti .....ila CCM hata aibu hawanaga asee
 
Back
Top Bottom