TRA wananiambia niingie VAT

TRA wananiambia niingie VAT

TRA wanamatatizo sana,
Tatizo kubwa hawatoi elimu kabisa watu wanahangaika kutafuta elimu wenyewe.Na hili wanalifanya kusudi ili wapate mwanya wa kuwatisha watu wawape rushwa.

Kikiubwa inapswa iwe wazi namna wanavyokokotoa 18% ya VAT,je wanapiga kwenye mauzo ama kwenye faida?

Kama VAT itakua inafanyiwa hesabu kwenye mauzo huu utakua ni wendawazimu,ila kama watakua wanafanya hesabu kwenye faida si mbaya.

Chukua mfano Mimi na Juma tuwe na biashara zinazo fanana kwa kila namna,Mimi niwe kwenye VAT na Juma awe kwenye kodi ya mapato,bidhaa ikiwa na thamani mf 10,000/=,nitalazimika kuweka 18% ya VAT ambayo ni 1800/=,nikiijumlisha kwenye bei nitalazimika niuze 11800,

Kwa mfano huo wa mimi na juma utaona kwamba Juma yeye kwakua hayupo kwenye VAT anauwezo wakuuza kwa 11,000 akapata faida ya 1000,je .Mimi nitapata wateja?

Hii ndio hofu ya mtoa mada na wafanyabiashara wengi.

Tatizo kubwa kwenye biashara, ni hizi mambo za kutengeneza makundi,kama ilivyosasa hawa wa VAT na hawa sio wa VAT.Hapa kuna leta unfair competition na hili ndio tatizo kubwa linaloua biashara za watu.

Kinachotakiwa watu wote wawekwe kwenye mfumo mmoja,mfano watu wote wawe kwenye VAT na wote wawe na EFD machine.Na hizi machine zitolewe bure TRA.

Unfair competition inaua sana biashara,naamini kama kila mfanya biashara akipewa EFD mashine inawezekana kabisa VAT ikashuka hata 5% na makusanyo yakawa maradufu kuliko ilivyosasa.
Wewe ni wakala wa kukusanya VAT,
VAT hulipwa na mlaji
 
Muongo

TIN husajiliwa kwa alama za vidole au NIDA
TIN lazima uende kukadiriwa ili upewe ya biashara
TIN ya Msimbazi huwezi itumia Tegeta

Punguza ubishi tin inasajiriwa kwa kitambulisho cha nida na kwenyw coment yangu nimeandika nimekusanya vitambulisho vya ndg ninavyo
Halaf sijawah hangaika kwenda kusajir ndg vishoka ndo kazi yao nawapa kitambulisho na chao wananiletea tin/makadirio na lessen
 
Kuna namna hesabu za ulipaji wa Return(ritani) za VAT hufanyika na ukalipa kiasi kidogo kabisa unachostahili kulipa naa bado ukabakia na faida kubwa ila wengi hawajui,kwa msaada zaidi unaweza nicheck mkuu.

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Tra wananiambia wanikadirie mil 3.4 na kila mwezi nalipa vat sasa naona ni makato juu ya tozo
Kuna namna hesabu za ulipaji wa Return(ritani) za VAT hufanyika na ukalipa kiasi kidogo kabisa unachostahili kulipa naa bado ukabakia na faida kubwa ila wengi hawajui,kwa msaada zaidi unaweza nicheck mkuu.

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Punguza ubishi tin inasajiriwa kwa kitambulisho cha nida na kwenyw coment yangu nimeandika nimekusanya vitambulisho vya ndg ninavyo
Halaf sijawah hangaika kwenda kusajir ndg vishoka ndo kazi yao nawapa kitambulisho na chao wananiletea tin/makadirio na lessen
Huwezi kupewa leseni kama huna tax clearance...na tax clearance unapewaje na hata hiyo robo ya makadilio na WHT hujalipa (endapo unapofanyia biashara umepanga).

Unalipa kodi husika, unapewa tax clearance unapeleka halimashauri unakoenda kupewa business licence.

Acha uongo boy
 
Obviously wewe ni wale wanaochukua mali kauli kwa matajiri wanaouzia store huku ukitoa receipts halali na bahati mbaya ukitengeneza faida ndogo.

Ukweli mchungu umewafaidisha wao hao magwiji wa biashara huku wewe ukijipiga pin,nenda zungumza nao hao TRA kisha ujifunze kufanya biashara kwa akili
Hii point nimesoma mara tatu,naona ina ujumbe sana ila bado sijaelewa vizuri naomba nieleweshe tena.

Kwamba mdau, anatumia laverage kisha anauza kwa receipts? Kama angenunua na akauza kwa receipts ingekuaje? Isingefika 100m?
 
Huwezi kupewa leseni kama huna tax clearance...na tax clearance unapewaje na hata hiyo robo ya makadilio na WHT hujalipa (endapo unapofanyia biashara umepanga).

Unalipa kodi husika, unapewa tax clearance unapeleka halimashauri unakoenda kupewa business licence.

Acha uongo boy

Njoo dm unipe kitambulisho chako then nipe 2days nitakupa tin/lessen/tax clearance za mkoa wa kikodi kinondon au endelea kubishana sababu unaamin kila kitu lazima ukipate kwa utaratibu
 
Hii point nimesoma mara tatu,naona ina ujumbe sana ila bado sijaelewa vizuri naomba nieleweshe tena.
Kwamba mdau, anatumia laverage kisha anauza kwa receipts? Kama angenunua na akauza kwa receipts ingekuaje? Isingefika 100m?
Huku mtaani wapo matajiri wanaoingiza mizigo wanawapa kwa mali kauli vendors,(kama mdau hapa) wao huwa hawana frame mzigo wanautoa store wanampa muhusika kwa makubaliano may be kila siku jioni au kila wiki watapitia pesa kiasi fulani sasa kinachomuumiza huyu yeye ndiye anayekutana moja kwa moja na mteja(anayetaka efd receipt) na mamlaka ya mapato (TRA waki-track mauzo yake kupitia efd) huku anakochukua mzigo risit hapewi kwa ajili ya kufanya return ya kodi TRA!

Kwenye bold,nimemsoma jamaa main post hapo juu anasema mtaji wake ni Tsh 15mill,kwa hela hii ni ngumu kubishana na ma-giant wa biashara kwa kuwataka wampe risiti kwa kila bidhaa na kawaida yao huwa hawatoi wanakata udhamini na hata wakitoa 15 mill atanunua items ngapi za kuzungusha sokoni ili biashara iende?kwa mtaji huo hata angezungusha vipi na faida aliyosema kwa siku ni 12K ndani ya mwaka bado asingefika VAT so ni kusema alitumbukia kwenye shimo baya la utumwa wa kibiashara.
 
Huku mtaani wapo matajiri wanaoingiza mizigo wanawapa kwa mali kauli vendors,(kama mdau hapa) wao huwa hawana frame mzigo wanautoa store wanampa muhusika kwa makubaliano may be kila siku jioni au kila wiki watapitia pesa kiasi fulani sasa kinachomuumiza huyu yeye ndiye anayekutana moja kwa moja na mteja(anayetaka efd receipt) na mamlaka ya mapato (TRA waki-track mauzo yake kupitia efd) huku anakochukua mzigo risit hapewi kwa ajili ya kufanya return ya kodi TRA!

Kwenye bold,nimemsoma jamaa main post hapo juu anasema mtaji wake ni Tsh 15mill,kwa hela hii ni ngumu kubishana na ma-giant wa biashara kwa kuwataka wampe risiti kwa kila bidhaa na kawaida yao huwa hawatoi wanakata udhamini na hata wakitoa 15 mill atanunua items ngapi za kuzungusha sokoni ili biashara iende?kwa mtaji huo hata angezungusha vipi na faida aliyosema kwa siku ni 12K ndani ya mwaka bado asingefika VAT so ni kusema alitumbukia kwenye shimo baya la utumwa wa kibiashara.

Sema hapo kwenye faida ya Elfu 12 ni [emoji477]️ hata muuza matunda tu anakunja faida mara mbili ya hiyo kwa siku
 
Asante,
Huku mtaani wapo matajiri wanaoingiza mizigo wanawapa kwa mali kauli vendors,(kama mdau hapa) wao huwa hawana frame mzigo wanautoa store wanampa muhusika kwa makubaliano may be kila siku jioni au kila wiki watapitia pesa kiasi fulani sasa kinachomuumiza huyu yeye ndiye anayekutana moja kwa moja na mteja(anayetaka efd receipt) na mamlaka ya mapato (TRA waki-track mauzo yake kupitia efd) huku anakochukua mzigo risit hapewi kwa ajili ya kufanya return ya kodi TRA!

Kwenye bold,nimemsoma jamaa main post hapo juu anasema mtaji wake ni Tsh 15mill,kwa hela hii ni ngumu kubishana na ma-giant wa biashara kwa kuwataka wampe risiti kwa kila bidhaa na kawaida yao huwa hawatoi wanakata udhamini na hata wakitoa 15 mill atanunua items ngapi za kuzungusha sokoni ili biashara iende?kwa mtaji huo hata angezungusha vipi na faida aliyosema kwa siku ni 12K ndani ya mwaka bado asingefika VAT so ni kusema alitumbukia kwenye shimo baya la utumwa wa kibiashara.
Nimepata kitu muhimu sana..ubarikiwe
 
Boss ni kuwa makini:

Shida ya huu mchezo baada ya miaka kadhaa Utajikaanga kwenye manunuzi na matumizi na siku wakikufanyia examination watakuumiza.

Sikia boss, unahitaji akili sana kuwadanganya TRA maana sio mafala. Unless ww sio mkubwa na mara nyingi hawaangaiki na examination ya data zako.

Kama unatoa risiti pungufu hakikisha na wewe unapokea risiti pungufu, una matumizi pungufu, faida pungufu sababu wanatumia mbinu ya kupima uwiano kati ya mauzo, manunuzi, faida na gharama za biashara.

Huwezi liona hili mpaka siku ukijifanyia analyis ndefu, miez m3 sita au mwaka na ukawa na jicho la kihasibu ndipo utaona hizo gapes.

Sasa sheria inawaruhusu TRA kufanya examination hata miaka 5 nyuma. Na wakikufanyia mtu wa aina yako watajiuliza tu haya maswali:

Kwann huyu mtu ana mauzo machache ila anafanya manunuzi kuongeza mzigo ambao upo stoo hauuzi?

Kama wewe ni smart kwamba hata manunuzi huchukui risiti linakuja swali la pili.

Kwanini huyu mtu ana manunuzi machache, mauzo machache ila gharama za uendeshaji ni kubwa?

Kama wewe ni smart kuficha manunuzi, mauzo na gharama, sheria inaaruhusu kuchungulia miamala yako na swali lingine linakuja

Kwann huyu mtu ana mauzo madogo, gharama sio kubwa, manunuzi madogo ila mzunguko wa fedha bank na mpesa,tigo pesa huko ni mkubwa?

Kama hupeleki pesa bank au tigo pesa huko mwonekano wa biashara yako unaweza ukakusaliti kutegemeana na eneo la biashara sababu serikali inaelewa nchi yake kila sehemu na mzunguko ulivyo.

Ukifanya kilakitu kwa 100% unaweza ukaumia na ukafunga biashara, ila ukiitafuna sana serikali basi uombe miaka 5 ipite bila ukaguzi otherwise watakutafuna wao.

TANZANIA MFANYABIASHARA WA DRS LA SABA ANA AKILI KULIKO GRADUATE WA DEGREE FIELD HUSIKA.
Kinacho katisha kulipa kodi ni kwamba wananchi wanalipa sana kodi halafu kodi hizo wanatumia wanasiasa ambao sio walipa kodi hivyo ni afadhari kukwepa tuu kodi
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kinacho katisha kulipa kodi ni kwamba wananchi wanalipa sana kodi halafu kodi hizo wanatumia wanasiasa ambao sio walipa kodi hivyo ni afadhari kukwepa tuu kodi
Mkuu sawa ila,
Ukwepaji wa kodi na ufujaji wa pesa za uma ni kinyume cha sheria. Kwepa kodi au fisadi pesa ya uma ila Jamhuri ikikupata na iwapo huna kinga unapoteza. Uamuzi ni wako boss.
 
Back
Top Bottom