Mkuu
1000 digits , hiyo siku, utaisubiri sana kufuatia Watanzania wanataka maendeleo na CCM ndicho chama pekee kinacholeta maendeleo hivyo Watanzania wataendelea kuichagua CCM daima dumu!.
Ushahidi ni usubiri October 28,
Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.
P
CCM mnakosea sana kudhani kuwa watanzania wote bado ni wajinga kwa kiwango cha kuwadanganya .
CCM inarudisha nyuma maendeleo ya nchi .
Sisi Tanzania tuna vijiji tofauti na Ulaya.
Huwezi kutumia bajeti yote kuweka majengo na maofisi mijini huku watu wa vijijini wakiwa na maisha magumu na miundo mbinu duni.
Hivi bunge lina kazi gani kama chama kingine kitashindwa kuleta maendeleo wakati kuna wawakilishi wao wanapiga bajeti ya maendeleo?
Huu ujinga wa CCM wa kutisha wabunge ili pato la nchi litumiwe na mtu mmoja kufuga wanayama na kujijengea kiwanja cha ndege nyumbani kwake ndio maendeleo?
Kwa nini Bunge lisiwe huru ili wabunge wapiganie maslahi ya wapiga kura wao na mgawanyo sawa wa pato la ncho kulingana na hali ya umaskini ilivyokaa.
Hivi Geita na Chato kuna umaskini wa kupeleka pato lote la nchi pale kama kipao mbele cha nchi nzima ukilinganisha hata na Loliondo, Liwale, Kilindi,kiteto, Dodoma vijijini na maeneo mengi ya kigoma,Pemba ,Mafia n.k? Kwa nini wabunge wa maeneo hayo walikaa kimya huku wakiona wazi kuwa Reli,ndege,kiwanja cha mtu binafsi sio mahitaji ya wapiga kura wao?
Bila shaka vitisho ,woga wa kupigwa mashangazi zao na kufukuzwa ubunge na kusakamwa wakipinga ndio sababu ya wao kukubaliana na hiyo mipango ya ajabu ya kuwatia umaskini watanzania wengi huku wachache wanaotumia mitutu ya bunduki kutisha watu wakiendelea kutembea na mabegi ya pesa . Wao pesa hazipungui kwenye mabegi ila wanyonge wanaambiwa pesa sio muhimu bali ndege. Wao hawazipeleki zao kwenye ndege badala yake wanatembea nao kwenye mabegi kugawa kama pipi ili wasifiwe kwao sifa ni muhimu kuliko shida za watu.
Chama kingine kitakuja labda kama Mungu naye ni mwanachama wa CCM ! Chama kingine kitakuaja na dalili yote ipo wazi mwaka huu ,CCM ijiandae mana hakuna mtu atakayewapigania matajiri wa CCM kwa maslahi yao na familia zao. CCM ijiandae kuanzaia Zanzibar mana weshajua kuwa kuwapigania watu kwa dhulma hakujawahi kupata kibali kwa Mungu. Mungu atabadili mioyo ya mamilioni ya watanzania na watajawa na roho ya ujasiri na wengi hawataamini . Nchi yetu tulifikia mahali pa kuvumiliana kisasa lakini amekuja mtu mmoja ameleta siasa za Chuki na kuteka watu na dhulma za kila aina huku watu wakijipendekeza kinafiki.