Uchaguzi 2020 Tofauti ya mikutano ya CCM na CHADEMA ni kuwa CCM inahudhuriwa na wanachama wengi wakiwa wamevaa nguo za CCM, CHADEMA hakuna

Hahaha kwa wizi inayofanya ccm ningeshangaa kama mgekosa manguo ya kugawa bure mikutanoni.
 
Ni kweli CCM wanavaa sana T-shirt. Mie hapa tayari Nina 2 za bure, nadubiri kupewa Shati na form six. Total NNE. Nitatinga zote. Chadema zao ukiacha wale walioshiriki mkutano mkuu, wengine wote ni kununua, hata hivyo naona wanajitahidi sana kununua.
Kikubwa hofia ile michango wanayocangia, lazima tu watampigia kura. Wale wote hutoa kwa moyo ssna. Na Si kinafiki
 
Z
sasa kama watu wa ccm ndio wanahudhuria kampeni za ccm..kuna haja gani ya ccm kupiga kampeni?
Kampeni si tu kuomba kura ni kueleza mafanikio ya yale uliyoyafanya kwenye ilani iliyopita

CCM inaenda kutoa ripoti kwa wanachama wake pia kupitia hiyo mikutano ndio maana wanajaa wasikie ripoti na pia wasikie nini kinafuata kwenye ilani mpya

Ule ni mkutano wa hadhara wa Chama pia ila ume combine vyote chama na kampeni
 
2015 Chadema mbona hali haikuwa hivyo enzi za Lowasa? Watu walikuwa na Mwamko mkubwa na chama. Tshirt Chadema kila kona na wala hawakuwa wamenunuliwa hizo Tshirt na Lowasa ni wao wenyewe

Chadema mkubalu chama kimedorora Mwanao wa wanachama umekufa umebaki kwa viongozi na tu ni kwa ajili ya maslahi tu lakini Chadema hakina wanachama wafia chama

Haiku yenu mbaya sio siri
Uvaaji nguo za Chama ni moja ya kiashiria cha mapenzi makubwa na Mwanao mkubwa wa wanachama kwa chama chao

CCM wanachama hununua nguo za CCM za familia nzima

Kukiwa n.a. tukio la CCM wote wanavaa nguo za CCM kuonyesha mapenzi yao makubwa waliyonayo kwa chama chap

Chadema hali tofauti. Hilo la mavazi tu ni kiashiria tosha kabisa kuwa CCM in a wapiga kura wengi royal kwake tofauti n.a. Chadema wategemea kura za wapita njia au wanaokuja tu mkutanoni kusafisha macho na masikio

Nakwambia hata confidence ya mgombea inakuwa kubwa na iko juu kuhutubia watu wengi waliovaa sare ya chama cake.Ukiangalia Lisu unamwonea hadi huruma akihutubia hiyo hali ka i note
Unakuta hakawii kuacha hata kuhutubia sera anakuwa mtu wa hasira ghafla n.a. uso unayeyuka uangavu wake sababu anaona anaowahutubia kama sio wenyewe vile na mwisho inathibitika kuwa ni kweli sio wenyewe akianza kuitisha mchango watu wanaondoka mkutanoni mbio kwa makundi makubwa haraka kukataa kuchanga
 
Sasa mnagawa fulana ,mashati na kofia bure ulitegemea nini?
 
miaka 5 kabla ya uchaguzi wa 2015, vyama vyote vilikuwa huru kuendesha mambo ya siasa. kwa hiyo vyama vyote viliingia uchaguzini vikiwa na nguvu sawa.... of course ukiondoa dola na NEC kuegemea zaidi upande wetu.

chini ya awamu ya 5, CCM ya MATAGA (ya Chaku Polepole asiyekumbuka jana alisema nini) imekuwa ikiendesha siasa peke yake. vyama vya upinzani vimekuwa kama adui wakati tunapoingia kwenye uchaguzi wa 2020. hii siyo siasa safi aliyotuachia kipenzi chetu Mwalimu (RIP mzee wetu).

kwenye hizi kampeni za sasa tupo CCM wengi tu tunaom support Tundu Lissu but tunafanya hivyo kwa kificho sana kuchelea backlash maana tumewekeza sana chamani tangu enzi za Mwalimu.
so, wengi wetu hata hatuhudhurii mikutano yake but kura za wana CCM anazo kwa mamilioni.
 
Moja ya sababu nyingine wanaogopa kuvaa nguo za timu yao wakimuogopa jini mnyonya damu asiwatambue kirahisi
 
Tofauti nyingine ni kuwa
Ccm watu wwnasombwa kwa malori
Mgombea anaongea kilugha akiwa kwao
Wananchi wanaenda kumuuona ZUCHU NA DIAMONDI na Maria nyerere kuongeza vichwa
Share za chama zinatolewa bure
Note. Sare za chama co idadi ya kura. Aliyepokwa KOROSHO zake na Kuhani hajasahau Kyle kusini.kumbuka hilo
 
N
Kwani si mnatumia kodi zetu, kununua mitishet na kuigawa bure??

Yaani kama ni mapenzi, Mapenzi walonayo wananchi kwa CHADEMA ndio Halisi.

Hamna cha hongo ya aina yoyote lakini nyomi lake sasa [emoji23][emoji23]
Na nyie tumieni ruzuku yenu ambayo ni pesa za wananchi,
Je za mabeberu?
 
Marofa ndo wnasema kuwa kubebwa ni marori ni shida, lengo pale ni kufika unapotaka kufika,
Huwezi kusema Umeenda kwa kutokubebwa ilihali umefika huku unaumia.
Kwa hiyo mateso sio sifa.
 
Bac tutakutana October lazima mshikwe na wazimu
 
Tofauti kubwa zaidi kwenye mikutano ya ccm watumishi wa umma na wanafunzi wanalazimishwa tena kwa vitisho kuhudhuria mkutano.
 
Hao wa ccm wanaongozwa kabisa wavaeje
 
Nyie mna ela za kuwahonga wananchi, ivi vile vitoto vya shule pale kirumba na mjimwema kigamboni vilinunua zile sare kwa ela gano au vilishurutishwa tu kuvaa baada ya kupewa elf2 kila kamoja.
Kweli hiyo ni tofauti
 
Pia umesahau juu ya wale wanaoenda kumuona diamond akikata mauno.
Na huo ni ufuasi feki
 
Wapo watanzania wengi wasio na vyama lakini sasa wamehamasika kuingia upinzani baada ya kukasirishwa na ushetani mpya wa CCM wa kupita bila kupingwa kwa njia haramu, CCM husombwa na magari kutoka sehemu nyingi za jirani na pia ukumbuke CCM huchukua pesa Hazina kienyeji pasipo idhini ya bunge ni rahisi kuwanunulia watu nguo za CCM kisha kuwalazimisha kuvaa, kwa mfano wahindi, waarabu wengi huvaa nguo za CCM kwa kujipendekeza tu wakihofia kubambikiwa kesi wakaporwa mali zao, wanaovaa nguo za CCM siyo kwamba wote wanaipenda CCM bali huvaa tu kulinda biashara zao.
 
Watu wa chadema hufuata sera maneno ya faraja lakini watu wa CCM huenda kuangalia show za wasanii mbalimbali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…