Tozo zatajwa na Rais Samia kupandisha mabando

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa Jijini Dodoma leo ameshiriki hafla ya utiaji saini mikataba ya miradi ya kufikisha huduma za mawasiliano ya simu katika Kata 763 nchini na miongoni mwa aliyoyasema ni kuhusu Watoa huduma za mitandao ya simu kudai tozo wanazowekewa ni kubwa hasa kwenye mamlaka za Serikali na Hifadhi mbalimbali na kwamba tozo hizo sasa ndizo zinafanya hata mabando yao kuwa ya bei juu.

Rais Samia amesema “Tozo moja waliyoilalamikia ni ile ambayo Mh.Spika ameizungumza tozo ya kupitisha mkongo kwenye eneo la akiba ya barabara”

“Kuna Taasisi kadhaa zinatumia maeneo yale tozo zipo chini lakini mkongo ni dola Elfu 1 kupitisha kwenye maeneo yale, sasa hiyo haiwi bure wanakwenda kutuongezea gharama ya bando, lazima Serikali tuliangalie hili ili kushusha gharama”
 
Zile tozo nyingine za miamala ya simu mbona hatuambiwi zinakusanywa ngapi na kupelekwa wapi?
 
Hapa watu tuchangie kwa staha tafadhali.
===
Lakini, Mheshimiwa Waziri wa Wizara husika alisema kama bando linakuwa bei kubwa basi tutumie muda wa maongezi. Nadhani lile lilikuwa suluhisho lisilo na mkanganyiko.
 
Zile tozo nyingine za miamala ya simu mbona hatuambiwi zinakusanywa ngapi na kupelekwa wapi?
Ni ingredient ya ASALI, asilani abadani, hutoambiwa.

Watakudanganya na makusanyo ya TRA kwa quarter quarter, kila mwezi hawatakuambia pia!

Watumishi wa karibu kabisa wa mawaziri, wakipiga stori, nilishangaa wakisema jinsi wanavyofanya kazi ya kubeba mabegi ya maburungutu
 
Ni sawa, mimi ningeshauri wapandishe bando hadi ifike MB 10 kwa shilingi elfu tano
 
Mwanzoni nilikuwa simuelewi ila nikichanganya dot, nimepata jibu.

Kama mtoto wa kiume Nape alibebwa BEBWA hadi kufika hapo, je vipi huyu wa KE?
 
Ama tuandaa kisaikolojia kutoka buku mb 490 itakua mb 300
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…