TRA ifanye marekebisho matumizi ya mashine za EFD ili watu walipe kodi kwa furaha

TRA ifanye marekebisho matumizi ya mashine za EFD ili watu walipe kodi kwa furaha

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Matatizo ya mashine za EFD yapo ya aina nyingi tangu umiliki wake mpaka katika matumizi.
Ukichunguza sana utagundua hizi mashine kama hazifanyi kazi ya kukushanya kodi peke yake bali na kumnyonya mfanyabishara. Hali hiyo ndiyo inayopelekea kufukuzana baina ya watumishi wa TRA na walipa kodi

1. Nikianza kwenye ulazima wa kumiliki hizi mashine hakuna mchanganuo wa uhakika juu ya nani anastahiki kuanza kutumia na nani sio lazima. Kuna wafanyabiashara hulazimishwa kununua mashine hizo wanapoanza tu biashara japo mitaji yao ni midogo sana na hata hajapata wateja katika biashara yake.

2.Umiliki huo hauzingatii aina ya biashara anayofanya mfanyabiashara.Kuna biashara kwa kweli haziendani na matumizi ya mashine hizo ambazo ni rahisi kuharibika.Mfano biashara sehemu za maji maji na vumbi.

3.Kanuni na kampeni kwa mlipa kodi ni kuwa ukiuza toa risiti na ukinunua dai risiti.Maana yake ni kuwa hata ukiuza kitu cha shilingi 100 mteja ana haki ya kudai risiti na una wajibu wa kumtolea risiti
Iwapo unauza shilingi 10000 kwa siku na biashara yako ni hiyo ya 100 mia basi kwa siku unaweza ukafikia kiwango cha risiti 1999 ambacho ndicho kiwango kinachofanya mashine ijae na kulazimika kununua nyengine.

4.Mashine ikiharibika unatakiwa utoe taarifa na kuitengeneza haraka.Kinyume chake ufunge biashara.
Sasa mashine zenyewe nyingi ni mbovu sana.Hazihimili vishindo na matengenezo ni ghali si chini ya 59,000/.Kwanini zisiagizwe mashine za matumizi yasiyokuwa na mazonge na ufundi ikawa ni kitu huru ukiondoa mifumo ya kielektronic ambayo itabaki kwao TRA.

4.Kuna taarifa kwamba mashine ukinunua unarejeshewa pesa.Urejeshwaji wa pesa hizo ni kitu hewa na hautekelezwi au urasimu wake unachosha.
Na kama kweli upo utaratibu huo basi hiyo pesa inayorejeshwa kwa kujaa mashine halafu ikastahiki kutupwa ni pesa ya walipo kodi.Kwanini TRA wasiagize mashine ambazo zikijaa zinafutika na kuendelea kutumika badala ya kuzitupa.
 
Kinachoumiza unakadiriwa kodi kwenye mauzo na sio faida kama mashine yako inamauzo ya million 50 kwa mwaka hiyo ndo itatumika kukadiriwa kodi
Kodi namna hiyo kwanza ni haramu kidini ndio maana uchumi mzima hauna afya.
Upande mwengine hawa wataalamu wa kodi sijui wamesomea sayari gani.Kwa sababu ni kweli wanaangalia mauzo wakati kuna biashara hata ukiuza sh.laki moja kwa siku faida yako haifiki hata 5000. lakini kiTRA unatakiwa ulipe 18000.
 
Kodi namna hiyo kwanza ni haramu kidini ndio maana uchumi mzima hauna afya.
Upande mwengine hawa wataalamu wa kodi sijui wamesomea sayari gani.Kwa sababu ni kweli wanaangalia mauzo wakati kuna biashara hata ukiuza sh.laki moja kwa siku faida yako haifiki hata 5000. lakini kiTRA unatakiwa ulipe 18000.
Upo sahihi nimekoma mimi kuandika risiti ovyo mwaka jana yalinikuta faida ya soda takeaway jumla ni sh 400 ukiandika risiti katoni kumi faida 4000, ukiuza soda elf 1 kwa mwezi faida ni laki 4 na ukitoa gharama zingine ushushaji kudelivery kwa wateja faida inapungua
Mfano kwa mwezi ukauza katon elf 1 au 900 na ukatoa risit halali zenye thaman ya million kumi ukazidisha kwa mwaka miezi 12 utapata mauzo ya million 120, kodi utakayokutana nayo TRA utajuta unaweza ambiwa hata ulipe million 3 kwa mwaka, wakati faida uliyobakiwa nayo baada ya uendeshaji wa biashara ni million 3 na laki 6 ukilipa TRA unajikuta kwa mwaka umeingiza laki 6
 
Upo sahihi nimekoma mimi kuandika risiti ovyo mwaka jana yalinikuta faida ya soda takeaway jumla ni sh 400 ukiandika risiti katoni kumi faida 4000, ukiuza soda elf 1 kwa mwezi faida ni laki 4 na ukitoa gharama zingine ushushaji kudelivery kwa wateja faida inapungua
Mfano kwa mwezi ukauza katon elf 1 au 900 na ukatoa risit halali zenye thaman ya million kumi ukazidisha kwa mwaka miezi 12 utapata mauzo ya million 120, kodi utakayokutana nayo TRA utajuta unaweza ambiwa hata ulipe million 3 kwa mwaka, wakati faida uliyobakiwa nayo baada ya uendeshaji wa biashara ni million 3 na laki 6 ukilipa TRA unajikuta kwa mwaka umeingiza laki 6
Bila mtu kuwa mfanyabiashara kweli hawezi kujitetea namna hiyo.
Wateja na wananchi kwa ujumla hawaelewi kuwa huu mfumo wa kodi kwa mashine za EFD una kasoro kubwa
Hofu peke yake ya kumiliki hiyo mashine inakufanya usiwe na uhuru wa kuuza.Kila anayeingia eneo lako unahisi amekuja kukutega akuwachie bomu la madai.
 
Upo sahihi nimekoma mimi kuandika risiti ovyo mwaka jana yalinikuta faida ya soda takeaway jumla ni sh 400 ukiandika risiti katoni kumi faida 4000, ukiuza soda elf 1 kwa mwezi faida ni laki 4 na ukitoa gharama zingine ushushaji kudelivery kwa wateja faida inapungua
Mfano kwa mwezi ukauza katon elf 1 au 900 na ukatoa risit halali zenye thaman ya million kumi ukazidisha kwa mwaka miezi 12 utapata mauzo ya million 120, kodi utakayokutana nayo TRA utajuta unaweza ambiwa hata ulipe million 3 kwa mwaka, wakati faida uliyobakiwa nayo baada ya uendeshaji wa biashara ni million 3 na laki 6 ukilipa TRA unajikuta kwa mwaka umeingiza laki 6
Duuh
 
Bila mtu kuwa mfanyabiashara kweli hawezi kujitetea namna hiyo.
Wateja na wananchi kwa ujumla hawaelewi kuwa huu mfumo wa kodi kwa mashine za EFD una kasoro kubwa
Hofu peke yake ya kumiliki hiyo mashine inakufanya usiwe na uhuru wa kuuza.Kila anayeingia eneo lako unahisi amekuja kukutega akuwachie bomu la madai.
Nilivoenda TRA kukadiliwa mwezi wa pili mwaka huu nikamuelekeza mfanyakazi wa TRA kwamba huu mfumo wa kuangalia mauzo kwenye EFD unatunyonya, nae alikiri kabisa kama mfumo si rafiki lakini hawana namna wanasimamia sheria kutoka juu
 
Nilivoenda TRA kukadiliwa mwezi wa pili mwaka huu nikamuelekeza mfanyakazi wa TRA kwamba huu mfumo wa kuangalia mauzo kwenye EFD unatunyonya, nae alikiri kabisa kama mfumo si rafiki lakini hawana namna wanasimamia sheria kutoka juu
Mabadiliko yanahitajika haraka.
 
Poleni sana walipa kodi
Aya maendeleo madogo tuliyonayo ni kwa ajili ya kodi zenu wakuu
Maana bila kodi zenu hali ingekuwa mbaya zaidi
Maendeleo hayakai sawa kwa sababu walipa kodi hizo hawatoi kwa kuridhika.Ndio maana unaona hazina baraka katika uchumi.Pesa zinavuja kama maji kwenye pakacha.
 
Matatizo ya mashine za EFD yapo ya aina nyingi tangu umiliki wake mpaka katika matumizi.
Ukichunguza sana utagundua hizi mashine kama hazifanyi kazi ya kukushanya kodi peke yake bali na kumnyonya mfanyabishara. Hali hiyo ndiyo inayopelekea kufukuzana baina ya watumishi wa TRA na walipa kodi

1. Nikianza kwenye ulazima wa kumiliki hizi mashine hakuna mchanganuo wa uhakika juu ya nani anastahiki kuanza kutumia na nani sio lazima. Kuna wafanyabiashara hulazimishwa kununua mashine hizo wanapoanza tu biashara japo mitaji yao ni midogo sana na hata hajapata wateja katika biashara yake.

2.Umiliki huo hauzingatii aina ya biashara anayofanya mfanyabiashara.Kuna biashara kwa kweli haziendani na matumizi ya mashine hizo ambazo ni rahisi kuharibika.Mfano biashara sehemu za maji maji na vumbi.

3.Kanuni na kampeni kwa mlipa kodi ni kuwa ukiuza toa risiti na ukinunua dai risiti.Maana yake ni kuwa hata ukiuza kitu cha shilingi 100 mteja ana haki ya kudai risiti na una wajibu wa kumtolea risiti
Iwapo unauza shilingi 10000 kwa siku na biashara yako ni hiyo ya 100 mia basi kwa siku unaweza ukafikia kiwango cha risiti 1999 ambacho ndicho kiwango kinachofanya mashine ijae na kulazimika kununua nyengine.

4.Mashine ikiharibika unatakiwa utoe taarifa na kuitengeneza haraka.Kinyume chake ufunge biashara.
Sasa mashine zenyewe nyingi ni mbovu sana.Hazihimili vishindo na matengenezo ni ghali si chini ya 59,000/.Kwanini zisiagizwe mashine za matumizi yasiyokuwa na mazonge na ufundi ikawa ni kitu huru ukiondoa mifumo ya kielektronic ambayo itabaki kwao TRA.

4.Kuna taarifa kwamba mashine ukinunua unarejeshewa pesa.Urejeshwaji wa pesa hizo ni kitu hewa na hautekelezwi au urasimu wake unachosha.
Na kama kweli upo utaratibu huo basi hiyo pesa inayorejeshwa kwa kujaa mashine halafu ikastahiki kutupwa ni pesa ya walipo kodi.Kwanini TRA wasiagize mashine ambazo zikijaa zinafutika na kuendelea kutumika badala ya kuzitupa.
Mkuu,Lipa kodi kwa maendeleo ya TAIFA.Kwanza kabisa kutoa risiti hakumaanishi kwamba utalipa kodi kubwa.Pili Mshine zipo za aina nyingi zikiwamo za kutumia kwenye SIMU au Kompyuta yako aka VFD.

Swali la kujiuliza ni JE shida na mashine ya EFD au ni mfumo wetu wa kodi na desturi yetu ya kodi?Kwa mtazamo wangu shida ni DESTURI na MFUMO wa kodi.Kwa ufupi KODI ni nyingi na kubwa sana ila mwamko wa ulipaji nao upo chini sana.Watanzania wengi hatupendi/hatutaki kulipa kodi na hata wale wachache ambao wanataka/kulazimika kulipa kodi huwa wanajikuta wanaelemewa na msururu mkubwa wa kodi na TOZO.Leo nimefika TRA nataka kuanzisha Kampuni afisa wa kodi ananiambia Mkataba wangu wa Pango kwa TRA W/H Tax kodi inapangwa na TRA na sio na mkataba wangu wa ofisi.Nikacheka kisha niksema hii ndio Tanzania ya Viwonder.
 
Mkuu,Lipa kodi kwa maendeleo ya TAIFA.Kwanza kabisa kutoa risiti hakumaanishi kwamba utalipa kodi kubwa.Pili Mshine zipo za aina nyingi zikiwamo za kutumia kwenye SIMU au Kompyuta yako aka VFD.

Swali la kujiuliza ni JE shida na mashine ya EFD au ni mfumo wetu wa kodi na desturi yetu ya kodi?Kwa mtazamo wangu shida ni DESTURI na MFUMO wa kodi.Kwa ufupi KODI ni nyingi na kubwa sana ila mwamko wa ulipaji nao upo chini sana.Watanzania wengi hatupendi/hatutaki kulipa kodi na hata wale wachache ambao wanataka/kulazimika kulipa kodi huwa wanajikuta wanaelemewa na msururu mkubwa wa kodi na TOZO.Leo nimefika TRA nataka kuanzisha Kampuni afisa wa kodi ananiambia Mkataba wangu wa Pango kwa TRA W/H Tax kodi inapangwa na TRA na sio na mkataba wangu wa ofisi.Nikacheka kisha niksema hii ndio Tanzania ya Viwonder.
Mimi kwangu kutoa risiti kumefanya nikadiriwe kodi kubwa lait kama mauzo yangu kwenye mashine yangekuwa chini na kodi ingekuwa chini vilevile
 
Mimi kwangu kutoa risiti kumefanya nikadiriwe kodi kubwa lait kama mauzo yangu kwenye mashine yangekuwa chini na kodi ingekuwa chini vilevile
Nilibishana nao sana kuhusu kodi hadi walinipa muongozo, kwamba mauzo yangu ya mwaka nizidishe kwa 3.5%
20240322_151604.jpg
 
Back
Top Bottom