TRA yafungulia akaunti zote za Wafanyabiashara zilizokuwa zimefungwa kutokana na madeni ya kodi

TRA yafungulia akaunti zote za Wafanyabiashara zilizokuwa zimefungwa kutokana na madeni ya kodi

Truth be told, mazoea mabaya ya muda mrefu yamewafanya wafanyabiashara wengi wawe na kasumba ya kutoridhia kutii sheria bila shurti --- lugha ya kutoa kodi kwa hiari hawaielewi kamwe.

Wamejifunza njia ya mikato, ujanjaujanja, wiziwizi, rushwarushwa, dilidili and the like. Sasa wakiletwa kwenye mstari, by definition, wao wanadhani wanaonewa. What!???
Sababu zinazoleta matatizo haya ni mazingira ya kuzungumzia ulipaji kodi. Hakuna vikao halali vya kuzungumzia makadirio ya kodi. Wakusanyaji kodi wamegeuka kuwa Polisi. Hilo ndiyo tatizo kubwa. Kukusanya kodi huendi kumvamia mtu, au kumshtukiza. Na mnaposhindwa kukubaliana siyo upande mmoja ukachukue rungu la kuja kuua, huwa kuna takiwa kuwe na levels za majadiliano. Iko haja ya kuelewa maana halisi ya ulipaji kodi. Kwa taarifa tu wakwepa kodi bado wanaendelea, waliofungiwa wengi ni wazalendo wajasiria mali waliokataa kutoa hongo. Kwani si tunawajua wakusanyaji walivyo matajiri sasa hivi? Au mwingine anafanya hivyo ili kwa madhumuni apandishwe cheo tu. Tumeshasema hapa, biashara zote zilizokufa kwa sababu ya kodi zifanyiwe uchunguzi maalum na matokeo yawekwe wazi.
 
Hakuna mtu anayependa kuzaliwa bila kumjua baba/Mama yake, kama ulipata hiyo privilege mshukuru Mungu
Isiwe excuse ya kuwafanya wenzio matendo maovu kama aliyofanya Mwendazake. Ule unyama ni sawa na Iddi Amin tu
 
Ngoja nikupe mfano mwepesi ya list ya tozo zilizopo kwenye income tax kama wewe umeajiriwa baadhi ya nchi EU, halafu unakabiashara kako pembeni, una saving accounts, umewekeza kwenye kampuni unapata dividend, unakaa nyumba ya serikali/kampuni, unatumia gari la serikali/kampuni, umefanya vizuri kazini umelipwa bonus.

Kwanza utapigiwa hesabu ya thamani gari unalotumia kama vile bado mpya: utatakiwa kulipa 18% kodi ambayo ni thamani ya hilo gari kwa mwaka kutoka mfukoni kwako.

Nyumba kama thamani yake ni 100m wanaweza toa 30m, hiyo 70million utalipa 2.25% kodi kutoka mfukoni kwako.

Umekopeshwa kama vile wabunge wa Tanzania labda 150m mkopo auna riba utatakiwa kulipa 2.25% ya hiyo hela kama kodi kila mwaka.

Mafuta kuna annual ya allowance kama unawekewa zaidi ya 5m kwa mwaka utaambia ulipe kodi labda 2m

Posho unayopokea unalipa kodi

Na mazazaga mengine ya ‘benefit in kinds’ unayopata.

Hizo tozo zote zinajumlishwa kwenye mshahara wako baada ya kulipa PAYE, wana jumlisha na faida yako ya biashara baada ya VAT, saving interest za bank ulizopata ndani ya mwaka na dividend received kwenye share za biashara. Hapo utatolewa personal allowance.

Halafu ndio mziki wako wa kodi unaanza, sasa inategemea upo kundi gani kutokana income zako zote kuna makundi matatu; sikia tu wale wenye income kubwa mziki wake kwenye income tax. Baada ya kulipa hapo kinachofuata ni National Insurance contribution payments.

Hayo ya pension utalipa kama wengine (if anything wataita allowable expenditures) yaani nyie vikodi vya VAT mnalalamika kweli. Kodi huko kwa wenzetu ni balaa hasa kwa matajiri.
Ndiyo maana tumebaki kutembeza bakuli kwa wahisani ambao wakitupatia hiyo peanut wanakuja kuchukua raw material na madini yetu bure. Tunawaita eti wawekezaji. Yaani hayo madini na raw materials ni zao, waliziwekeza tu kwetu?
 
Hivyo dhana yakusema watu hawapendi kulipa kodi si sahihi.
Acha kudanganya. Duniani kote na enzi zote hakuna anayependa kulipa kodi. Vitabu vitakatifu kama Bibilia vimeandika hivyo. Mtoza ushuru alihesabika ni mdhambi ambaye akifariki moto wa milele ulikuwa unamngojea. Mtoza ushuru alihesabika ni agent wa shetani Lucifer. Ndiyo nature ya binadamu ilivyo. Lazima mabavu yatumike kukusanya hizo kodi. Mabavu hayo yamewekwa kwenye sheria za kila nchi. Ukitaka kuyaondoa basi ondoa au badilisha hizo sheria husika. Weka sheria za kubembelezana na majadiliano na miafaka ya kulipa au kutolipa kodi stahiki.
 
Yule mzee ujue hakuwa na simile hata kidog dhidi ya uovu.Hata kama ulifanya maovu miaka 10 iliyopita anakushughlikia .Kiufupi alifukua makaburi kitu ambacho usipojitoa kafara huwezi.Kwan watumishi hewa waliajiriwa leo? C ni zaid ya miaka 20 nyuma! Pembejeo hewa,wanafunzi hewa vyuo Vikuu na mengi mengi kabisa.Kwa upande wa biashara kama mwenendo ulikuwa hivyo basi huenda kulikuwa na Tax clearance za kifisad .Walifuatiliwa na hatua zikachukuliwa na ndio Maana wanaolalamika leo wala mahakaman hawajaenda. Sasa Leo wamesamehewa tuu wanataka huruma ooh account zetu zilifungwa, mbona hamsemi zilifungwa kwa sababu zipi? Inamaana waliofunga walikuwa wendawazimu wakaendesha zoez la fungafunga tuu? Jiulize mbona cio wote? ,,,,,,Mimi cio Sukuma Gang ila sikuuuona utawala wa Nyerere,sikuwa na ufahamu utawala wa Mwinyi na Mkapa kwan 1995 tuu yenyewe nilikuwa Std four. Ila niliona yale mambo ambayo yalikuwa wazi kwa wananchi awamu ya Nne ya maisha bora! Wengi walitafsiri Maishabora ni ilimrad uwe na Maishabora bila kujali umeyapata kwa njia ya halal ama Harman,kilichotakiwa ni Maishabora tuu. Sasa waliojitafutia Maishabora wakayapata kwa njia za haramu ndio hao wamekuja kunywa maji kwa karai awamu ya tano !RIP JPM🙆 tutakukumbuka wanyonge . Uliwaona mafisad ukiwa waziri , wale wote ambao walijitafutia maisha bora bila kujali haki za wanyonge ukalala nao mbele kwelikweli. Kwkuwa walikuwa na uwezo kifedha ndio hao wenye sauti katika jamii,na ndio Maana uliporudi kwa baba muumba wanakuita majina Mabaya (Si unakumbuka ukiwa hai walikuita Dictator) saivi wanakuita "mwendazake" Jina ambalo nalikasirikia kishenzi.Tangu JPM amefariki inakuaje tunasikia Mabaya tuu Ile hali Mikoan tunapita chochoro zenye lami? Mwenzenu nilipoziona barabara zenye mabaki ya lami nikadhan Wakolon tuu ndio waliweza kujenga.Hayat JPM akanibadilisha mtizamo sasa najua kumbe wabongo tunaweza!!!!!
Ndugu ungekuwa unazielewa sheria za kodi basi ungekuwa umegundua yote uloandika hapo uko nje ya mada. Ndo maana kuna mtu alisema we need strong institutions and not strong people
Huyo mtu wako unayemsifia yuko wapi sasa
Elewa mada iliyo mezani vinginevyo utakuwa unademka tuu
 
Back
Top Bottom