DOKEZO TRA Kipata nani anamkingia kifua Thom Lardha/Phares Lardha kupandisha kodi kubwa ghalfa ndani ya muda mfupi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
HII NI DUNIA NA DUNIA NI DUARA AJIANDAE KWA LOLOTE LILE LITAKALOMFIKA NEVER PLAY WITH SUCH A MEN,KATIKA MAMBO AMBAYO SITHUBUTU KUYAFANYA NI MAMBO YA AINA HIYO, KWANI HUFUPISHA UMRI WA MTU, BURE BURE! JAMII HII HUFUGA GOLIM NDANI ACHA KABISA!
 
Wamiliki wa majengo ya biashara wana tabia hiyo.
Kodi inayoandikwa kwenye mkataba siyo inayolipwa .
Huu ni ukwepaji mkubwa sana wa kadi unaofanywa na hao wamiliki
Hawa si ndiyo wafadhili wa CCM? Unadhani watafanywa chochote? Kuna yule mwamba ambaye wanadai alijiua kwa risasi, aliripoti ukwepaji wa kodi mkubwa, lakini alizungushwa na kughasiwa mpaka waliposema amejipiga risasi. Bila kuindoa CCM kila mtu atakumbana na janga kwa wakati wake. Dunia imeendelea sana kama tungekuwa na serikali makini ukwepaji kodi kama huu ungekomeshwa kwa kutumia electronics.
 
Kama ni mwana ccm hilo litaisha kama yale madudu ya Kariakoo
 
TRA Tanzania mnalala sana
 
Nashauri usome vizuri mkataba wako,usikute umeandikwa kodi na mengineyo analipa mpangaji. Pia kwa kutaja kiwango halisi unacholipa kama kodi,kibao kinaweza kubadirika kwako kuwa makadirio ya kodi kwako kwa miaka iliyopita hayakuwa sawa na kutakiwa kulipa zaidi
 
Unajitafutia matatizo tu kushindani na WAKWASI

Kama ni hasira tu ungetafuta namna ya kuzimaliza

Kama ni kisasa ungetafuta namna.

Otherwise don't hunt what u can't kill.
 
Mimi nilidhani withholding tax inawasilishwa TRA na mpangaji kwa maana anazuia 10% ya kodi anayolipa. Mwenye jengo analipwa 90%.
 
Serikali ingekuwa na utaratibu wa kuwalipa masnitch/wazalendo kama wewe wanaofichua wakwepa kodi na wala rushwa na mkaiwezesha ikakusanya chake, tungekuwa mbali sana.
 
Huu ndio uzalendo, wewe ni mzalendo wa kweli wa nchi hii.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…