TRA wanatumia sana ule usemi kuwa "kutijua sheria sio utetezi". Sheria iko wazi kuwa chombo kikiharibika kiasi cha kutoweza kutembea barabarani basi taarifa zake zipelekwe TRA ili malipo ya tozo la barabara (road lisence) yasimamishwe. Pia sheria hiyo inamtaka mmiliki wa chombo cha barabarani akiona chombo chake hakiwezi kutengenezeka atoe taarifa TRA aombe kufuta usajili wa chombo hicho.
Kutofanya hivyo kutasababisha chombo hicho kuelendela kutozwa tozo hiyo kila mwaka.
Kwa utaratibu wa sasa, ikiwa unadaiwa tozo ya barabara ya chombo chako na ukaenda TRA kwa shughuli nyingine kama kutaka kibali cha kufanya buashara au kulipa leseni ya udereva, wanakunasa hapohapo.
Ni ushauri wangu kwa TRA kuweka angalizo kwenye kadi za magari ili kuwakumbusha wamiliki wajibu huu.