Tractor gani zuri kati ya Massey Ferguson 590 na New Holland

Tractor gani zuri kati ya Massey Ferguson 590 na New Holland

ndoto2020

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2017
Posts
267
Reaction score
373
Wajuzi na wazoefu wa kilimo nataka kununua tractor la kulimia liwe multipurpose kwa kulimia knye mashamba ya mpunga ludewa na mbarali lakini pia kwa kilimo cha mahindi vwawa . Nasikia massey ni imara sana na spea ni bei rahisi na life span yake ni ndefu ila new holland td 82 naona kama lina nguvu na ndo nilizoea kuyaona turiani yakilima knye mpunga na ifakara huko sijawahi kuona massey ferguson . Nishaurini lipi bora nissiiingie chaka
 
Zote hizo ni vyuma haswa. Massey ferguson zipo za pakistan na uingereza. Uingereza ndo bei juu zaidi na spare ndo hivyo hivyo. New holland nae yupo vizuri sana
 
Zote hizo ni vyuma haswa. Massey ferguson zipo za pakistan na uingereza. Uingereza ndo bei juu zaidi na spare ndo hivyo hivyo. New holland nae yupo vizuri sana
Shukran kwa ushauri ndugu lakini Massey sizioni mikoa ya kati dodoma na manyara
 
Wajuzi na wazoefu wa kilimo nataka kununua tractor la kulimia liwe multipurpose kwa kulimia knye mashamba ya mpunga ludewa na mbarali lakini pia kwa kilimo cha mahindi vwawa . Nasikia massey ni imara sana na spea ni bei rahisi na life span yake ni ndefu ila new holland td 82 naona kama lina nguvu na ndo nilizoea kuyaona turiani yakilima knye mpunga na ifakara huko sijawahi kuona massey ferguson . Nishaurini lipi bora nissiiingie chaka
Massey Ferguson ni mashine Ila iwe ya Ulaya Sio Yale ya Pakistan. New Holland pia yapo vizuri Sana
 
Wajuzi na wazoefu wa kilimo nataka kununua tractor la kulimia liwe multipurpose kwa kulimia knye mashamba ya mpunga ludewa na mbarali lakini pia kwa kilimo cha mahindi vwawa . Nasikia massey ni imara sana na spea ni bei rahisi na life span yake ni ndefu ila new holland td 82 naona kama lina nguvu na ndo nilizoea kuyaona turiani yakilima knye mpunga na ifakara huko sijawahi kuona massey ferguson . Nishaurini lipi bora nissiiingie chaka

Kila moja inafaida na hasara zake.
Massey inadumu kwa muda, na matengenezo yake si ghali, ila haina uwezo wa kufanya kazi muda mrefu mfululizo.New holand inaweza fanya kazi kubwa mfululizo lakini ikiharibika matengenezo ni ghali, na si rahisi kuitengeneza ikarudi sehemu ya awali.
Mfono, KAMA MASSEY ITALIMA 20HEKA KWA SIKU, NEW HOLANDI ITALIMA 30-40 KWA SIKU.

NAKUSHAURI UNUNUE SWARAJ NI NZURI ZAIDI NA MATENGENEZO YAKE SI GHALI
 
Weka sifa kwanza bwana

Jitangaze na utushawishi
Atakuja na Mahindra huyo maana tractor za Indiana China Wahawasemi brand gani wanakuambia njoo tukupe tractor imara kwa bai nafuu
 
Asante sana Mkuu cilla

Hii figure ni bei au model?

Massey Ferguson (Brand New Tractor Model) 240,260,375,385.
 
Wajuzi na wazoefu wa kilimo nataka kununua tractor la kulimia liwe multipurpose kwa kulimia knye mashamba ya mpunga ludewa na mbarali lakini pia kwa kilimo cha mahindi vwawa . Nasikia massey ni imara sana na spea ni bei rahisi na life span yake ni ndefu ila new holland td 82 naona kama lina nguvu na ndo nilizoea kuyaona turiani yakilima knye mpunga na ifakara huko sijawahi kuona massey ferguson . Nishaurini lipi bora nissiiingie chaka

Mimi nakushauriii Rafita brand ya FIAT....hutoijutiaaa hii brand....
Ingawa kampuni mama ya Fiat imeshanunuliwa na New Holland lkn kama unaweza tafuta Fiat OG yenyewe...
Hizi New Holland unazoziona sasa hivi ni advanced version ya Fiat ndio maaana kuna Fiat nyngn unakuta imeandikwa Fiat-New Holland 100s
 
Kuna maeneo wanapenda swaraj. Dodoma ni sehemu mojawapo sababu ardhi ya kule ni mchanga pia kwahiyo swaraj inatosha kwao. Trekta nyingi zinafaa, ila zingatia matunzo sana, wingi wa trekta ina maanisha urahisi wa kupata mafundi wake na vipuri kwa wakati pia
Shukran kwa ushauri ndugu lakini Massey sizioni mikoa ya kati dodoma na manyara
 
Kila moja inafaida na hasara zake.
Massey inadumu kwa muda, na matengenezo yake si ghali, ila haina uwezo wa kufanya kazi muda mrefu mfululizo.New holand inaweza fanya kazi kubwa mfululizo lakini ikiharibika matengenezo ni ghali, na si rahisi kuitengeneza ikarudi sehemu ya awali.
Mfono, KAMA MASSEY ITALIMA 20HEKA KWA SIKU, NEW HOLANDI ITALIMA 30-40 KWA SIKU.

NAKUSHAURI UNUNUE SWARAJ NI NZURI ZAIDI NA MATENGENEZO YAKE SI GHALI
Ulimbo Swaraj zaidi ya dodoma na kondoa sizioni ifakara wala mbeya zina mudu kweli kazi ngumu?
 
Ulimbo Swaraj zaidi ya dodoma na kondoa sizioni ifakara wala mbeya zina mudu kweli kazi ngumu?
Kiberege pale swaraj huwa zinakuja msimu wa kuandaa mashamba na zinalima vizuri tu. Sema madereva wengi(si wote) wa swaraj mawenge sana. Zinaendeshwa utafikiri gari tu. Yani shambani linakimbizwa hatari, matokeo yake udongo unarushwa mbali na wanaacha viraka vingi sana. Kumudu kazi ngumu inaweza ila inategemea na aina ya kazi pia. Kubeba magogo mazito swaraj haitomudu kwa muda mrefu ila kulima eka 10 hadi 12 kwa siku inaweza
 
Kiberege pale swaraj huwa zinakuja msimu wa kuandaa mashamba na zinalima vizuri tu. Sema madereva wengi(si wote) wa swaraj mawenge sana. Zinaendeshwa utafikiri gari tu. Yani shambani linakimbizwa hatari, matokeo yake udongo unarushwa mbali na wanaacha viraka vingi sana. Kumudu kazi ngumu inaweza ila inategemea na aina ya kazi pia. Kubeba magogo mazito swaraj haitomudu kwa muda mrefu ila kulima eka 10 hadi 12 kwa siku inaweza
Shukran sana kwa taarifa hizo huwa ni four wheel au two wheel? Kingine bei ya kukodi tractor kipindi cha msimu sh ngapi? Na kazi huwa zinapatikana za kutosha najiuliza nikimpa ndugu yangu tractor aje nalo Kigerege au ifakara ni rahisi kupata angalau eka 70 mpaka 100 kwa wiki kwa sababu tractor ni Zima sana
 
Shukran sana kwa taarifa hizo huwa ni four wheel au two wheel? Kingine bei ya kukodi tractor kipindi cha msimu sh ngapi? Na kazi huwa zinapatikana za kutosha najiuliza nikimpa ndugu yangu tractor aje nalo Kigerege au ifakara ni rahisi kupata angalau eka 70 mpaka 100 kwa wiki kwa sababu tractor ni Zima sana
Kiberege nina uzoefu nako. Ifakara sijawahi kufanya kazi kule. Swaraj zote zinazokuja kule ni 2wd, sijawahi kuiona ya 4wd. Kupata eka 40 hadi 50 kwa wiki inawezekana kama una dereva mzoefu wa maeneo ya kule au ukubali kufanya kazi na madalali. Bei ya juu ni elfu 45 kwa eka na bei ya chini ni 35 kwa eka(hii bei ya chini wanapenda sana watu wa swaraj kutokea kibaigwa na huwa wanakaa kijiwe cha peke yao maana wakichanganyika na wenye matrekta mengine hawapati kazi). Kama huwezi kusimamia mwenyewe hilo trekta nakuomba usilipeleke huko au usinunue kabisa hilo trekta. Narudia tena, kama huwezi kusimamia mwenyewe hilo trekta nakuomba usilipeleke huko au usinunue kabisa hilo trekta. Maana hutoiona pesa yake ila trekta utaona linachakaa tu. Kule kazi zipo nyingi tena ukiwa na trailer huwezi kukosa kazi. Ila ndo hivyo vizuri kula na wenzio, lazima upate mzoefu wa kule awe dereva wako au upate dalali. Kingine uwe mjanja, usiwe wa kukubali kila kitu. Fuatilia kila kitu wewe mwenyewe. Trekta likipata kazi ya kulima hakikisha upo hapo linapolima na wewe ndio uwe mpimaji wa ukubwa wa hilo shamba. Kila taarifa ihakiki na utunze kumbukumbu za hela zinazoingia na kutoka kupitia hilo trekta
 
Kingine service, kubadili oil, oil filters, diesel filters, kusafisha (kupuliza) air filter. Weka mafuta masafi. Japo kwa kiberege diesel ni ya kuuziwa kwenye madumu ila kuna sheli inajengwa jirani pale (mang'ula) nauli kwa pikipiki ni elfu 5 hadi elfu 8, ukizembea utauziwa diesel yenye maji. Usitumie oil za kupima, nunua dumu la lita 20 au lita 5, badili mwenyewe au simamia inavyobadilishwa. Oil inayobaki hifadhi utaitumia wakati mwingine. Engine oil no40, utatumia kati ya lita 5 hadi 8. Chagua kampuni moja na uwe unajitahidi kutumia hiyo hiyo kila wakati.
 
Kiberege nina uzoefu nako. Ifakara sijawahi kufanya kazi kule. Swaraj zote zinazokuja kule ni 2wd, sijawahi kuiona ya 4wd. Kupata eka 40 hadi 50 kwa wiki inawezekana kama una dereva mzoefu wa maeneo ya kule au ukubali kufanya kazi na madalali. Bei ya juu ni elfu 45 kwa eka na bei ya chini ni 35 kwa eka(hii bei ya chini wanapenda sana watu wa swaraj kutokea kibaigwa na huwa wanakaa kijiwe cha peke yao maana wakichanganyika na wenye matrekta mengine hawapati kazi). Kama huwezi kusimamia mwenyewe hilo trekta nakuomba usilipeleke huko au usinunue kabisa hilo trekta. Narudia tena, kama huwezi kusimamia mwenyewe hilo trekta nakuomba usilipeleke huko au usinunue kabisa hilo trekta. Maana hutoiona pesa yake ila trekta utaona linachakaa tu. Kule kazi zipo nyingi tena ukiwa na trailer huwezi kukosa kazi. Ila ndo hivyo vizuri kula na wenzio, lazima upate mzoefu wa kule awe dereva wako au upate dalali. Kingine uwe mjanja, usiwe wa kukubali kila kitu. Fuatilia kila kitu wewe mwenyewe. Trekta likipata kazi ya kulima hakikisha upo hapo linapolima na wewe ndio uwe mpimaji wa ukubwa wa hilo shamba. Kila taarifa ihakiki na utunze kumbukumbu za hela zinazoingia na kutoka kupitia hilo trekta
Du ndugu yangu una details za kutosha ki ukweli nina ndugu Tz na nilipo matrecta used sio bei mbaya sema zikifika bongo story nyingi sana , NILILETA MF 590 wakasema haina dili sana kubwa mafuta mengi haina four wheel kwa hiyo haiwezi kulima mashamba ya hela nyingi ambayo ni ya mpunga, nikaongeza New holland TD 75 4 WHEEL team nyingine inaanza kusema hamna kazi morogoro labda waende mbarali na sisi home base ni A town naomba no yako yenye whatsup tuongee kidogo
 
Shukran sana kwa taarifa hizo huwa ni four wheel au two wheel? Kingine bei ya kukodi tractor kipindi cha msimu sh ngapi? Na kazi huwa zinapatikana za kutosha najiuliza nikimpa ndugu yangu tractor aje nalo Kigerege au ifakara ni rahisi kupata angalau eka 70 mpaka 100 kwa wiki kwa sababu tractor ni Zima sana
Mbona heka za kawaida hizo mkuu!
 
Back
Top Bottom