TOZO|CORONA: Idadi ya watali nchini imepungua kwa 77%, Mapato yatokanayo na utali yameshuka kwa 87%, Je mnaopinga tozo hadi leo mnalijua hili?

TOZO|CORONA: Idadi ya watali nchini imepungua kwa 77%, Mapato yatokanayo na utali yameshuka kwa 87%, Je mnaopinga tozo hadi leo mnalijua hili?

Pamoja na upungufu mkubwa hivyo wa mapato uliosababishwa na ugonjwa wa Corona mbona serikali haipunguzi matumizi yasiyo ya lazima. Hizo V8 zinatumia mafuta kiasi gani kwa siku nchi nzima? Misafara mikubwa ya viongozi wa kisiasa kwa pesa za serikali je? Rais inatakiwa aongoze kwa mfano kwa kukubali nae alipe kodi kwenye mapato yake ya mshahara nk.
 
Mpaka umeweza kuweka umeme maana yake wewe upo njema, imagine unabundle la kusurf kila uzi una comment na hii ni JamiiForums pekee sijui huko Twitter na IG….
Masikini wa kiukweli kweli hizi tozo na yeye ni kama ardhi na mbingu, hawakutani. Tumezaliwa maisha ya shida na majani ndio lishe yetu kuu, nyie wala kuku zamu yenu sasa kuisoma namba.
karibu chama la u-green
Ndugu yangu mimi natumia bando la chuo na naweka mara moja kwa wiki.

Haya mambo ya kujiita sisi ni donor country ni kuumiza tu walala hoi.Kama Kenya wanapokea misaada kibao ya UVIKO kwa nini sisi tukatae.Kuendelea kukamua walala hoi kwa kupitia tozo ili kufidia kupungua kwa mapato ya utalii ni kuzidi kuongeza umaskini.
 
Kenya wa
Ndugu yangu mimi natumia bando la chuo na naweka mara moja kwa wiki.

Haya mambo ya kujiita sisi ni donor country ni kuumiza tu walala hoi.Kama Kenya wanapokea misaada kibao ya UVIKO kwa nini sisi tukatae.Kuendelea kukamua walala hoi kwa kupitia tozo ili kufidia kupungua kwa mapato ya utalii ni kuzidi kuongeza umaskini.
Wanakopokea hiyo misaada wananchi wanasemaje? Masikini hakombolewi na misaada bro, kamwe haiwezekani. Masikini anakombolewa na juhudi zake mwenyewe.

wangapi unawajua walikuwa choka mbaya lakini leo ni habari nyingine tena bila hata mkono wa mzungu katikati? Tumejilemaza sana, wazungu waje sawa lakini kama partners sio donors.
 
Wewe ni mjinga? Kwani unafikiri sie vyanzo vya mapato au mapato yetu yameongezeka. Watu wenu ni maskini na jobless, waboresheeni maisha na vipato vyao, then leteni hizo tozo hata mara nne ya hizi.
Unakumua pasipo malisho, maana yake mchungaji hayuko serious na kazi yake. Mwisho wa siku hata maziwa kidogo ya kupandia Airbus kila siku kama ilivyoa ada, atayakosa kabisa.
 
Kenya wa

Wanakopokea hiyo misaada wananchi wanasemaje? Masikini hakombolewi na misaada bro, kamwe haiwezekani. Masikini anakombolewa na juhudi zake mwenyewe.

wangapi unawajua walikuwa choka mbaya lakini leo ni habari nyingine tena bila hata mkono wa mzungu katikati? Tumejilemaza sana, wazungu waje sawa lakini kama partners sio donors.
Kwa hiyo unaunga mkono tozo zidumu na kodi katika bia ipungue?
 
Wananchi hawana shida na Tozo,Ila wanataka kujua kwanini leo Tozo, Mbona Mwaka jana hazikuwepo,

Kongole nyingi kwa mleta mada,

Tunahitaji kuwa na serikali inayowajibika kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutoa maelezo ya kina kwani hiki leo sio jana,

Kazi iendelee kiroho safi, Ila muwe mnasema,
 
Unaweza kutueleza kwanini juzi mlipokea ule Mkoppo wa ujenzi barabara vijijini , huku mnaendelea kukata Tozo?

Hata watalii waje wafike billioni hapoa bongo hamna akili za kutumia pesa kwenye maendeleo zaidi ya kujaza hizo pesa kwenye posho na bajeti zenu za mafuta na vikao visivyo na maana wala kichwa.

Endeleeni kula jasho la Wananchi muda ukifika zitawatokea puani hizo.
 
Samia ni mtu anamwogopa Mungu,

Hata tu kupata taarifa za kweli kwamba wataali hakuna tusingeweza kujua,

Tuliaminshwa nchi iko vizuri na uchumi unakuwa kwa kasi kumbe uchumi ulikuwa kwa 2% toka 7%

Tuliambiwa watalii ni kama wote kumbe watalii hakuna,

Binafsi nampongeza sana mama Samia,

Mbele ya Mungu wangu namwahidi kura yangu 2025,

Pamoja na hayo Nashauri Tozo ziendelee tatizo hatukuwa na Taarifa,

Serikali toeni taarifa ,

Sio kutuambia "Vumilieni "

Lazima usema kwanini tuvumilie,
 
HII NCHI NGUMU SANA|WATU WANAPINGA TOZO ZA HIARI WANATAMANI ENZI ZA TRA NA MITUTU YA BUNDUKI,



_________________________________

Kazi iendelee|Tozo ziendelee

Sikilizeni, Mfano, kutoka Wizara ya Maliasili & Utalii FY2021/22 tulitegemea kukusanya jumla ya Tshs 2.7trl kama mapato yatokanayo na Utali kwa matarajio ya kupokea jumla ya watali 1,867,000 but kutokana na COVID-19 tunatarajia kupokea watalii 437,000 sawa na anguko la 77%,na matarajio mapya ya makusanyo ni Tshs 598BL kwa mwaka toka matarajio ya Tshs 2.7trl hii ni sawa na nakisi|pungufu wa Tsh 2.102trl kwa mwaka huu. Wananzengo, hii pesa ya kufidia tunaipataje?

Tukumbushane, Kabla ya Corona kwa mfano, FY 2017/18 mapato yatokanayo na Utali tu yalifikia kiasi cha US$ 2.4BL sawa na Tshs 5.3trl leo Mapato hayohayo ni chini ya Tshs 598BL sawa na anguko la 87% ambayo ni Tsh 4.702trl. Kwa lugha rahisi zaidi ya Tshs 4.7trl tulizopata miaka ya 2010's zitokanazo na Utali zimeyeyushwa na Corona na hazipo tena Serikalini wala kwenye mzunguko,Kumbuka hii Corona si ya CCM, CHADEMA, NCCR, CUF wala TLP ni Ya Mungu na Mungu hakosei, Hii pesa tunaipataje?

Dk Mwigulu Nchemba Waziri wa Fedha na Mipango amesema Serikali ya JMT imekusanya Tshs 48.4BL kwa mwezi moja tu ( wiki nne ) toka kwenye tozo,Kama tozo hizi tulio wengi tutazikubali basi kwa mwaka mmoja wa fedha tutakusanya jumla ya Tshs 581BL ambazo ni zaidi ya hata makusanyo yote ya Wizara ya madini ambayoni ni Tshs 528.24BL kwa mwaka, kwamiaka hii mitano ya Kwanza ya Mama Samia kwa tozo za miamala tu, tutakusanya zaidi ya 3trl kama wapinga maendeleo wa hii nchi hawatashinda hii Vita ya Ujenzi wa nchi bila kumdhulumu yeyote awaye.

Pamoja na Corona, Vituo vya afya 560, Ukarabati wa Hospitali za wilaya 99, Wodi za wagonjwa 201, Vyumba vya madarasa 10,000, Zahanati 1,198, Kilometa 73,242 za Changarawe yote haya lazima yajengwe na njia ni mbili tu, niama TRA wachukue Mitutu ya bunduki wakawatengenezee wafanyabiashara wetu "Presumtive Tax accessment" ili kuwadai kodi hadi za wakati wa JK au Watanzania wote zaidi ya 60M kwa umoja wetu tu-share baraka hizi kwa kuchangia miamia zetu kwenye miamala na tozo nyinginezo zilizopitishwa na bunge ili kuifanya Tanzania kuwa nchi salama kwa yeyote kuishi iwe ni kijijini au mjini,


...tuendelee kumwombea Mama kazi anaipiga ...

..maana yake ni kwamba kuna Watz wengi sana ambao vipato vyao vinategemea sekta ya utalii nao wameathirika kiuchumi na kimapato.

..serikali inayojielewa haiwezi kuongeza tozo au kodi wakati wananchi wake wameathirika kiuchumi au kimapato.

..Na imekosa mapato ya matrillion kutokana na utalii kuporomoka kwanini imekwenda kununua ndege za thamani ya sh trillion 2?
 
HII NCHI NGUMU SANA|WATU WANAPINGA TOZO ZA HIARI WANATAMANI ENZI ZA TRA NA MITUTU YA BUNDUKI,



_________________________________

Kazi iendelee|Tozo ziendelee

Sikilizeni, Mfano, kutoka Wizara ya Maliasili & Utalii FY2021/22 tulitegemea kukusanya jumla ya Tshs 2.7trl kama mapato yatokanayo na Utali kwa matarajio ya kupokea jumla ya watali 1,867,000 but kutokana na COVID-19 tunatarajia kupokea watalii 437,000 sawa na anguko la 77%,na matarajio mapya ya makusanyo ni Tshs 598BL kwa mwaka toka matarajio ya Tshs 2.7trl hii ni sawa na nakisi|pungufu wa Tsh 2.102trl kwa mwaka huu. Wananzengo, hii pesa ya kufidia tunaipataje?

Tukumbushane, Kabla ya Corona kwa mfano, FY 2017/18 mapato yatokanayo na Utali tu yalifikia kiasi cha US$ 2.4BL sawa na Tshs 5.3trl leo Mapato hayohayo ni chini ya Tshs 598BL sawa na anguko la 87% ambayo ni Tsh 4.702trl. Kwa lugha rahisi zaidi ya Tshs 4.7trl tulizopata miaka ya 2010's zitokanazo na Utali zimeyeyushwa na Corona na hazipo tena Serikalini wala kwenye mzunguko,Kumbuka hii Corona si ya CCM, CHADEMA, NCCR, CUF wala TLP ni Ya Mungu na Mungu hakosei, Hii pesa tunaipataje?

Dk Mwigulu Nchemba Waziri wa Fedha na Mipango amesema Serikali ya JMT imekusanya Tshs 48.4BL kwa mwezi moja tu ( wiki nne ) toka kwenye tozo,Kama tozo hizi tulio wengi tutazikubali basi kwa mwaka mmoja wa fedha tutakusanya jumla ya Tshs 581BL ambazo ni zaidi ya hata makusanyo yote ya Wizara ya madini ambayoni ni Tshs 528.24BL kwa mwaka, kwamiaka hii mitano ya Kwanza ya Mama Samia kwa tozo za miamala tu, tutakusanya zaidi ya 3trl kama wapinga maendeleo wa hii nchi hawatashinda hii Vita ya Ujenzi wa nchi bila kumdhulumu yeyote awaye.

Pamoja na Corona, Vituo vya afya 560, Ukarabati wa Hospitali za wilaya 99, Wodi za wagonjwa 201, Vyumba vya madarasa 10,000, Zahanati 1,198, Kilometa 73,242 za Changarawe yote haya lazima yajengwe na njia ni mbili tu, niama TRA wachukue Mitutu ya bunduki wakawatengenezee wafanyabiashara wetu "Presumtive Tax accessment" ili kuwadai kodi hadi za wakati wa JK au Watanzania wote zaidi ya 60M kwa umoja wetu tu-share baraka hizi kwa kuchangia miamia zetu kwenye miamala na tozo nyinginezo zilizopitishwa na bunge ili kuifanya Tanzania kuwa nchi salama kwa yeyote kuishi iwe ni kijijini au mjini,


...tuendelee kumwombea Mama kazi anaipiga ...
😍👍👊💪
 
..maana yake ni kwamba kuna Watz wengi sana ambao vipato vyao vinategemea sekta ya utalii nao wameathirika kiuchumi na kimapato.

..serikali inayojielewa haiwezi kuongeza tozo au kodi wakati wananchi wake wameathirika kiuchumi au kimapato.

..Na imekosa mapato ya matrillion kutokana na utalii kuporomoka kwanini imekwenda kununua ndege za thamani ya sh trillion 2?



Ndio maana wamepunguza matozo karibia mia tatu chifu,

Kilio cha wengi ni sherehe,

Lazima kuwa mzalendo kwa nchi yako otherwise ulegee kwa Mabeberu,

Mimi Samia tu, Tozo kiroho safi kwanza wanaoumia zaidi ni akina Bakresa na akina MO,



Ndio
 
😍👍👊💪

..mtoa mada amejenga hoja ya kuondoa au kupunguza tozo.

..kama sekta ya utalii na uchumi kwa ujumla umekuwa impacted negatively na janga la corona, basi huu siyo wakati sahihi wa kuongeza tozo au kodi na kuwakamua wananchi.
 
Hizo za watalii uliambiwa wamepewa wananchi wa kawaida ambao mnawaongezea kodi na tozo mara mbili mbili?
HII NCHI NGUMU SANA|WATU WANAPINGA TOZO ZA HIARI WANATAMANI ENZI ZA TRA NA MITUTU YA BUNDUKI,



_________________________________

Kazi iendelee|Tozo ziendelee

Sikilizeni, Mfano, kutoka Wizara ya Maliasili & Utalii FY2021/22 tulitegemea kukusanya jumla ya Tshs 2.7trl kama mapato yatokanayo na Utali kwa matarajio ya kupokea jumla ya watali 1,867,000 but kutokana na COVID-19 tunatarajia kupokea watalii 437,000 sawa na anguko la 77%,na matarajio mapya ya makusanyo ni Tshs 598BL kwa mwaka toka matarajio ya Tshs 2.7trl hii ni sawa na nakisi|pungufu wa Tsh 2.102trl kwa mwaka huu. Wananzengo, hii pesa ya kufidia tunaipataje?

Tukumbushane, Kabla ya Corona kwa mfano, FY 2017/18 mapato yatokanayo na Utali tu yalifikia kiasi cha US$ 2.4BL sawa na Tshs 5.3trl leo Mapato hayohayo ni chini ya Tshs 598BL sawa na anguko la 87% ambayo ni Tsh 4.702trl. Kwa lugha rahisi zaidi ya Tshs 4.7trl tulizopata miaka ya 2010's zitokanazo na Utali zimeyeyushwa na Corona na hazipo tena Serikalini wala kwenye mzunguko,Kumbuka hii Corona si ya CCM, CHADEMA, NCCR, CUF wala TLP ni Ya Mungu na Mungu hakosei, Hii pesa tunaipataje?

Dk Mwigulu Nchemba Waziri wa Fedha na Mipango amesema Serikali ya JMT imekusanya Tshs 48.4BL kwa mwezi moja tu ( wiki nne ) toka kwenye tozo,Kama tozo hizi tulio wengi tutazikubali basi kwa mwaka mmoja wa fedha tutakusanya jumla ya Tshs 581BL ambazo ni zaidi ya hata makusanyo yote ya Wizara ya madini ambayoni ni Tshs 528.24BL kwa mwaka, kwamiaka hii mitano ya Kwanza ya Mama Samia kwa tozo za miamala tu, tutakusanya zaidi ya 3trl kama wapinga maendeleo wa hii nchi hawatashinda hii Vita ya Ujenzi wa nchi bila kumdhulumu yeyote awaye.

Pamoja na Corona, Vituo vya afya 560, Ukarabati wa Hospitali za wilaya 99, Wodi za wagonjwa 201, Vyumba vya madarasa 10,000, Zahanati 1,198, Kilometa 73,242 za Changarawe yote haya lazima yajengwe na njia ni mbili tu, niama TRA wachukue Mitutu ya bunduki wakawatengenezee wafanyabiashara wetu "Presumtive Tax accessment" ili kuwadai kodi hadi za wakati wa JK au Watanzania wote zaidi ya 60M kwa umoja wetu tu-share baraka hizi kwa kuchangia miamia zetu kwenye miamala na tozo nyinginezo zilizopitishwa na bunge ili kuifanya Tanzania kuwa nchi salama kwa yeyote kuishi iwe ni kijijini au mjini,


...tuendelee kumwombea Mama kazi anaipiga ...
 
Ndio maana wamepunguza matozo karibia mia tatu chifu,

Kilio cha wengi ni sherehe,

Lazima kuwa mzalendo kwa nchi yako otherwise ulegee kwa Mabeberu,

Mimi Samia tu, Tozo kiroho safi kwanza wanaoumia zaidi ni akina Bakresa na akina MO,



Ndio

..wametuletea matozo mapya yanayoumiza wananchi.

..kwani serikali imechukua hatua gani za kubana matumizi yake?

..Kubana matumizi ya serikali ndio inapaswa kuwa hatua ya mwanzo kabisa, siyo kuwakamua wananchi.
 
Kama hilo wanaliona, kwa nini wananchi pekee ndio wanaofunga mkanda kwa kutoa kodi ili serikali iendeshe mambo yake vema, halafu wao kila leo ni safari tuu!! mara semina na posho za ajabuajabu!!

Serikali ikisema tufunge mkanda, basi ianzie kwao, misafara ipungizwe, semina zikatizwe, safari ziachwe, hapo tutasogea
Naunga mkono

Ufungaji MKANDA umekuwa BIAS,wao atujasikia vya kwao vikiguswa na safari hadi za kwenda kufunua VYUNGU pale Kizimkazi.
 
Kama hilo wanaliona, kwa nini wananchi pekee ndio wanaofunga mkanda kwa kutoa kodi ili serikali iendeshe mambo yake vema, halafu wao kila leo ni safari tuu!! mara semina na posho za ajabuajabu!!

Serikali ikisema tufunge mkanda, basi ianzie kwao, misafara ipungizwe, semina zikatizwe, safari ziachwe, hapo tutasogea
Nakuunga mkono.
Bado hakuna logic ya kuwakata pesa wananchi wa kawaida,hiyo kufunga mkanda ianzie kwa viongozi kwanza kabla haijawafikia raia.
Haiwezekani wakati wa shida hao bado waendelee na maisha yaleyale ya kutumbua pesa kwa safari zisizo na msingi wakitembelea mashangingi.
Hivi umejiuliza kama serikali imeshindwa kupata mapato huyo raia unayemkata tozo anapataje pesa?
 
Back
Top Bottom