Touched: Bradley aomba afie mikononi mwa Defoe

Sir_Mimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2013
Posts
7,171
Reaction score
15,760

Huyu dogo Bradley Lowery shabiki wa Sunderland aliambiwa na madokta kwamba zimebaki siku60 tu afe ambazo zimetimia jana,aliomba kabla hajafa aje shujaa wake mshambuliaji Jermaine Defoe awe nae kitandani wakati izrail anafanya yake.inasikitisha sana aisee mtu kuzijua siku zako za kufa.Mungu amtendee miujiza.
 
Bado anadunda. Naomba kujua Defoe haendi mazoezini wala mechi kwa wakati huu!
 
Hapana alisema naomba Defoe abaki hapa mpka nitakapolala,,,nae Defoe hakuona noma akajilaza dogo alipolala usingizi Defoe akasepa,,,ila sio kwamba alisema akifa Defoe awepo nop nop
Sure kaka...
Bado anadunda. Naomba kujua Defoe haendi mazoezini wala mechi kwa wakati huu!
Dogo karuhusiwa leo nyumbani mkuu..bado Mungu hajamuhitaji bado nadhani.
 
Anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ujulikanao kama neuroblastomia.Baada ya kugunduliwa alichangiwa zaidi ya paund laki saba,timu ya Everton ikitoa laki mbili kati ya hizo, kwa ajili ya matibabu marekani.

Kwa bahati mbaya ilikutwa kansa imesambaa kwa kiasi kikubwa hivyo kuondoa uwezekano wa kupona.Matibabu anayoendelea kuyapata ni yale tu ya kumpunguzia makali ya kansa lakini sio kuimaliza.
Wanamichezo mbalimbali wameendelea kumuonyesha upendo katika kipindi hiki ikiwemo timu ya Sunderland,wachezaji wa Sunderland,Lumelu Lukaku,Pep Guardiola na wengine.
 
Wazungu kwa kuandaa story hawajambo
sana mkuu,wakati hapo china wajanja wanatibu kansa kwa siku kadhaa tuu unarudi kuwa mzima kabisa,na ni wazungu ndio wanaotuaminisha kuwa kansa haitibiki kwa story zao uchwara kama hizi
 
sana mkuu,wakati hapo china wajanja wanatibu kansa kwa siku kadhaa tuu unarudi kuwa mzima kabisa,na ni wazungu ndio wanaotuaminisha kuwa kansa haitibiki kwa story zao uchwara kama hizi
Mkuu kweli usemayo yana ukweli haya?!hivi cancer ingekuwa na dawa kwa gharama yoyote ile unadhani hao wazungu wangekubali watu wao wafe,wakiwapo watu muhimu kama kina Stive Jobs etc!tuache kudanganyana omba Mungu akuepushie maradhi hayo yanatesa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…