TRA na TANESCO wanajua kwamba Nyumba ni chache kuliko idadi ya mita za Luku?

TRA na TANESCO wanajua kwamba Nyumba ni chache kuliko idadi ya mita za Luku?

Mkuu RRONDO!

uko sawa kabisa, shida ni kwamba, jengo moja lenye mita zaidi ya moja, ni mita zote zitaingiziwa kodi ama ni utaratibu upi utafanyika ili hizo luku zihesabike zinalipia kodi jengo moja?
Kwa mujibu wa TRA muhusika anatajiwa aende kuainisha.
 
Chief sinumesikia asubh taalifa inasema mita hata kama 10 itayolipa ni moja tu.kikubwa wewe na mweny nyumba mkubalia ne mtakatana vip mfano kod 150.afanye 148 kufidia hilo la 12 lilipongua apo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani hujui serekale inakaaga vikao kabisa kupanga wizi wa kuwaibia wananchi?
 
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesiko, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku

Kwanza ninahakika, hili limekuja baada ya serikali kukosa namna ya kuwabana wamiliki wa majengo ili kuyalipia

Na pia ninahakika, Sheria waliyokuwa wameitunga kwa ajili wamiliki wa majengo kulipia majengo yao, inaipa ugumu serikali kuwabana wamiliki hao
Hili limeishatolewa ufafanuzi kama nyumba moja,kila chumba kina MITA yake,hapo mwenye nyumba inabidi atoe taarifa ni MITA ipi inalipia Kodi ya jengo,kama kiwanja kimoja kina nyumba zaidi ya moja,na kila nyumba ina MITA,MITA zote lazima zilipe Kodi ya jengo,hata kabla ya huu utaratibu kuja,ilikuwa hivyo,unalipa Kodi ya jengo kwa kila jengo lililopo kwenye kiwanja.

Nyumba ya kawaida Kodi yake ni 12000 kwa mwaka,unakatwa 1000 kila mwezi,ukikaa miezi miwili au zaidi bila kununua LuKu,siku ukinunua,unakatwa malipo yote ya miezi ambayo ukufanya manunuzi ya LuKu,hakuna wizi wapo,
 
Hili limeishatolewa ufafanuzi kama nyumba moja,kila chumba kina MITA yake,hapo mwenye nyumba inabidi atoe taarifa ni MITA ipi inalipia Kodi ya jengo,kama kiwanja kimoja kina nyumba zaidi ya moja,na kila nyumba ina MITA,MITA zote lazima zilipe Kodi ya jengo,hata kabla ya huu utaratibu kuja,ilikuwa hivyo,unalipa Kodi ya jengo kwa kila jengo lililopo kwenye kiwanja.
Nyumba ya kawaida Kodi yake ni 12000 kwa mwaka,unakatwa 1000 kila mwezi,ukikaa miezi miwili au zaidi bila kununua LuKu,siku ukinunua,unakatwa malipo yote ya miezi ambayo ukufanya manunuzi ya LuKu,hakuna wizi wapo,
Umeeleza vema sana mkuu
 
Mbona hilo wamelitolea ufafanuzi kuwa kama nyumba ina zaidi ya mita moja ya umeme, mwenye nyumba anatakiwa achague mita moja , aende tanesco akatoe taarifa kuwa hiyo ndio itakayokuwa inakatwa kodi ya majengo.
Hiyo ndio tundu la kutokea. Mita nyingi sanq zitaondolewa kwenye mfumo kimagendo kwa kisingizio hicho. Na zinazotakiwa ziondolewe ndo hazitakndolewa.

Wengi wataona mda wa kufuatilia elfu moja haupo hivyo wataacha tu ichukuliwe
 
Wabongo walalamishi sana ndio maana viongozi huwa wanapuuza malalamiko yoyote, 12,000 kwa mwaka mtu mwenye nyumba anaona hio ni kodi kubwa?!!! Mimi nitailipa na mpangaji wangu nitamlipia yote.
Magufuli aliwaharibu akawaita wanyonge, sasa hawataki kuchangia walitegemea. Waporwe wale wale waliokuwa wakiporwa na wao washangilie
 
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kushirikiana na shirika la umeme nchini Tanesiko, kesho tarehe 20 wataanza kulipisha kodi za nyumba kwa mfumo wa luku

Kwanza ninahakika, hili limekuja baada ya serikali kukosa namna ya kuwabana wamiliki wa majengo ili kuyalipia

Mkuu nadhani tuipongeze Serikali kwa kuwa wabunifu kwavile itaongeza wigo wa ukusanyaji wa kodi za majengo. Nakubaliana na wewe kuwa kuna mambo ya kuweka sawa hasa juu ya nani na nani asikatwe kodi ya Jengo. Hii option ya mtu kusema Luku/Metre hizi zisikatwe kodi ya Jengo ni hatari kwani inaweza kutumiwa vibaya na "Vigogo" wasio Wazalendo
 
Magufuli aliwaharibu akawaita wanyonge, sasa hawataki kuchangia walitegemea. Waporwe wale wale waliokuwa wakiporwa na wao washangilie
Kwahiyo unataka kutuambia kwamba kibao kimetugeukia au[emoji23][emoji23]
 
Magufuli aliwaharibu akawaita wanyonge, sasa hawataki kuchangia walitegemea. Waporwe wale wale waliokuwa wakiporwa na wao washangilie
Aisee!

Kwa hiyo najengo yalipiwe na wapangaji wenye nyumba waendelee kula maisha siyo
 
Nchi hii haijitambui. Inaanzisha mambo ambayo haina uwezo nayo
 
Wabongo walalamishi sana ndio maana viongozi huwa wanapuuza malalamiko yoyote, 12,000 kwa mwaka mtu mwenye nyumba anaona hio ni kodi kubwa?!!! Mimi nitailipa na mpangaji wangu nitamlipia yote.
Ndugu yangu inawezekana wewe una hali nzuri kimaisha,ndio maana unaweza hata kumlipia mpangaji wako.Hongera kwa hilo.
 
Ndugu yangu inawezekana wewe una hali nzuri kimaisha,ndio maana unaweza hata kumlipia mpangaji wako.Hongera kwa hilo.
Ni ajabu mtu aweze kujenga nyumba,alipie umeme lakini ashindwe kulipa 1,000/- kwa mwezi. Nashukuru Mungu sishindwi kulipa 1,000/- kwa mwezi. Na siwezi kumkosea Mungu shukrani niwe mnafiki kuwafurahisha watu kama nyinyi niseme kuwa 1,000/- ni nyingi kwa mtu mwenye nyumba.
 
Ni ajabu mtu aweze kujenga nyumba,alipie umeme lakini ashindwe kulipa 1,000/- kwa mwezi. Nashukuru Mungu sishindwi kulipa 1,000/- kwa mwezi. Na siwezi kumkosea Mungu shukrani niwe mnafiki kuwafurahisha watu kama nyinyi niseme kuwa 1,000/- ni nyingi kwa mtu mwenye nyumba.
Nafikiri ulikusudia kusema 1,000 sio kubwa kwa mtu mwenye nyumba.
Ni sahihi
 
Aisee!

Kwa hiyo najengo yalipiwe na wapangaji wenye nyumba waendelee kula maisha siyo
Mtafanya reconciliation wakati wa kulipana pango. Kwanza sheria inataka umkate 10% withholding tax kwenye pango.
 
Mtafanya reconciliation wakati wa kulipana pango. Kwanza sheria inataka umkate 10% withholding tax kwenye pango.
Hahahaa!
Mwenye nyumba akigoma utafanya nini sasa! na ukipnekana kutaka kumpeleka mahakani, anakutimua kwenye nyumba yake, Je kunasheria inamlinda mpangaji?
 
Ni ajabu mtu aweze kujenga nyumba,alipie umeme lakini ashindwe kulipa 1,000/- kwa mwezi. Nashukuru Mungu sishindwi kulipa 1,000/- kwa mwezi. Na siwezi kumkosea Mungu shukrani niwe mnafiki kuwafurahisha watu kama nyinyi niseme kuwa 1,000/- ni nyingi kwa mtu mwenye nyumba.
Sawa, Hongera Sana.
 
Back
Top Bottom