Tozo za Majumbani ni kero

Tozo za Majumbani ni kero

Chiblak

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2014
Posts
662
Reaction score
921
Habari wanajamvi poleni na majukumu ya kila siku. Moja kwa moja twende kwenye mada yetu.

Aisee kumekua na hili suala la kutozana tozo mbalimbali ambazo baadhi zimekua sahihi na nyingine si sahihi. Kumekua na tozo ya takataka (sahihi) na pia tozo ya ulinzi shirikishi (si sahihi).

Tozo ya takataka, hii kwangu naona ni sahihi japo na yenyewe ina mapungufu kadhaa. Kawaida tunalipishwa 2000 mpaka 3000 kwa kila kaya kitu ambacho si sahihi kwani kila kaya inazalisha taka kwa kiwango tofauti. Kwa mfano kuna mabachelor wasioshinda nyumbani kabisa na wengine hurudi nyumbani kwa aijli ya kulala tu, kwangu si sahihi kuwatoza kiwango sawa na kaya ya Mama Ally yenye wanafamilia sita.. Badala yake kungekua na mfumo wa kutoza kwa nyumba ili wakazi wa nyumba husika wapangiane wenyewe viwango vya kutozana. Mbaya zaidi watozaji hawatoi risit.

Tozo ya ulinzi shirikishi, hii kwangu ndio si sahihi kabisa kwani tunatozwa 2000 mpaka 3000 kwa kila kaya ila bado watu wanaibiwa na kujeruhiwa kila kukicha. Mimi Nina swali la kuhoji hapa.... Hawa shirikishi tunaowalipa si ni kwa aijli ya ulinzi na usalama wetu na mali zetu? Sasa inamaana inapotokea watu kuibiwa na kujeruhiwa tuna haki ya kuwa hold responsible Hawa watu?Je na wao wanao wajibu ku refund upotevu wa mali na majeraha ya watu? Na Je jeshi letu la polisi Lina majukumu gani ikiwa shirikishi wasio na mafunzo yoyote ya kijeshi wanapewa jukumu la kumlinda raia mwenzake? Mwisho shirikishi wamewekwa kwa mujibu wa sheria ni Nani mwenye wajibu wa kuwalipa?

Mwisho .... Hizi tozo hupangwa huko serikali za mitaa pasipo hata sisi wana mtaa kushirikishwa!.. kumalizia hata Kama tutashirikishwa na kukubaliana basi tuzingatie utoaji wa risit za EFD.
 
Huku Mbezi tunalipa elfu kumi takataka hata hatuelewi. Tunahitaji mkurugenzi wa wilaya ya kinondoni atoe taarifa rasmi bei ya takataka kwa kaya moja ni kiasi gani.

Unakuta roli bovu sana linapita mara 3 kwa wiki na nyumba moja inachangia elfu kumi hii si sawa. Huu ni unyanganyi chini ya serikali awamu ya sita.
 
Nasikia matatizo haya yameanzia manispaa maana wao ndio wanatoa muongozo wa eneo fulani labda mikocheni takatataka kila nyumba itie elfu 15. Huu ni utapeli na una chonganisha utawala na wananchi punguzeni hizi tozo shs 3000 si mbaya.
 
Huku Buza hakuna tozo ya takataka, bali kila Jumamosi au Jumapili unapeleka taka zako barabarani gharama utatajiwa pale.
Mfuko wa kilo 25 ni 1k.
Mfuko wa kilo 50 ni 2k.

Ni hayo tu, ila ya ulinzi ni 2k kwa mwezi.
Jap sijawahi kupishana hata na sungusungu yeyote yule usiku wa manane.
 
Polichi kazi yao n kuilinda serikal iliyopo madarakan na sio raia

Kwa kwel kwa hili la ulinzi shirikishi na bado watu tunaibiwa ni ushenzi
 
Hii imekua kero,watu wanabuni mbinu za upigaji kiholelaholela,eti hawataki mashimo ya takataka.
 
Tozo ya takataka ni sahihi bila kujali unazalisha taka nyingi au chache usafi ni muhimu na swala la pesa lazima mlingane kama unadhani unazalisha chache ba na wewe zalisha nyingi muende sawa.
Swala la ulinzi shirikishi kwanza inabidi ujue hawa watu wanalinda na malungu hawana siraha za kutisha hivyo ni ngumu kupambana na mtu mwenye "mkwaju" anapovamia pia kuna swala la malipo hawa jamaa huwa wanapigwa panga sana Hela yao malipo na viongozi wao hivyo ni vizuri kufatilia kinacholipwa kinamfikia muhusika inavyotakiwa hii inaweza kusaidia kuwaondolea tamaa hao walinzi lakini pia unaweza kuona wizi bado upo ila ukisema uwatoe walinzi wizi ndio ukazidi maradufu
 
Habari wanajamvi poleni na majukumu ya kila siku. Moja kwa moja twende kwenye mada yetu.

Aisee kumekua na hili suala la kutozana tozo mbalimbali ambazo baadhi zimekua sahihi na nyingine si sahihi. Kumekua na tozo ya takataka (sahihi) na pia tozo ya ulinzi shirikishi (si sahihi).

Tozo ya takataka, hii kwangu naona ni sahihi japo na yenyewe ina mapungufu kadhaa. Kawaida tunalipishwa 2000 mpaka 3000 kwa kila kaya kitu ambacho si sahihi kwani kila kaya inazalisha taka kwa kiwango tofauti. Kwa mfano kuna mabachelor wasioshinda nyumbani kabisa na wengine hurudi nyumbani kwa aijli ya kulala tu, kwangu si sahihi kuwatoza kiwango sawa na kaya ya Mama Ally yenye wanafamilia sita.. Badala yake kungekua na mfumo wa kutoza kwa nyumba ili wakazi wa nyumba husika wapangiane wenyewe viwango vya kutozana. Mbaya zaidi watozaji hawatoi risit.

Tozo ya ulinzi shirikishi, hii kwangu ndio si sahihi kabisa kwani tunatozwa 2000 mpaka 3000 kwa kila kaya ila bado watu wanaibiwa na kujeruhiwa kila kukicha. Mimi Nina swali la kuhoji hapa.... Hawa shirikishi tunaowalipa si ni kwa aijli ya ulinzi na usalama wetu na mali zetu? Sasa inamaana inapotokea watu kuibiwa na kujeruhiwa tuna haki ya kuwa hold responsible Hawa watu?Je na wao wanao wajibu ku refund upotevu wa mali na majeraha ya watu? Na Je jeshi letu la polisi Lina majukumu gani ikiwa shirikishi wasio na mafunzo yoyote ya kijeshi wanapewa jukumu la kumlinda raia mwenzake? Mwisho shirikishi wamewekwa kwa mujibu wa sheria ni Nani mwenye wajibu wa kuwalipa?

Mwisho .... Hizi tozo hupangwa huko serikali za mitaa pasipo hata sisi wana mtaa kushirikishwa!.. kumalizia hata Kama tutashirikishwa na kukubaliana basi tuzingatie utoaji wa risit za EFD.
Hizo tozo zenyewe zina mahesabu ya CAG?
 
Watoe risiti za EFD ili serikali nayo inufaike na biashara hizi.
 
Tozo ya takataka ni sahihi bila kujali unazalisha taka nyingi au chache usafi ni muhimu na swala la pesa lazima mlingane kama unadhani unazalisha chache ba na wewe zalisha nyingi muende sawa.
Swala la ulinzi shirikishi kwanza inabidi ujue hawa watu wanalinda na malungu hawana siraha za kutisha hivyo ni ngumu kupambana na mtu mwenye "mkwaju" anapovamia pia kuna swala la malipo hawa jamaa huwa wanapigwa panga sana Hela yao malipo na viongozi wao hivyo ni vizuri kufatilia kinacholipwa kinamfikia muhusika inavyotakiwa hii inaweza kusaidia kuwaondolea tamaa hao walinzi lakini pia unaweza kuona wizi bado upo ila ukisema uwatoe walinzi wizi ndio ukazidi maradufu
Mkuu,hii haari ya kulipa ulinzi shirikishi ni sawa na kuklipa protection money kwa gangs za wahuni ambayo kwangu mimi ni ishara ya kufeli kwa uongozi katika jamii.Kama eneo lina tatizo la uhalifu basi polisi ndio wanaopaswa kuwajibika kutoa ulinzi kama wameshindwa uweke utaratibu wa kisheria kuhusu hawa sungu sungu na watambulike na kulipwa kwa mujibu wa haki zao.Sio kukusanya vijana wahuni na kuwalipa pesa ili wasifanye uhuni na mwisho wake wanakuwa wanawafanyia watu wasiokuwa na hatia harassment za kila namna
 
kampuni ya taka huko ilala aifola mpaka wamekuwa matajiri umenunua mabasi ya kwenda kigoma dar ofisi yao ipo karibu na nssf ilala. wameacha kusomba taka
 
Back
Top Bottom