TRA hawatoi majina ya walioajiriwa badala yake wanapigiwa simu, hii inaonesha wazi kuna kuajiriwa kwa kujuana

GOSSO MZEKEZEKE

Senior Member
Joined
Dec 13, 2013
Posts
180
Reaction score
204
Habari,

Kuna tetesi ya walioajiriwa TRA kuwa wanapigiwa simu kwenda kuchukua ajira. Swali langu ni kwanini wakati wameita interview walitangaza? na wanapoajiriwa wasitangaze?

Hii inaonesha wazi kuna ukiritimba unafanyika, wanapeana ajira kwa kujuana na watoto wa vigogo.

Suala la mtoto wa maskini kuajiria TRA itakuwa ni ndoto za mchana kweupe, Natamani Raisi Samia angelijua hili arudishe mamlaka kwa tume yua ajira ya serikali.
 
Kama mtu katumiwa offer letter na kupiga simu, unataka Tena jina lake liwekwe Google Hadi wachawi wa kijijini walione?

Kuna wachawi huwa Wana kazi ya ku download PDF na utumishi, then wanatafuta majina ya classmates wajue wamepangiwa wapi, kisha wanatangulia kuchafua anga la kule
 
ww n mjinga ingawaje mm sijaomba kazi tra wala hazinihusu lkn kama taasisi kubwa kama tra inaajiri kwa mtindo huo bas system ya serikali ya kufatilia mambo ya ajira za watanzania ni dhaifu na inawalakini
 
Wachawi wenyew wanauwezo wa kufatilia taarifa zako bila ilo PDF,so pdf has nothing to do na ao wachaw wanawez kukuharibia tu.
 
Si mlikubaliana taasisi ziajiri zenyewe wazee!?

........Huu ni mwanzo.
 
Bro! Kwa uhaba wa ajira uliopo bongo, bado unajiuliza hayo maswali! Fulsa ni chache,lazima watu washikane mashati!
 
Bado hamjasema ,mtasema tu. Huu ni mwanzo ikifika katikati hata mabubu wataongea, viziwi watasikia na vipofu wataona.
 
interview hapo bado huja ajiriwa umeitwa ili ukafanyiwe usahili sasa kama umekosa jina lako liwekwe la nini kwenye matangazo? ushasema aliyeshinda anaitwa na siyo tra tu sehemu kubwa hata private utasikia tukikuhitaji tutakutafuta. Ndiyo maana CV unatakiwa uweke anuani yako au namba ya simu unadhani waliofanya hivo ni wajinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…