Tozo ya uzalendo inatakiwa isizidi gharama za muamala, iwe 'fixed', iwe na muda maalum na iwe hiari

Tozo ya uzalendo inatakiwa isizidi gharama za muamala, iwe 'fixed', iwe na muda maalum na iwe hiari

Joined
Feb 18, 2019
Posts
53
Reaction score
539
Haya ni maoni yangu juu ya hii tozo ya uzalendo (Ingawaje hili jina limekaa fyongo sana, kwa nini unitoze kwa sababu mimi ni mzalendo?):

  1. Serikali hasa wizara husika inapaswa kuweka benchmark/fixed rate ambayo kila mzalendo atakatwa kiwango sawa bila kujali kiwango cha muamala anaofanya. Uzalendo ni uzalendo, sote tunapaswa kukatwa kiwango sawa bila kujali ukubwa wa muamala anaofanya mtu. Kitu ambacho hamkijui ni kwamba mkiweka fixed amount ambayo ni affordable kwa kila mtu basi miamala itakuwa mingi na mtakusanya kiwango kikubwa tofauti na sasa. Kwa sasa mnachoambulia ni ile miamala ya dharura ambayo mtu anakuwa hana namna sababu amebanwa.
  2. Haiwezekani mtu anatuma 1000,000/=, gharama za muamala ni lets say ni 3500/= halafu tozo ya uzalendo ni 8000/=. Hii haijakaa sawa na itafanya watu waache kufanya miamala na mtakosa vyote kodi na tozo. Kwa hizo gharama ni bora nitume hizo pesa kama percel tuu kwa njia zingine kama hamna dharura.
  3. Serikali inatakiwa ituambie wananchi hii tozo itaenda kwa muda gani, miezi, mwaka, miaka ama muongo kabisa. Sababu ya hizi tozo mmetuambia ni za kujenga barabara za vijijini na vituo vya afya. Lakini hamjatuambia gharama za kujenga hizo barabara na vituo ni kiasi gani, tunapaswa kujua ili hayo makusanyo ya makato yakitimia kiasi kinachotakiwa kwa hizo shughuli basi msitishe makato. Kunatakiwa kuwe na cut-off limit ya muda wa makusanyo pamoja kiasi cha makusanyo sababu "uhitaji" wa hizo huduma utaendelea kuwepo milele na milele sababu kila siku watu wanaendelea kuzaliana na uhitaji utaendelea kuwepo tuu.
  4. La mwisho kabisa kwa kuwa mmetuambia hii tozo ni ya uzalendo na uzalendo si kulazimishana basi napendekeza iwe ni hiari ya mtu kuchangia ama kutokuchangia. Pia mchangiaji apewe uhuru wa kuchangia kile anachoweza ku-afford sio serikali kuweka rates inazotaka yenyewe.
Tofauti na hapo basi serikali itegemee kuona namba ya miamala ikipungua siku hadi siku.
 
Kama baba yako ndio serikali kampe huu ushauri atakushukuru kinyume chake unaleta ujinga.

Hii tozo ni kodi kama zingine sio 20,000 ya vitambulisho vya ujasiliamali.
 
Nimetoa elfu 60,000 nimekatwa 4775 ,hiyo ni sawa na hela ya kununua kilo moja ya unga na nyama nusu.Hizi tozo hawamajaa hawakuwaza vizuri kwasababu wao wapo kwenye V8 wanapigwa na AC mda wote ,mfano mmoja wao kule bungeni aseme wakatwe tozo ya uzalendo sh 100,000 kwa mwezi mbali na PAYE kama hawajatoana damu mle
 
Kama baba yako ndio serikali kampe huu ushauri atakushukuru kinyume chake unaleta ujinga.

Hii tozo ni kodi kama zingine sio 20,000 ya vitambulisho vya ujasiliamali.
baba yake kaingiaje kwenye hoja ,tozo ikiwekwa unakata mauno ,ikipunguzwa unakata mauno ,hata ikifutwa utakata mauno ,ccm tumeshawazoea Kama vilaza kila kitu mnapiga makofi
 
Nimetoa elfu 60,000 nimekatwa 4775 ,hiyo ni sawa na hela ya kununua kilo moja ya unga na nyama nusu.Hizi tozo hawamajaa hawakuwaza vizuri kwasababu wao wapo kwenye V8 wanapigwa na AC mda wote ,mfano mmoja wao kule bungeni aseme wakatwe tozo ya uzalendo sh 100,000 kwa mwezi mbali na PAYE kama hawajatoana damu mle
Ulitaka ukatwe ngapi Ili ujue kuwa waliwaza vizuri?
 
Ulitaka ukatwe ngapi Ili ujue kuwa waliwaza vizuri?
afadhali kama awali siyo wanakaa chini na akili zao pombe kuja kupandisha mara tatu na zaidi,bungeni wamejaa vilaza tu wanaojuangalia wao tu
 
Ni akili za nguruwe pori kumkata kodi ya jengo mtu ambaye hajajenga
 
Uwezo wa watawala wetu kubadilisha rasilimali zote tulizonazo kuwa hela umekwama, ndio maana wanataka mlipe kodi, na sasa kila kitu kimepanda bei. Soon tutasikia na vyoo vya jiji wanapandisha bei.
 
Sidhani kama huo ujenzi tunaoambiwa utakuwa na mwisho maana ni miaka nenda rudi tunasikia haya.

Madarasa yanajengwa kila Mwaka na hayajawahi kutosha...bidii ya Wananchi kuzaana nayo ipo juu maana elimu ya uzazi wa mpango hawana.

Kiufupi ni mpaka pale tutakapoweza kuhamisha digrii zetu za uchumi kwenye hali halisi, bila hivyo tusitarajie mijuiza zaidi ya kutumia hizo digrii kujitambia nazo "mimi ni dokta" alafu basi.

Nchi tunahitaji shughuli za Kiuchumi kupitia Viwanda, huduma za kitalii, Michezo, sanaa n.k....sasa kwa kuwa akili zimegota maeneo hayo njia pekee na ya mkato ni kama hiii ya kukwangua kilichopo mbele yao.
 
Uwezo wa watawala wetu kubadilisha rasilimali zote tulizonazo kuwa hela umekwama, ndio maana wanataka mlipe kodi, na sasa kila kitu kimepanda bei. Soon tutasikia na vyoo vya jiji wanapandisha bei.
Uwezo wa watawala wetu kubadilisha rasilimali zote tulizonazo kuwa hela umekwama, ndio maana wanataka mlipe kodi, na sasa kila kitu kimepanda bei. Soon tutasikia na vyoo vya jiji wanapandisha bei.
Watakimbilia huko kwenye Vyoo vya kulipia, Maegesho ya Magari n.k...maana hazihitaji akili nyingi ni kuamka tu na kutoa maagizo.
 
Sidhani kama huo ujenzi tunaoambiwa utakuwa na mwisho maana ni miaka nenda rudi tunasikia haya.

Madarasa yanajengwa kila Mwaka na hayajawahi kutosha...bidii ya Wananchi kuzaana nayo ipo juu maana elimu ya uzazi wa mpango hamna.

Kiufupi ni mpaka pale tutakapoweza kuhamisha digrii zatu za uchumi kwenye hali halisi basi tusitarajie mijuiza zaidi ya kutumia hizo digrii kujitambia nazo "mimi ni dokta" alafu basi.

Nchi tunahitaji shughuli za Kiuchumi kupitia Viwanda, huduma za kitalii, Michezo na n.k....sasa kwa kuwa akili zimegota maeneo hayo njia ya mkato ndio hiii ya kukwangua kilichopo mbele yao.
Shida watu hawahoji...., Tunaambiwa wahitaji elimu wanaongezeka hivyo tunahitaji madarasa zaidi..., swali ni kwamba mbona hatuoni idadi ya waajiriwa (waalimu inaongezeka)? Au wanafunzi wanakwenda kufundishwa na Buibui ?

Hizi ni Brah Brah Brah za kisiasa tu....
 
Naunga mkono hoja, kuwe na option ya kumuuliza mhusika kama angependa kuchangia au laa......maana tuliambiwa mwanzo hiyo ni solidarity fund ikiashiria kwamba ni mchango wa hiyari lakini baadaye imegeuka kuwa kodi.
 
Back
Top Bottom