Tory Lanes ategemee Mvua ya miaka 23 Jela kwa kumpiga Risasi Megan Thee Stallion

Tory Lanes ategemee Mvua ya miaka 23 Jela kwa kumpiga Risasi Megan Thee Stallion

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2020
Posts
1,667
Reaction score
2,595

9b85967d2a43413706aab9d3f41834fa

Mwanamuziki Tory Lanez pengine akatupwa jela kwa muda usiopungua miaka 23 ikiwa atakutwa na hatia juu ya kesi inayomkabili ya kumpiga risasi rapa wa kike kutoka nchini Marekani Megan Jovon Ruth maarufu Megan Thee Stallion.

Kwa sasa ni takribani mwaka mmoja, tangu mwanamuziki Tory Lanez kukanusha mashtaka ya kumpiga risasi msanii mwenzie Megan, ambapo Lanez ameamua kuweka mgomo wa kuingia makubaliano na waendesha mashtaka kwenye shauri hilo ambalo anadaiwa kumshambulia kwa kumpiga risasi mbili za mguuni msanii wa kike maarufu Megan Thee Stallion mnamo Julai 2020.

Kwa mujibu wa jarida la Rolling Stone la nchini Marekani, Tory Lanez atahitajika kufika mahakamani kwaajili ya kutoa ushuhuda wa kilichotokea kati yake na Megan usiku wa tukio hilo ifikapo Disemba 14, 2021.

Kulingana na sheria za nchi ya Marekani inaelezwa kuwa kesi ya shambulio la namna hiyo ikiwa Lanez atakutwa na hatia, inawezekana akahukumiwa kutumikia kifungo cha mpaka miaka 23 Jela.

©Dar24
 
Back
Top Bottom