View attachment 3232930
Malaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu zangu mmetoa matangazo ya kazi na kuwataka Watanzania waombe lakini sijui ni kwa makusudi au bahati mbaya mtandao wenu ni shida kiasi kwamba inakuwa ni vigumu hata kujisajili.
View attachment 3232920
Hali hiyo imesababisha hata wanaohitaji huduma nyingine za kimtandao nao kuathirika, siamini kama server yenu imezidiwa siku zote hizo, au kuna watu wameamua kufanya yao ili maombi yapungue kwa sababu wanazozijua wao.
View attachment 3232921
Mmetoa nafasi zaidi ya 1,000, mnatakiwa kutambua mmeshikilia hisia za watu wengi muda huu, rekebisheni network yenu, TRA ni taasisi kubwa hamstahili kulalamikiwa kwa hili wiki nzima sasa.
View attachment 3232927