SoC01 Tozo mpya za Miamala zitumike kutengeneza Walipa Kodi kwa hiari

SoC01 Tozo mpya za Miamala zitumike kutengeneza Walipa Kodi kwa hiari

Stories of Change - 2021 Competition

michu03

Member
Joined
Dec 1, 2018
Posts
72
Reaction score
39
IMG_20210827_130905_335.jpg


Neno Tozo kwa siku za hivi karibuni limekuwa kama wimbo unaoimbwa na kila mtanzania wa kila hali, hivi sasa tozo za maiamala ya simu hata tozo za majengo ni jambo la kuumiza na selikali imetoa tamko la kusisitiza kwamba tozo haziwezi kuondolewa ikiamini kuwa ndio mojawapo ya njia halali za kujiingizia kipato , lakini kiuhalisia watu wengi walioko mtaaniwanaumia sana na kwa siku za karibuni kumekuwa na matabaka kati ya serikali na watu imetengeneza utofauti kati ya serikali na watu inaowahudumia mtaani.

Ni kawaida kwa watanzania kuyafanyia mzaha hata mambo yanayowaumiza ili kujifurahisha imefikia hatua wanalinganisha Neno Tozo na TZ vitu viwili ambavyo hata havihusiani.

Labda niziainishe athari za kiuchumi zinazoweza kutokana na tozo miongoni ni kama zifuatazo:-

Kuzorota kwa biashara matandaoni
Ongezeko la la tozo itapelekea wakati mgumu sana kwa wafanyabiashara walioanza kuchipukia na kutumia mtandao kwa ajili ya kuuza biadhaa pia kufanya malipo mitandaoni.

Mfumuko wa bei za bidhaa na huduma
Kama kuna ongezeko la fedha katika miamala ya simu ni wazi fika kwamba gharama za huduma au bidhaa zitolewazo mtandaoni zitaongezeka kwa wanaofanya miamala. Hivi sasa kuna hatari ya mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali, mfumuko wa bei uko kwenye tarakimu 3.3% na ongezeko la tozo kinaweza kupandisha hali ya mfumuko zaidi.

Mzunguko wa fedha kudorora
Kutokana na kupungua kwa kasi ya huduma ya kutuma na kutoa fedha basi fika kutakuwa na mdororo wa fedha na kufanya hali ya kiuchumi ya mtu mmoja mmoja kuwa ngumu.

Gharama za maisha ya watu zitaongezeka kuzingatia ongezeko la gharama katka huduma mbalimbali wakati pato la mtu mmoja mmoja likiendelea kuwa lilelile ama kushuka kutokana na athari zinazosababishwa na COVID-19.

Kuyumba kwa sekta binafsi kama makampuni ya simu kutokana na kupungua kwa watumiaji ama matumizi (Expenditure) kupungua.

Dhumuni la makala hii ni kujaribu kuziamsha fikra kuona ni kwa namna gani mamlaka husika , wizara yafedha wanaweza kuyatumia mapato yatokanayo na tozo kutengeneza walipa kodi zaidi na wa hiari lakini pia kwa vijana wenzangu kuibadili changamoto hii kuwa fursa ya kibiashara na kujalibu kuziangazia fursa zitokanazo na tozo.

Ningependa nianze na ushauri kwa wizara ya fedha na mipango:

Hivi karibuni Waziri wa Fedha na mipango Dkt Mwigulu Nchemba alitangaza wamefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi za kitanzania Bilioni 48.4 katika kipindi cha wiki nne za mwanzo toka kuanza kwa tozo hizi na wakaanisha matumizi ya fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa miradi inayosimamiwa na serikalilakini pia kuwezesha huduma mbalimba kama afya, elimu, maji n.kLakini moja ya vitu mhimu vilivyo takiwa kufanywa ni kuhakikisha unatengeneza ama kulifanya zoezi hili liwe endelevu ni lazima uwawezeshe wananchi kiuchumi kwani wao ndio walipa kodi, kuwafanya wazimudu gharama za maisha pia kuwekeza katika miradi itakayohakikisha inakuwa chanzo cha mapato, Kuliko kuwekeza kwenye miradi inayoweza kupelekea rushwa na ubadhilifu kwa watendaji na wasimamizi wasiowaaminifu na kuongeza maumivu zaidi kwa walipa kodi.Ingependeza kungekuwa na miradi yenye lengo la kuendelea kuzalisha walipa kodi na kuongeza makusanyo maradufu.

Mfano najaribu kuwaza iwapo wizara ingeamua kufadhili miradi katika maeneo yafuatayo:-Miezi kadhaa iliyopita Soko la Kariakoo Kitovu cha biashara katika jiji la kibiashara lenye muingiliano wa zaidi ya watu milioni 4, JIJI LA DAR ES SALAAM liliteketea kwa moto, Mali za wafanyabiashara ambao kimsingi wengi wao walitegemea biashara zao kuyaendesha maisha yao ya kila siku pia ziliteketea, Ambao ni walipa kodi na wananchi wa kawaida hakuna jitihada za kuwawezesha zikifanyika.

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiatafakari Ubora, Miundombinu, Utaratibu na Muundo katika soko hili lenye taswira na umaarufu ukanda wa afrika masharariki haviaksi ushindani kimataifa na kutengeneza mapto zaidi.

Nawaza kama pesa ya iliyopatikana katika tozo ingetumika katika ukarabati na kuboresha miundombinuya kisasa,yenye ubora na inayoweza kudhibiti majanga yanayoweza kujitokeza kama moto, kimbunga, mafuriko nk pia usanifu wa viwango na wakuvutia unaoweza kulitangaza soko kimataifa kuvutia wachuuzi, wawekezaji na watalii afrika hata ulaya.

Kuwezesha matumizi ya TEHAMA katika miundo, utendaji kazi, ukusanyaji mapato, Utunzaji kumbukumbu pia katika malipo na manunuzi. Kuongeza viwango vya utaoji huduma na utaratibu rafiki kwa wateja ambapo wafanya biashara ama watoa huduma walete pamoja na wasomi na wataalamu wa wabiashara kutoka taasisi mbalimbali za elimu na vyuo kuwapa mafunzo maalumu ya kuwawezesha ni jinsi gani ya kuhusianisha elimun na biashara, biashara na uhusiano wa kimataifa, Bajeti, Kuandaa mpango wa biashara , Kuweka kumbukumbu za biashara, Elimu ya kulipa kodi, Kujikinga na majanga , Elimu ya bima na Uwekezaji katika soko la hisa. Baada ya ukarabati na mafunzo kukamilika wafanyabiashaara wanawezeshwa kwa kupewa mitaji ama kukopeshwa, wanpewa uhuru wa kufanya biashara chini ya uangalizi wa tasisi za elimu za biashara na wataalamu ili waendelee kukuza biashara zao.

Kuna faida zinazoweza kupatikana kutokana na mpango kama huu ni zifuatazo:-

  • Kuwezesha wakulima na wazalishaji wa bidhaa kupata soko la uhakikika la bidhaa na mazao yao
  • Kuongeza ushindani na kutengeneza soko shirikishi ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara
  • Kusaidia kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja kwa kupunguza mdororo wa mzunguko wa kifedha na kufungua fursa zaidi za kiuchumi, Uwekezaji na utalii na uhusiano wa biashara kimataifa
  • Kuchochea uvumbuzi na matumizi ya teknolojiaa ya habari na mawasiliano. Kusaidia kuongeza mapato yatokanayo na tozo zaidi
  • Kusaidia kuendeleza miundombinu ya barabara na mawasiliano mfanom reli ya kisasa (SGR).

Ipo mipango mingi inayoweza kushabiana na huu ambayo inaweza kuelekezea mapato yatokanayo na tozo kutengeneza mapato mengi zaidi pia kupunguza tatizo la ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu waliopo mtaani kwa mfano kuanzisha benki ya vijana itakayowezesha kutoa mikopo na mitaji kwa vijana wenye uhitaji wa mitaji kuanzisha makampuni ya usimamizi ya wazawa na serikali kuyagawia tenda makampuni iliyaweze kujiendeleza.

Pia Inawekana kutumia Tozo kuchochea uvumbuzi na matumizi ya TEHAMA ambayo yanaanza kuzorota kutokana tozo kuwa upande wa mtandaoni, kuna biashara za mtandaoni zenye faida zinazohusisha watu wengi Kama E- Commerce, Sarafu za mtandao( Crypto-currencies) na vingine kama hivyo.

Kwa kuhitimisha, ningependa kushiriki na wasomaji wa makala hii baadhi ya fursa zinazoweza kupatikana kutokana na changamoto na kupelekea mawazo ya biashara yenye kutengeneza mapato mazuri waswahili wanasema “Kila baya mbolea”.

Kwa mujibu wa Takwimu kutoka Mamlaka y Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kati ya laini 53.1 millioni zilizosajiliwa kisasa 32.7 Millioni zinatumia huduma za kifedha mtandaoni, Huku Tanzania ikiwa na jumla ya watumiaji 29 Millioni wa huduma za Intaneti. Yanga yam zee mpili wanasema “wana watu” na mimi nataka niseme fursa ama biashara ni watu. Ikiwa serikali imeweza kukusanya mapato ya billion 48+ kwa wiki nne tu za ,mwanzo hii inamaana kibiashara kuna watu wengi sana mtandaoni na Mapato ya biashara ya mtandaoni yanakadiliwa kuwa makubwa sana.

Nataka twende taratibu tikichambua changamoto moja hadi nyingine na njia ya kuitatua, Kutokana na swala hili la Tozo waathirika wakubwa ni makundi yafuatayo:-Makampuni ya simu na benki za mtandaoni, Wafanyabiashara wa mtandaoni, Mawakala ambao wote wanawategemea watumiaji wa huduma za kifedha mtandaoni kama watumiaji wa huduma zao.

Katika dunia ya sasa ya mapinduzi ya nne viwanda biashara za mtandao ya kijamii ya kuuza data, sehemu ambapo makampuni yanaweza kupata watu kutangaza biashara zao mfano mzuri ni facebook, Twitter, Google nk.

Najaribu kuwaza kuwepo na platform inayowaunganisha wateja wa huduma za kifedha wa mtandao w uhakika na makampuni ya simu, wafanyabiashara wa mtandao na mawakala walipie kuwapata wateja hao kulingana na idadi ya wateja katika mtandao husika.Hii inakuwa hivi kunakuwa na namna watu wanajiunga na wanajisajili katika mfumo kwa kujaza taarifa zao mhimu na ni mtandao upi wanatumia kutuma na kupokea fedha ili waweze kutuma na kutoa fedha mtandaoni bure taarifa data hizi zinnauzwa kwa makampuni ya simu kutokana na wateja waliojiunga.

Pia kuna malipo ya awali naya mwezi yatakayotakiwa kufanywa na mawakala na wafanyabiashara ili kulipata kundi hili, lakini pia kunaweza kuwa na namna ya kutengeneza pesa kwa kampuni kulipia kufanya matangazo, kutengeneza application na kuiweka kwenye store kama appstore na playstore.Pia ukiachana na hayo kunaweza kuwa na makampuni ya Tax consultant, kuzishauri kampuni za simu na wafnyabiashara wa mtandaoni na namna ambavyo wanaweza kukabiliana na hali , Pia makampuni mfano wa bima ambapo watu na makampuni yatajiunga ili watume na kupokea fedha bure lakini wanafanya malipo kila baada ya kipindi cha muda( subscription) mfano siku, wiki ama mwezi.Ningependa kumaliza na niwakalibishe watu wenye maoni na namna ambayo tunaweza kuibadilisha changamoto ya Tozo na kuwa kama fursa.
 
Upvote 3
Miezi miwili iliyopita Serikali imeanzisha utaratibu mpya wa kujipatia mapato kutokana na muamala ya simu na Tozo nyingine za majengo nk
Hii imekuwa changamoto hasa kwa watanzania wa kipato cha kawaida lakini pia hata kasi ya uvumbuzi wa kiteknolojia katika biashara za mitandao,. Mifumo ya kifedha ya kimtandao pia hata kwa makampuni na taasisi za simu inapungua.
Kwa mujibu wa takwimu kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Kati ya laini 53.1 Milioni zilizosajiliwa kisasa, 32.7 Milioni zinatumia huduma za kifedha mtandaoni, Huku Tanzania ikiwa na jumla ya watumiaji 29 Milioni wa huduma za intaneti, Idadi hii kubwa ya watumiaji wameathirika kwa namna moja ama nyingine katika Tozo hizi mpya za miamala na makato mengine mtandaoni na imepelekea kupungua kwa kasi ya watumiaji wa huduma za kifedha mtandaoni ( watumiaji wa kipato cha kawaida wanaotuma na kupokea fedha) ama maumivu ambayo hawawezi kuyavumilia muda mrefu, lakini pia athari zake kwa sekta binafsi, mawakala, wafanya biashara mtandao, kampuni na taasisi za simu na fedha zinazoguswa moja kwa moja na huduma hizi.
Kwa kuliona hili nimeamua kuleta ubunifu ambao utasaidia kupunguza ama kuondoa changamoto hii hasa kwa waathirika wa huduma za kifedha mtandaoni. Lakini pia kama fursa ya kujipatia kipato, kuchochea ufumbuzi na matumizi ya TEHAMA katika sekta ya fedha.

Naomba unitumie muda wako kidogo nikipitishe katika miundo mbinu minne ya ubunifu huu:-

1. Technical Design

Mfumo wa kidijitali ama (platform) iliyobuniwa ili kuweza kupata taarifa za watumiaji na kuwawezesha watumiaji wa kipato cha chini wa huduma za kifedha mtandaoni ( miamala) kutuma na kupokea fedha kama awali bila kuathiri mapato ya serikali, kampuni na taasisi za simu na sekta binafsi kama mawakala,benki, wafanya biashara wa mitandaoni ni
Mfumo utakao tumia teknolojia na rahisi kiupatikanaji kupitia APP na Website.
Na mfumo huu utawagawa wabia muhimu wa huduma hii katika makundi mawili kulingana na mahitaji yao. Kundi la kwanza ni watumiaji wa kawaida ambao ni wengi kama bidhaa na kundi la pili ni wahitaji wa taarifa ambao ndio watumiaji wa bidhaa nao ni makampuni na taasisi za simu, serikali, mawakala wa huduma za kifedha mtandaoni, wafanya biashara na makampuni mbalimbali.

2. Service Design

Utoaji wa huduma utajikita zaidi kutengeneza jamii ya kimtandao na kukusanya taarifa muhimu za watumiaji ili kuwawezesha kupata huduma kulingana na mahitaji yao. Watumiaji watajisajili katika mfumo uliobuniwa kwa teknolojia kupokea na kutunza taarifa zao na kuwatofautisha watumiaji wa kawaida na wahitaji wa taarifa mfano wa taarifa zitakazotolewa na watumiaji ni Majina, Namba za simu na aina ya mitandao ya simu wanayotumia, email, Je mtumiaji ana umiliki wa nyumba ama amepanga, Idadi ya miamala anayoifanya kwa siku, wiki au mwezi.
Lakini pia mfumo utakuwa na chaguo (option) kwa watumiaji ambao ni mawakala wa huduma za kifedha, wafanya biashara wa mitandaoni, benki na kampuni za simu, mamlaka za serikali kujisajili pia ili kupokea huduma zinazotolewa katika mfumo.

3 Organization Design

Taarifa zinazotolewa na watumiaji ndio kielelezo muhimu na kiunganishi baina ya watoaji taarifa, watunzaji taarifa na wahitaji taarifa.
Ikumbukwe kwamba makundi mawili yanayotenganishwa ili kupata bidhaa na wahitaji wa bidhaa.

4 Revenue Design

Hiki ndio kipengele muhimu kuangazia kwa namna gani mfumo unaweza kujiendesha na kutengeneza faida lakini pia kutimiza malengo ya kuwawezesha wananchi wa kipato cha kawaida kutuma na kupokea fedha bila makato makubwa, lakini pia serikali kujipatia mapato yake na taasisi na kampuni za simu kuendelea kupata faida.
Siku kadhaa zilizopita wizara ya fedha na mipango kupitia waziri wa fedha Dkt Mwigulu Nchemba alitangaza kupitia Tozo serikali imefanikiwa kukusanya bilioni 48.4 kwa kipindi cha wiki nne za kwanza hii inamaanisha kuna mzunguko mkubwa sana wa fedha kupitia mitandao lakini pia inawezekana kutengeneza mapato makubwa sana kupitia huduma za mitandaoni na bunifu mbalimbali za teknolojia.
Zifuatazo ni baadhi ya njia zitakazotumika na mfumo huu kutengeneza mapato na kufanikisha kutimiza malengo:-

* Matangazo
Ukifanikisha kupata watumiaji wengi wanaoweza kujiunga na mfumo ( active users) inawezekana kiyaalika makampuni yaweze kutangaza kupitia mfumo.

* Subscription payment
Hii ni kwa watumiaji wakubwa, wafanyabishara wa mitandaoni, mawakala wa huduma za kifedha mtandaoni, kampuni na taasisi mbalimbali. Kwa mfano ukifanikiwa kuwapata watumiaji hawa 1000000 na kila mwezi wanalipa 10000 kama malipo ya huduma wanayoipata inakutengenezea zaidi ya Bilioni 10 Kwa mwezi.

* Commissions
Malipo yatafanyika kutokana na makubaliano na kampuni za simu ambazo wateja wake wamejiunga kutumia huduma za mfumo mfano watumiaji wa mfumo wa kifedha kwa mujibu wa takwimu ni 30+ Milioni na kampuni kubwa za simu kama Vodacom, Airtel na Tigo zina wateja zaidi ya milioni 5+ kila moja na inafanikisha kuwa na watumiaji waliojiunga kwenye mfumo Milioni 20 kwa kila mteja mmoja kampuni ikitoa Sh 1000 kwa mwezi inamaa inatengeneza 20+ Bilioni kwa mwezi

* Deals and Investment
Kupata uwekezaji na madeal kutoka kampuni mbalimbali lakini pia kampuni za nje zinazotumia mtandao kuuza bidhaa mchumi na malipo yanafanyika kwa kupitia mitandao.

*Direct sales of Virtual goods
Mfano kuuza data(taarifa) kwa mfano wizara ya ardhi na TANESCO hawana data zinazowatofautisha wamiliki wa nyumba na ardhi na wapangaji, Lakini pia mauzo ya hisa nk.
 
View attachment 1911687

Neno Tozo kwa siku za hivi karibuni limekuwa kama wimbo unaoimbwa na kila mtanzania wa kila hali, hivi sasa tozo za maiamala ya simu hata tozo za majengo ni jambo la kuumiza na selikali imetoa tamko la kusisitiza kwamba tozo haziwezi kuondolewa ikiamini kuwa ndio mojawapo ya njia halali za kujiingizia kipato , lakini kiuhalisia watu wengi walioko mtaaniwanaumia sana na kwa siku za karibuni kumekuwa na matabaka kati ya serikali na watu imetengeneza utofauti kati ya serikali na watu inaowahudumia mtaani.

Ni kawaida kwa watanzania kuyafanyia mzaha hata mambo yanayowaumiza ili kujifurahisha imefikia hatua wanalinganisha Neno Tozo na TZ vitu viwili ambavyo hata havihusiani.

Labda niziainishe athari za kiuchumi zinazoweza kutokana na tozo miongoni ni kama zifuatazo:-

Kuzorota kwa biashara matandaoni
Ongezeko la la tozo itapelekea wakati mgumu sana kwa wafanyabiashara walioanza kuchipukia na kutumia mtandao kwa ajili ya kuuza biadhaa pia kufanya malipo mitandaoni.

Mfumuko wa bei za bidhaa na huduma
Kama kuna ongezeko la fedha katika miamala ya simu ni wazi fika kwamba gharama za huduma au bidhaa zitolewazo mtandaoni zitaongezeka kwa wanaofanya miamala. Hivi sasa kuna hatari ya mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali, mfumuko wa bei uko kwenye tarakimu 3.3% na ongezeko la tozo kinaweza kupandisha hali ya mfumuko zaidi.

Mzunguko wa fedha kudorora
Kutokana na kupungua kwa kasi ya huduma ya kutuma na kutoa fedha basi fika kutakuwa na mdororo wa fedha na kufanya hali ya kiuchumi ya mtu mmoja mmoja kuwa ngumu.

Gharama za maisha ya watu zitaongezeka kuzingatia ongezeko la gharama katka huduma mbalimbali wakati pato la mtu mmoja mmoja likiendelea kuwa lilelile ama kushuka kutokana na athari zinazosababishwa na COVID-19.

Kuyumba kwa sekta binafsi kama makampuni ya simu kutokana na kupungua kwa watumiaji ama matumizi (Expenditure) kupungua.

Dhumuni la makala hii ni kujaribu kuziamsha fikra kuona ni kwa namna gani mamlaka husika , wizara yafedha wanaweza kuyatumia mapato yatokanayo na tozo kutengeneza walipa kodi zaidi na wa hiari lakini pia kwa vijana wenzangu kuibadili changamoto hii kuwa fursa ya kibiashara na kujalibu kuziangazia fursa zitokanazo na tozo.

Ningependa nianze na ushauri kwa wizara ya fedha na mipango:

Hivi karibuni Waziri wa Fedha na mipango Dkt Mwigulu Nchemba alitangaza wamefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi za kitanzania Bilioni 48.4 katika kipindi cha wiki nne za mwanzo toka kuanza kwa tozo hizi na wakaanisha matumizi ya fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa miradi inayosimamiwa na serikalilakini pia kuwezesha huduma mbalimba kama afya, elimu, maji n.kLakini moja ya vitu mhimu vilivyo takiwa kufanywa ni kuhakikisha unatengeneza ama kulifanya zoezi hili liwe endelevu ni lazima uwawezeshe wananchi kiuchumi kwani wao ndio walipa kodi, kuwafanya wazimudu gharama za maisha pia kuwekeza katika miradi itakayohakikisha inakuwa chanzo cha mapato, Kuliko kuwekeza kwenye miradi inayoweza kupelekea rushwa na ubadhilifu kwa watendaji na wasimamizi wasiowaaminifu na kuongeza maumivu zaidi kwa walipa kodi.Ingependeza kungekuwa na miradi yenye lengo la kuendelea kuzalisha walipa kodi na kuongeza makusanyo maradufu.

Mfano najaribu kuwaza iwapo wizara ingeamua kufadhili miradi katika maeneo yafuatayo:-Miezi kadhaa iliyopita Soko la Kariakoo Kitovu cha biashara katika jiji la kibiashara lenye muingiliano wa zaidi ya watu milioni 4, JIJI LA DAR ES SALAAM liliteketea kwa moto, Mali za wafanyabiashara ambao kimsingi wengi wao walitegemea biashara zao kuyaendesha maisha yao ya kila siku pia ziliteketea, Ambao ni walipa kodi na wananchi wa kawaida hakuna jitihada za kuwawezesha zikifanyika.

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiatafakari Ubora, Miundombinu, Utaratibu na Muundo katika soko hili lenye taswira na umaarufu ukanda wa afrika masharariki haviaksi ushindani kimataifa na kutengeneza mapto zaidi.

Nawaza kama pesa ya iliyopatikana katika tozo ingetumika katika ukarabati na kuboresha miundombinuya kisasa,yenye ubora na inayoweza kudhibiti majanga yanayoweza kujitokeza kama moto, kimbunga, mafuriko nk pia usanifu wa viwango na wakuvutia unaoweza kulitangaza soko kimataifa kuvutia wachuuzi, wawekezaji na watalii afrika hata ulaya.

Kuwezesha matumizi ya TEHAMA katika miundo, utendaji kazi, ukusanyaji mapato, Utunzaji kumbukumbu pia katika malipo na manunuzi. Kuongeza viwango vya utaoji huduma na utaratibu rafiki kwa wateja ambapo wafanya biashara ama watoa huduma walete pamoja na wasomi na wataalamu wa wabiashara kutoka taasisi mbalimbali za elimu na vyuo kuwapa mafunzo maalumu ya kuwawezesha ni jinsi gani ya kuhusianisha elimun na biashara, biashara na uhusiano wa kimataifa, Bajeti, Kuandaa mpango wa biashara , Kuweka kumbukumbu za biashara, Elimu ya kulipa kodi, Kujikinga na majanga , Elimu ya bima na Uwekezaji katika soko la hisa. Baada ya ukarabati na mafunzo kukamilika wafanyabiashaara wanawezeshwa kwa kupewa mitaji ama kukopeshwa, wanpewa uhuru wa kufanya biashara chini ya uangalizi wa tasisi za elimu za biashara na wataalamu ili waendelee kukuza biashara zao.

Kuna faida zinazoweza kupatikana kutokana na mpango kama huu ni zifuatazo:-

  • Kuwezesha wakulima na wazalishaji wa bidhaa kupata soko la uhakikika la bidhaa na mazao yao
  • Kuongeza ushindani na kutengeneza soko shirikishi ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara
  • Kusaidia kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja kwa kupunguza mdororo wa mzunguko wa kifedha na kufungua fursa zaidi za kiuchumi, Uwekezaji na utalii na uhusiano wa biashara kimataifa
  • Kuchochea uvumbuzi na matumizi ya teknolojiaa ya habari na mawasiliano. Kusaidia kuongeza mapato yatokanayo na tozo zaidi
  • Kusaidia kuendeleza miundombinu ya barabara na mawasiliano mfanom reli ya kisasa (SGR).

Ipo mipango mingi inayoweza kushabiana na huu ambayo inaweza kuelekezea mapato yatokanayo na tozo kutengeneza mapato mengi zaidi pia kupunguza tatizo la ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu waliopo mtaani kwa mfano kuanzisha benki ya vijana itakayowezesha kutoa mikopo na mitaji kwa vijana wenye uhitaji wa mitaji kuanzisha makampuni ya usimamizi ya wazawa na serikali kuyagawia tenda makampuni iliyaweze kujiendeleza.

Pia Inawekana kutumia Tozo kuchochea uvumbuzi na matumizi ya TEHAMA ambayo yanaanza kuzorota kutokana tozo kuwa upande wa mtandaoni, kuna biashara za mtandaoni zenye faida zinazohusisha watu wengi Kama E- Commerce, Sarafu za mtandao( Crypto-currencies) na vingine kama hivyo.

Kwa kuhitimisha, ningependa kushiriki na wasomaji wa makala hii baadhi ya fursa zinazoweza kupatikana kutokana na changamoto na kupelekea mawazo ya biashara yenye kutengeneza mapato mazuri waswahili wanasema “Kila baya mbolea”.

Kwa mujibu wa Takwimu kutoka Mamlaka y Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kati ya laini 53.1 millioni zilizosajiliwa kisasa 32.7 Millioni zinatumia huduma za kifedha mtandaoni, Huku Tanzania ikiwa na jumla ya watumiaji 29 Millioni wa huduma za Intaneti. Yanga yam zee mpili wanasema “wana watu” na mimi nataka niseme fursa ama biashara ni watu. Ikiwa serikali imeweza kukusanya mapato ya billion 48+ kwa wiki nne tu za ,mwanzo hii inamaana kibiashara kuna watu wengi sana mtandaoni na Mapato ya biashara ya mtandaoni yanakadiliwa kuwa makubwa sana.

Nataka twende taratibu tikichambua changamoto moja hadi nyingine na njia ya kuitatua, Kutokana na swala hili la Tozo waathirika wakubwa ni makundi yafuatayo:-Makampuni ya simu na benki za mtandaoni, Wafanyabiashara wa mtandaoni, Mawakala ambao wote wanawategemea watumiaji wa huduma za kifedha mtandaoni kama watumiaji wa huduma zao.

Katika dunia ya sasa ya mapinduzi ya nne viwanda biashara za mtandao ya kijamii ya kuuza data, sehemu ambapo makampuni yanaweza kupata watu kutangaza biashara zao mfano mzuri ni facebook, Twitter, Google nk.

Najaribu kuwaza kuwepo na platform inayowaunganisha wateja wa huduma za kifedha wa mtandao w uhakika na makampuni ya simu, wafanyabiashara wa mtandao na mawakala walipie kuwapata wateja hao kulingana na idadi ya wateja katika mtandao husika.Hii inakuwa hivi kunakuwa na namna watu wanajiunga na wanajisajili katika mfumo kwa kujaza taarifa zao mhimu na ni mtandao upi wanatumia kutuma na kupokea fedha ili waweze kutuma na kutoa fedha mtandaoni bure taarifa data hizi zinnauzwa kwa makampuni ya simu kutokana na wateja waliojiunga.

Pia kuna malipo ya awali naya mwezi yatakayotakiwa kufanywa na mawakala na wafanyabiashara ili kulipata kundi hili, lakini pia kunaweza kuwa na namna ya kutengeneza pesa kwa kampuni kulipia kufanya matangazo, kutengeneza application na kuiweka kwenye store kama appstore na playstore.Pia ukiachana na hayo kunaweza kuwa na makampuni ya Tax consultant, kuzishauri kampuni za simu na wafnyabiashara wa mtandaoni na namna ambavyo wanaweza kukabiliana na hali , Pia makampuni mfano wa bima ambapo watu na makampuni yatajiunga ili watume na kupokea fedha bure lakini wanafanya malipo kila baada ya kipindi cha muda( subscription) mfano siku, wiki ama mwezi.Ningependa kumaliza na niwakalibishe watu wenye maoni na namna ambayo tunaweza kuibadilisha changamoto ya Tozo na kuwa kama fursa.
1 done sijasoma wote ila nimeuelewa.
 
Yaani upo unakaa chini unatumia muda wako na akili yako kuisaidia SERIKALI kunyonya wananchi wake?

Hivi kwanini msibuni solutions kwa ajili ya wananchi na watanunua tu kwa upendo?

Wewe unaisaidia serikali kunyang'anya watu wake pesa zao halali na mimi najenga muundo wa ku-bypass huo uonevu

Sipatagi picha hivi inakuaje mwanadamu anaisaidia serikali kwa lolote lile tena baya zaidi ni kuisaidia kukata hela jasho halali la wananchi waliochoka?
Nafikiri utakuwa haujaielewa maana yangu katika hili ukisoma andiko langu la kwanza nimepelezea athari za Tozo na kwa sababu serikali imetangaza haitofuta Tozo nimejaribu pia kushauri ni kwa namna gani wanaweza kuzitumia fedha wanazokusanya kuwawezesha wananchi kiuchumi zaidi ya kuwekeza kwenye miradi.
Lakini pia solution hii niliyoibuni ni kwa ajili ya vijana wasio na ajira wasomi na wataalamu wa teknolojia wanaweza kuitumia kuwapunguzia makali ya Tozo wananchi wanyonge na wao wenyewe iwe kama njia ya kujitengenezea kipato lengo la wazo hili ni kuwasadia watu kutumia njia za kifedha mtandaoni kama mwanzo lakini pia serikali kujipatia mapato yake.
Pia hata kwa wasomaji kuwa fikirisha kwenye kila changamoto yoyote kuna fursa.
Nakushauri ipitie tena nilichoandika kwa umakini bila chuki utaelewa, Asante!
 
Lakini pia hongera kwa kuamua kujenga muundo kuby-pass uonevu huu.
 
Serikali akishakusanya hela yake huwezi mpangia cha kufanyia

Bado hujatoa suluhisho la hela ya serikali inatoka wapi wakati una claim mwananchi hakatwi popote

Hapa una suggest Payment System mpya itakayomeza payment systems zingine mfano Mpesa,Tigopesa,etc,hawatakubali hawa,they will kill you before you arrive.

Naona unataja eti hela itapatikana kwenye revenues za advertisement kuilipa ile hela ya serikali,hii haiwezekani maana watumia App TZ ni wachache compared na wanaotumia USSD,na kwenye USSD utatangazia wapi mzee na hakuna nafasi?

Hiyo kutuma hela bure na serikali kupata makato yake hapa naona ni ndoto za mchana

Na mobile money kutoka mitandao ya simu haiwezi kukubali wewe uwe juu yao,they will cut you off right away maana it is in not their best interest kukuza dude lije kua competitor later on.

Na kwenye andiko lako,sijaona solution yeyote ya mtu kutuma hela bure na the same time eti serikali ipate yale makato yake which are astronomical sijui utayatolea wapi maana numbers do not add up kabisa.
Hatuipangii serikali cha kufanya lakini kama wadau tunaishauri namna ambavyo wanaweza kutumia mapato wanayopata kuwasadia wananchi na kuwawezesha zaidi kiuchumi.
 
Kwa kujibiwa takwimu Tanzania tuna zaidi ya watu 20 wanaotumia intaneti na ukiangalia kama serikali inaweza kuzalisha billion 48+ kwa mwezi unaweza kuimagine how the market value is big online lakini kumbuka tayari kuna kikwazo cha Tozo ambapo makampuni unayoclaim yatabania yanaathirika umekuja na misaada watanzania vipi?
Mfano mzuri ni kopa gas wamekuwa haraka kuliko kampuni zinazouza gas hapa Tanzania and still ni partners wa kampuni hizo.
Upande wa Revenue nimejaribu kuelezea zaidi ya njia nne ambazo zinaweza kutoa mapato and I wonder why una stick kwenye njia moja na unatumia njia hiyo kuhitimisha as if pia njia nyingine haziwezi kufanya kazi.
 
Naona mkuu unazunguka around and around...

Hebu nieleze kwa kinaga ubaga,serikali imenikata tozo ya 2000 kwenye Luku,hebu nidadavulie hiyo 2000 serikali iitumieje eti mimi mimi mwananchi niwezeshwe kiuchumi like how?

Dadavua hiyo 2000 hapo juu kwa mahesabu sahihi

Nachoona hapa,unataka serikali ikupe hiyo 2000 uishike ujaribu kuzungusha unakojua wewe kwa hoja za kusaidia wananchi of which it is not true

Bado hujaweka wazi,na hutakaa uweke wazi maana unajua its a pile of bullshit unataka wewe uwashikie serikali hiyo hela of which it is another series of nonsense both kwa wananchi for one na serikali kwa upande mwingine.

Tukuamini wewe ushike hizi hela wewe kama nani na kwa lipi?Hela unazipeleka wapi?Huwezi taja mzee
Labda nikupe summary ya andiko langu nimejaribu kuelezea mambo yafuatayo kwa mifano:-
* Athari zitokanazo na tozo
*Nimemshauri serikali ni kwa jinsi gani unaweza ukatumia makusanyo inayopata katika uwezeshaji wananchi kiuchumi na nimeanisha mifano mbalimbali.
Na
* Na mwisho nimejaribu kushare na vijana ni kwa namna gani wanaweza kuona fursa katika kila changamoto.
Kwa maana hiyo swali lako linajitokeza moja kwa moja katika kipengele cha pili ambacho nimetoa mifano mingi na ya kutosha tu si kwamba nahitaji serikali unipatie mapato inayowapata katika Tozo lahasha bali nafasi yangu kupitia story of change ni kushauri mambo serikali inaweza kuyafanya na yakawanufaisha wananchi kiuchumi.
 
SERA YA TAIFA YA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI.
Imeeleza bayana baadhi ya mambo yafuatayo:-
*Hali halisi ya wananchi kiuchumi na ushiriki wa wananchi katika shughuli za uchumi wa kisasa ni duni, hali inayopingana na dhana ya kuleta maendeleo yanayonufaisha na kutoa nafasi kwa wananchi wengi.
* CHANGAMOTO
Vikwazo vinavyowakabili wananchi katika kushiriki kikamilifu shughuli za uchumi na maendeleo
  • Upatikanaji wa mitaji
  • Ukosefu wa masoko na ajira
*Ukosefu wa ujuzi na uzoefu, upungufu wa mafunzo, elimu, mila, desturi na mitazamo
* Ukosefu wa ushirikiano
Aidha vikwazo vingine vya jumla ni pamoja na
*Udhaifu wa mifumo ya kodi, Sheria, kanuni, leseni na huduma za kiserikali.
*Upungufu wa miundombinu ya kiuchumi nk
 
DIRA YA MAENDELEO YA 2025
Imeelekeza yafuatayo
* Kuwapa nafasi wananchi wanyonge, kuweka mazingira mazuri ya ujenzi wa uchumi imara unaoweza kuhimili ushindani katika soko la dunia na utandawazi.
MUELEKEO
  • Uwezeshaji utazingatia sekta binafsi
  • Italenga haswa maeneo yenye kuleta matokeo kwa haraka hasa yanayogusa maisha ya wananchi ujasiriamali, kilimo, uvuvi, ufugaji, misitu nk
*Aidha pia kuwezesha walioko tayari katika sekta hizo kufanya vizuri zaidi
* Na mwisho kuwezesha wananchi kujenga uwezo wa ushindani katika soko la ndani, soko la EAC, soko la SADC na masoko ya jumuiya nyingine duniani.
Haya yote ni baadhi ya mambo niliyoyaelezea na kutoa mifano halisi ni kwa namna gani serikali inaweza kuwawezesha wananchi kiuchumi, kutengeneza walipa kodi wengi wa wa hiari na kusukuma maendeleo haraka ili kupunguza maumivu kwa wananchi katika suala zima la Tozo.
Kupitia mapato inayowapata serikali inaweza kujikita zaidi katika sera ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na dira yake ya maendeleo ya 2025.
 
Sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi
Screenshot_20210909-150956.jpg
Screenshot_20210909-150745.jpg
Screenshot_20210909-150840.jpg
 

Attachments

  • Screenshot_20210909-150745.jpg
    Screenshot_20210909-150745.jpg
    37.1 KB · Views: 10
  • Screenshot_20210909-150745.jpg
    Screenshot_20210909-150745.jpg
    37.1 KB · Views: 10

Tozo mpya za Miamala zitumike kutengeneza Walipa Kodi kwa hiari
 
Back
Top Bottom