TRA: Hatukumtuma Sabaya kukusanya kodi

TRA: Hatukumtuma Sabaya kukusanya kodi

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
KAIMU Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Arusha, Kayobio Majogoro(41), ameieleza mahakama kwamba ofisi yake haikuwa na taarifa kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya, kuongoza kikosi kazi maalumu kwenda kukusanya kodi katika Jiji la Arusha.

Akiongozwa kutoa ushahidi wake na wakili wa Serikali mwandamizi, Ofmed Mtenga mbele ya hakimu mkazi, Patrisia Kisinda shahidi huyo amedai kuwa kwa mujibu wa sheria mwenye mamlaka ya kuunda kikosi kazi maalum ni kamishna mkuu wa TRA. Ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kuwa mkuu wa wilaya hawezi kuwa na jukumu la kukusanya kodi.

Katika shauri hilo la uhujumu namba 27,2021, washtakiwa wengine ni Enock Mnkeni, Watson Mwahomange, John Aweyo, Sylvester Nyegu, Jackson Macha na Nathan Msuya.

Sabaya.jpg

Chanzo: Nipashe
 
TRA haikuwa mamlaka ya uteuzi ya Lengai Ole Sabaya.

Mamlaka ya juu ilikuwa inajua na ilibariki operesheni hiyo.

Waziri wa fedha wa wakati huo alikuwa anajua na kubariki zoezi zima.

Gavana wa benki kuu alikuwa anafahamu na alitambua kazi nzuri kwa kumpongeza hadharani (In a televised record).

Kama hakutumwa na makusanyo alifanya na kukabidhi ama mamlaka iliyomtuma au hazina kwanini walizipokea?

Mashahidi wanatakiwa kuongezeka (waziri wa fedha na mipango wa wakati huo) ( gavana wa benki kuu), (katibu mkuu hazina na mlipaji mkuu wa serikali), kiongozi wa wilaya au mkoa husika zoezi lilikofanyikia walikuwa na taarifa na hawakuzuia.

Hata mamlaka iliyopo sasa ilikuwa na taarifa lakini hakuna hata mmoja aliyetoa notisi ya kujiuzulu kwa kutoridhika na operesheni iliyokuwa inafanyika.

Huyo kijana Lengai Ole Sabaya aachiwe samba na Freeman Aikaeli Mbowe WAACHIWE wote maana kesi zao zimegubikwa na chuki za kisiasa
 
shahidi huyo amedai kuwa kwa mujibu wa sheria mwenye mamlaka ya kuunda kikosi kazi maalum ni kamishna mkuu wa TRA. Ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kuwa mkuu wa wilaya hawezi kuwa na jukumu la kukusanya kodi.

=====
Huyo Shahidi amejiridhisha kuwa KamishnA wa wakati huo hakuunda kikosi kazi kilichojumuisha 'walalamikiwa'?

Kisheria na kitaratibu, kwa cheo chake ni lazima aelezwe timu ya kikosi kazi kilichoundwa na Kamishna?

Kwa nini kauli ya shahidi itiliwe maanani wakati...!
 
Back
Top Bottom