Tofauti ya usalama kati ya ebay na amazon

Joined
Sep 27, 2014
Posts
27
Reaction score
2
Je ni ipi iko salama zaidi katika manunuzi ya vitu online kati ya ebay na amazon

Naombeni msaada wakuu.
 
NaUnGa mKoNo hOjA....[emoji30][emoji30]
 
MImi ni mzoefu wa hizi plafforms mbili kwa miaka mingi na sijapata tatizo lolote la kuwezesha kutumia sheria.

Lakini Ebay unapaswa kuhakikisha muuzaji ni wa UK au US bila kujali suppliers wake ni wa wapi kwani ni rahisi kufanya tracking kwake.

Nikisema tracking namaanisha physical address na VAT number kuonyesha analipa kodi na ataweza kulipa refunds.

Usinunue bidhaa toka Eastern Europe maana wengi ni matapeli na unaweza kununua simu na ukaletewa boksi limejazwa karatasi.

Kama muuzaji yupo Easteren Europe basi angalia reputation yake na iwe kuanzia 99% - 100%

Pia usitoe taarifa zozote za kuhusu kadi zako za benki wala taarifa zingine binafsi kwenda Ebay mpaka utakaporidhika na maelezo ya hapo juu.

Amazon ni salama kwa 100% na ndo huwa nawatumia mara nyingi, isipokuwa hawasafirishi mizigo kuja Tanzania kwa sasa.

Bidhaa nyingi ambazo utazipata Ebay zinapatikana Amazon, hivyo waweza kununua bidhaa kutoka Amazon.co.uk au Amazon.com
 
Nikisema tracking namaanisha physical address na VAT number kuonyesha analipa kodi na ataweza kulipa refunds.
EBAY/AMAZON ndio wanakufanyia refund. Iwapo utafungua case, Hata kama ulisha ulisha pokea mzigo na kuthibitisha kuwa ulipokea mzigo ila baada ya muda ukatamba kuwa ni fake au una kasoro.
Usinunue bidhaa toka Eastern Europe maana wengi ni matapeli na unaweza kununua simu na ukaletewa boksi limejazwa karatasi.
Iwapo utatumia taratibu sahihi za manunuzi, bado uko salama na fedha yako inarudishwa.
Kama muuzaji yupo Easteren Europe basi angalia reputation yake na iwe kuanzia 99% - 100%
Muuzaji anaweza kuwa na feedback mbili tu na ikawa inaonyesha rep. ni asilimia 100%
Kinachotakiwa angalia idadi ya positive and negative reviews
Angalia kama amewekewa logo ya Top rated seller.
Tembelea store yake hakiki bei ya bidhaa zingine, Je bei zina uhalisia ukilinganisha na site zingine kama amazon au bestbuy etl, ndipo fanya manunuzi.

Mfano unaona wazi laptop ya USD900 imeandikwa USD 130 na wewe unaaamua kununua, hapo ni kujitafutia usumbufu usio wa lazima.
Pia usitoe taarifa zozote za kuhusu kadi zako za benki wala taarifa zingine binafsi kwenda Ebay mpaka utakaporidhika na maelezo ya hapo juu.
Njia salama ya kufanya malipo ni kutumia Paypal, alipay, amazon pay na sio matumizi ya card direct. (Jpokuwa zipo site salama za kutumia card direct)
Amazon ni salama kwa 100% na ndo huwa nawatumia mara nyingi, isipokuwa hawasafirishi mizigo kuja Tanzania kwa sasa.
Sites zote ebay, amazon ni salama kwa asilimia 100, Kinachotakiwa ni mnunuzi kuwa na ABCs za vitu vya kuzingatia kabla ya kufanya manunuzi ya bidhaa husika.
isipokuwa hawasafirishi mizigo kuja Tanzania kwa sasa.
Ila zipo njia za kufikisha mzigo hapa Tanzania toka hizo site husika

Ref
 
Vipi kuhusu mzee mzima kupatana.com !? Maana nahisi ni genge la wahuni!![emoji21]
 
Vipi kuhusu mzee mzima kupatana.com !?
Ukifuata taratibu sahihi za manunuzi, Ndio waweza kunua bidhaa.
Iko wazi kupatana usifanye nalipo kabla ya kuiona na kukagua bidhaa husika. NJE YA HAPO HAKUNA BIASHARA
Maana nahisi ni genge la wahuni!!
Licha ya kuhisi, Je kuna utafiti umefanya wa njia bora zaidi ya kununua kupitia kupatana??
 
Nilitaka nunua vitu flani kupitia krazytrendz ila naona hawana paypal. Kuna mtu ashawahi watumia kulipa direct na wapo salama!?..
 
Mwalimu, Mimi kule nimeshapigwa mpaka huruma!!
 
Mwalimu, Mimi kule nimeshapigwa mpaka huruma!!
1. Hakuna biashara ya kutanguliza fedha ( Hasa kupatana)
2. Ni lazima ufike sehemu husika (au uletewe mahala wewe ulipo)ukague na unapokuwa umerishishwa na bidhaa ndio unalipia. Kupata inawaunganisha wauzaji na wanunuzi na iko wazi USITUME FEDHA KABLA YA BIDHAA KUIPATA/ KUKUFIKIA, sasa wewe inakuwaje unalipia bidhaa ambayo huijakufikia, haujaikagua
3. Wengi hupoteza fedha kwa kutokuzingatia taratibu za kuhakikisha unakuwa salama.
 

Mkuu, shukrani kwa kuchangia.

Ila hizi plafrorms mbili mimi ni mwanachama miaka zaidi ya 10 sasa nazielewa ndani nje.

Ebay kuna watu wengi wamepigwa sana hasa na wazungu wa Eastern Europe, hiyo nna uhakika wa 100%.

Mimi pia kuna wakti nikiwa huko majuu huwa nafanya "delivery services" mwenyewe kwa njia ya Amazon Flex.

Na mimi ni muumini mkubwa wa Amazon na nimeizoea mno kuliko Ebay.

Pia niliwahi na bado nafanya kama "ad- hok" B2B na natumia DX, Royal Mail, Fedex na UPS kusafirisha bidhaa mbalimbali.

Ila mwaka wa kwanza umepita niliamua kuingia "venture" ingine ya kukaanga chips kwanza na mbawa za kuku hapahapa eneo la tukio Tanzania.

Nipo Tandale- Kwamtogole.

Karibu.

😀😀
 
Ebay kuna watu wengi wamepigwa sana hasa na wazungu wa Eastern Europe, hiyo nna uhakika wa 100%.
Ukiwa Kama ni mtumiaji wa EBAY/ PAYAPAL:

Je wajua kuwa una siku zisizozidi 180 (Miezi sita) kudai fedha yako na EBAY/ PAYPAL wakakurudishia??

Je unajua nini unatakiwa ufanye pindi ununuapo bidhaa na bidhaa haijakufikia ( hapa wewe umetumia neno kupigwa) ??

Je wajua kwa AMAZON/ EBAY waweza nunua bidhaa ukapokea, bidhaa yako vizuri tu, ila ukaamua kuomba refund na ukapewa?? JE UNADHANI NI KWA NINI?? amazon/EBAY wana huo utaratibu??

Naendelea kusisitiza EBAY/ AMAZON zote ni salama, Tatizo liko kwa watumiaji wa mitandao husika.

Site zote EBAY/AMAZON zina mifumo salama ya kuhakikisha mteja anakuwa salama, Na mteja anaridhika kwa huduma anayoipata EBAY/AMAZON.
 
Vipi kuhusu alibaba ni Salama kuagiza bidhaa.Maana China vitu bei rahisi
 
Umenena kweli cjawahi nunua ebay wala amazon mm nipo tu huku kwangu (aliexpress)
 
Vipi usafirishaji wa bidhaa kwa ebay na amazon huchukua muda gani ukilinganisha na aliexpress?
 
Zipi site salama za kununua kwa card directly mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…