TRA na TANESCO wanajua kwamba Nyumba ni chache kuliko idadi ya mita za Luku?

TRA na TANESCO wanajua kwamba Nyumba ni chache kuliko idadi ya mita za Luku?

Plsm

Senior Member
Joined
Aug 19, 2021
Posts
177
Reaction score
266
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesco, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku

Kwanza ninahakika, hili limekuja baada ya serikali kukosa namna ya kuwabana wamiliki wa majengo ili kuyalipia

Na pia ninahakika, Sheria waliyokuwa wameitunga kwa ajili wamiliki wa majengo kulipia majengo yao, inaipa ugumu serikali kuwabana wamiliki hao kwa sababu wengi wa wamiliki wa majengo makubwa na yanayotakiwa kulipiwa kodi kubwa, ni haohao walioko serikalini

Ninayohakika pia kwamba, hata ukifuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya majengo, utawakuta ni viongozi wa serikali wenye majengo mengi na makubwa yanayolipiwa kodi kubwa

Sasa basi, Serikali inapokuja na mfumo huu mpya wa kila luku itumike kulipia kodi ya jengo, ninahakika kuwa, huu ni mpango wa kinyonyaji na wizi wa wawazi kwa wasio wamiliki wa majengo hayo yaani kodi hii maana yake imeelekezwa kwa walala hoi tena bila huruma

Kwa sababu hiyo, Serikali kupitia TRA na Tanesco, Je wanajua kuwa jengo moja linaweza kuwa na mita no zaidi ya 10?

Je, katika kulipia Jengo moja lenye mita zaidi ya 1, Serikali inaweka mfumo gani kwa nyumba zenye mita zaidi ya moja? au kila mita inahesabika na Jengo lake?

Kama itakuwa kila mita inahesabika iko kwenye jengo linalojitegemea! basi huu utakuwa ni wizi wa Serikali kwa wananchi wake!
 
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesiko, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku
Mbona hilo wamelitolea ufafanuzi kuwa kama nyumba ina zaidi ya mita moja ya umeme, mwenye nyumba anatakiwa achague mita moja , aende tanesco akatoe taarifa kuwa hiyo ndio itakayokuwa inakatwa kodi ya majengo.
 
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesiko, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku

Kwanza ninahakika, hili limekuja baada ya serikali kukosa namna ya kuwabana wamiliki wa majengo ili kuyalipia

Na pia ninahakika, Sheria waliyokuwa wameitunga kwa ajili wamiliki wa majengo kulipia majengo yao, inaipa ugumu serikali kuwabana wamiliki hao kwa sababu wengi wa wamiliki wa majengo makubwa na yanayotakiwa kulipiwa kodi kubwa, ni haohao walioko serikalini
Si uondoe hizo mita ubakiwe na moja kama nyumba ni moja
 
Hivi hii kodi ya majengo ni mpya au ilikuwepo? Mimi naona kilichobadilika ni namna ya ulipaji na kutoka 10,000 mpaka 12,000 kwa mwaka. Tujiulize kwenda kupanga foleni TRA ili ulipe 10,000/- na kulipa 12,000/- kupitia manunuzi ya Luku kipi kina rahisisha maisha? Wabongo tunapenda sana kulalamika.
 
Tulipe Kodi kwa maendeleo ya nchi
Wabongo walalamishi sana ndio maana viongozi huwa wanapuuza malalamiko yoyote, 12,000 kwa mwaka mtu mwenye nyumba anaona hio ni kodi kubwa?!!! Mimi nitailipa na mpangaji wangu nitamlipia yote.
 
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesiko, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku

Kwanza ninahakika, hili limekuja baada ya serikali kukosa namna ya kuwabana wamiliki wa majengo ili kuyalipia
Maendeleo hayana chama!!
 
Huu ni zaidi ya ujinga bahati nzuri kwa viongozi wenye nchi bado wamelala usingizi mzito shame on you
 
Hivi hii kodi ya majengo ni mpya au ilikuwepo? Mimi naona kilichobadilika ni namna ya ulipaji na kutoka 10,000 mpaka 12,000 kwa mwaka. Tujiulize kwenda kupanga foleni TRA ili ulipe 10,000/- na kulipa 12,000/- kupitia manunuzi ya Luku kipi kina rahisisha maisha? Wabongo tunapenda sana kulalamika.
kwakweli watu wanapenda Sana kulalamika
 
wabongo walalamishi sana ndio maana viongozi huwa wanapuuza malalamiko yoyote, 12,000 kwa mwaka mtu mwenye nyumba anaona hio ni kodi kubwa?!!! Mimi nitailipa na mpangaji wangu nitamlipia yote.
Mbongo anaona kapambana sana kujenga Nyumba peke yake,alafu tena umlipishe Kodi kutoka kwenye Nyumba yake,anaona Kama anatupa pesa!![emoji3][emoji2][emoji1]
 
Hivi hii kodi ya majengo ni mpya au ilikuwepo? Mimi naona kilichobadilika ni namna ya ulipaji na kutoka 10,000 mpaka 12,000 kwa mwaka. Tujiulize kwenda kupanga foleni TRA ili ulipe 10,000/- na kulipa 12,000/- kupitia manunuzi ya Luku kipi kina rahisisha maisha? Wabongo tunapenda sana kulalamika.
Jaribu kusoma na uelewe alicho andika.nahisi kama umekurupuka.
 
TRA wanapaswa kutoa ufafanuzi wa huu utaratibu mpya wa kulipia kodi ya majengo. Kwa wenye biashara, baadhi kodi ya majengo kwa mwaka huu 21/22 imeishalipwa wakati wa kufanyiwa uthamini wa biashara zao na kupata Tax clearance.

Tangazo la TRA linaonyesha kuwa utaratibu mpya wa malipo ya kodi ya majengo kupitia Luku, unaanza tarehe 20/08/2021. Je waliokwisha lipia kodi hii kwa mwaka mzima ina maana wakinunua umeme wanalipia kodi tena?.... Huu mbona ni wizi katika jina la Serikali?.
 
Hivi hii kodi ya majengo ni mpya au ilikuwepo? Mimi naona kilichobadilika ni namna ya ulipaji na kutoka 10,000 mpaka 12,000 kwa mwaka. Tujiulize kwenda kupanga foleni TRA ili ulipe 10,000/- na kulipa 12,000/- kupitia manunuzi ya Luku kipi kina rahisisha maisha? Wabongo tunapenda sana kulalamika.
Mkuu RRONDO!

uko sawa kabisa, shida ni kwamba, jengo moja lenye mita zaidi ya moja, ni mita zote zitaingiziwa kodi ama ni utaratibu upi utafanyika ili hizo luku zihesabike zinalipia kodi jengo moja?
 
Hili linahitaji kuboreshwa tu kwa kuhakiki wamiliki wa nyumba na kuwe na mfumo unao tally majina ya wamiliki wa nyumba na majina yaliyo kwenye LUKU. Huu utaratibu ni mzuri na wakupongezwa sana.
 
Back
Top Bottom