Travelholic (wanaopenda kusafiri) na adventurers tukutane hapa

Hata mm kusafiri ni hobby yangu ila tatizo vyuma vimekaza


Wenzetu walio endelea huwa wanatembea sana embu jiulize huwa wanatafuta nn..?

Asikwambie mtu kusafiri raha sana hasa unapo safari na bby mama wako aisee mnaenjoy sana




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafikir mim pia ni Travelholic juz kat disemba nimepiga route ambayo nafikir sitasafir for four months yan sina ham! Nlitoka Dar to kigoma via dom, manyoni tabora then kasulu nikala pozi mjin kasulu then nikaanza kuitafuta mwanza kupitia kakonko, kibondo, nyakanazi, geita then mwanza duh nilichoka sana. Ila safar yang ya kwanza zanzibar na flying horse sitakuja isahau aiseee dakika 20 baada ya kutoka ferry nilitaman nimtafute mhudum ninwambie nirudisheni ferry [emoji28], tulitumia masaa matatu, picha linaanza engine moja ikazima wakapambana ikawaka kufika mbele mawimbi hatar, boti inayumba hakuna mfano, nikamuuliza mama mmoja hii hali ni kila siku?! Akasema 'hapana hata mim leo nashangaa'! Nilichofanya nikatuma msg kwa watu wangu wa karibu nikajikabidh kwa Mungu baba [emoji28]! Ila tulifika salama tukala bata sanaa!! At the mid of bata nikikumbuka kuna kurud bara nachoka [emoji28], kuna mtu akanambia panda Azam sea link ile ya mizigo you will feel nothing kweli bana nili enjoi kupanda lile dude tulitoka zanzibar sa nne usiku tulifika fery sa 11 alfajir! So far nimepita/tembea mikoa isiyopungua 15 (mikoa yote niliyokua nataman kutembelea nishaitembelea)! Najifunza vingi kupitia kusafir
 
Mbugani mzee huwaga kuna upekee wake sana...unapata aman ya moyo ya kweli. Ndy maana wazungu husafiri na kuja kukaa Serengeti hata mwezi mzima akitafakari maisha.
 

Mkuu hapo Nungwi ulipita na jahazi kweli una roho ngumu watu wanapita na meli tu hapatoshi bu the way hongera sana.......
 
Kusafiri ni advanture kwa kweli me napenda hasa kwa usafiri wa bus safari ninayoikumbuka ni ya kutoka Dar - são paulo, Brazil masaa 17 angani ilinikera kwa kuwa angani huoni kitu....another trip ni ndani ya Brazil kutoka mji wa São paulo kwenda Rio de janeiro niliipenda kwa kuwa nilisafiri kwa bus masaa 10
 
Mkuu hapo Nungwi ulipita na jahazi kweli una roho ngumu watu wanapita na meli tu hapatoshi bu the way hongera sana.......
haha ndio tulipita na jahazi ilikua ni kama nambeep Allah bahat siku zetu zilikua mbali tulifika salama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…