Tony Laurent
JF-Expert Member
- Jan 5, 2011
- 5,606
- 7,032
Jamani naomba msaada kwa waalimu na wataalamu wa lugha ya Kiingereza. Je, ni kwa mtu ambaye ndio anaanza kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ujumla inatakiwa mwalimu aanze na topic gani na kumalizia na ipi. Kwa ufupi naomba mtiririko mzima wa topic gani inaaza ikifuatiwa na ipi hadi mwisho wa kujifunza lugha nzima ya Kiingereza.
Greeting And Parts Of The Body
Jinunulie kitabu kama 'Teach Yourself English'. Itakufundisha au kuonyesha hatua kwa hatua kadiri unavyohitaji.
Unaweza kutumia Youtube kwenye internet na tafuta Learn English. Zipo websites nyingi sana, kwa mfano:
https://www.youtube.com/watch?v=ixErCnZ8c54#aid=P-UwsoqZMR0
https://www.youtube.com/watch?v=w6E3Qw2eXPA
---------------
Kwa English grammar website hii inafaa kuliko nyingine kadiri nilivyoona:
ENGLISH PAGE - Online English Grammar Book Hapa ni index.
Hii ni Homepage: Advanced English lessons
---------------
Kusoma na kusikiliza Kingereza (at the same time) BBC Worldservice Learning English ni bora.
Learning English - General & Business English
Chini ya General & Business English menu, 6 Minute English na English at Work hasa inafaa.
Learning English - Grammar, Vocabulary & Pronunciation
Pia unaweza kutumia British Council website:
LearnEnglish | British Council
-------------
Kupakua/Download kamusi English-Swahili / Swahili-English nenda kwenye
www.somabiblia.com na chagua link kwenda kamusi (ni website yangu).
Jamani naomba msaada kwa waalimu na wataalamu wa lugha ya Kiingereza. Je, ni kwa mtu ambaye ndio anaanza kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ujumla inatakiwa mwalimu aanze na topic gani na kumalizia na ipi. Kwa ufupi naomba mtiririko mzima wa topic gani inaaza ikifuatiwa na ipi hadi mwisho wa kujifunza lugha nzima ya Kiingereza.
Hili ni jambo ambalo limenitatiza sana na ni vema umeeliza swali hili. Kwa maoni yangu, Greetings and parts of the body haina maana sana, ingawa wasomi wengi watanipinga. Naamini ulisoma kingereza shuleni, sijui silabasi ya TZ iko vipi. Ningependa waTZ wanieleze. Hapa Kenya, Darasa la kwanza wanaanza na Greetings, halafu home, school, parts of the body na kadhalika kwa darasa la kwanza. Lakini katika shule za chekechea, huwa wanaanza na Phonics. Kwa maoni yangu, ni vyema uanze na Phonics (Jinsi ya kusoma Kiingereza.) Kama MTZ, kingereza utakijua kupitia Kusoma...kwa hivyo ni vyema ujue Kudecode English words. Kwa mfano, neno Tide, Swipe, na Wipe zina long vowel (I). Kwa hivyo, unaweza kusoma neno Shike (Sha-i-k), hata kama hujawahi liona. Ukisha zielewa hizo 44 phonemes na over 70 ways in which they can be written, basi unaweza anza kwa ku google 100 words Kwa kuzielewa hizo words kwa ufasaha, utaweza kusoma zaidi asilimia hamsini ya maneno yote ya kiingereza yaliyo katika maandishi.
Most common words in English - Wikipedia, the free encyclopedia
Hivi sasa, naandika kitabu cha kiingereza cha darasa la kwanza hapa Kenya, na jambo hili linanitoa jasho sana.
Kwa hoja nyingine; unaweza kujua jinsi naweza pata vitabu vya darasa la kwanza vya TZ. Asante