Habari Wana-JF, mimi nina azma ya kutengeneza bidhaa hivi karibuni. Bidhaa na utengenezaji wake, unahitaji pia utambulisho.
>>Ninaomba ufafanuzi, bei ya kutengeneza, na tofauti, kama ipo, ya LEBO na NEMBO. Katika mafunzo yangu ya uzalishaji wa bidhaa za viwandani, nilifundishwa pia namna ya ku-design lebo. Pia hapa JF, nimewahi kuona tangazo la biashara ya kudizain nenbo. Swali langu ninahitaji kujua kama kuna tofauti ya LEBO na NEMBO, na bei ya kutengeza hizi alama/vitambulisho..#Asante
Nembo au Logo kwa ki english ni alama ya utambulisho wa bidhaa, kampuni, biashara. Lebo inaandikwa label maana yake ni bandiko, weka alama. unaweza ukabandika nembo kwenye bidhaa.
Wewe unahitaji nembo, ambayo itabandikwa kwenye bidhaa zako.
Nembo au Logo kwa ki english ni alama ya utambulisho wa bidhaa, kampuni, biashara. Lebo inaandikwa label maana yake ni bandiko, weka alama. unaweza ukabandika nembo kwenye bidhaa.
Wewe unahitaji nembo, ambayo itabandikwa kwenye bidhaa zako.
Nembo ni alama ya utambulisho wa biashara yako na lebo ni alama ya bidhaa inayotambulisha brand ambapo katika lebo yako lazima kutakuwa na nembo ya biashara yako hivyo kama unataka kutengeneza lebo au stika kama wengi walivyozoea unatakiwa kwanza utengeneza nembo ya biashara ambayo itatumika kama utambulisho wa mmiliki wa biashara na baadae ndio lebo ambayo inakuwa ni mmiliki wa bidhaa.