TPL: Simba SC vs Alliance FC - October, 24.

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
Baada ya mapumziko ya siku 2, hatimae TPL inaendelea leo (24/10/2018) tena. Bingwa Mtetezi, Simba SC anawakaribisha 'Watoto wa Sekondari' Alliance FC katika dimba la Taifa Stadium. Mechi hii inatarajiwa kuanza mnamo saa 1 (moja) kamili usiku.
Katika mechi zao za mwisho Simba SC alitakata vilivyo kwa kuwagagadua ipasavyo Stand United 3-0, huku Alliance FC ikifungwa na Yanga SC. Katika mechi ya leo, Alliance FC watajaribu kutafuta pointi, huku Simba SC akitarajiwa kuendeleza wimbi lake la ushindi.

Simba SC 5-1 Alliance FC
 
Kwa upande wa Simba SC..
1. Captain Bocco anarejea baada ya kumaliza kutumikia adhabu yake ya kutocheza mechi 3.
2. James Kotei ataendelea kuitumikia adhabu ya kukosa mechi 3.
3. Jonas Mkude nae anarejea leo dimbani, baada ya kuumia wakati akilitumikia Taifa lake.
 
Kwa Upande wa Alliance FC..
Baada ya mechi ya Yanga SC walienda kuweka kambi mkoani pwani.. Na leo wanatokea Pwani.
 
Mpaka sasa..

Simba SC kafunga goli 11 huku Alliance FC wakifunga goli 3.
Simba SC kafungwa goli 3 tuu huku Alliance FC akifungwa 12.
 
Inasemekana hii Alliance wanacheza mpira mzuri na kuumiliki kwa muda mrefu licha ya ubutu wa safu ya ushambuliaji kuwaangusha. Kama ndivyo watakaokuwa uwanjani watafaidi sana mpira halisi
 
Kwanini Yanga ana viporo vingi hivyo kuna nini kinachofanya asivimalize viporo vyote hivyo ?
Tatizo la Yanga ni kama house girl anashinda ndani tu, anaogopa kabisa katoka nje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…