TRC na TANESCO kuweni makini na SGR, iko siku itagoma kusimama

TRC na TANESCO kuweni makini na SGR, iko siku itagoma kusimama

Upekuzi101

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
221
Reaction score
542
Sitaki kusema natabiri ila napenda kuwatadharisha shirika la reli wawe makini na SGR, hayo makosa madogo madogo ya hii train kusimama simama bila kuelewa sababu za msingi, mara wakati mwingine utasikia umeme umekatika, kuweni makini ipo siku hii train itakataa kusimama, sijui kitakachotokea hapo lakini tunaomba tusisikie kuwa kazi ya Mungu haina makosa.

Train imenunuliwa kwa pesa za watanzania, hatujui kama tumepigwa au hatujapigwa ila tumewakabidhi nyinyi TRC muhisimamie ilete matokeo tunayotarajia na ituletee heshima katika nyanja ya usafirishaji barani Afrika. Tumeanza kuona tukimwagiwa sifa na nchi za jirani kuwa tumepiga hatua, wanasema Tanzania sasa ni nchi ya kupigiwa mfano ila hichi kinachoendelea hapa kila siku train kuzimazima na kusimamasimama ni aibu.

Tunaanza kuaibishana sasa, mwisho wa siku maintenance itatushinda kama ilivotokea kwa mabasi ya mwendo kasi. Mabasi yananunuliwa kibao unayakuta yard mengine yamelala eti kisa bolt moja hakuna na anayetakiwa kusaini amesafiri mwezi mzima.

Mama Samia tunaomba utoe tamko lako la kiuongozi kwa watu wa TANESCO NA TRC, wasilete utani na SGR hii ni investment yetu kubwa na tunatakata ufanisi siyo blabla na excuse za kila siku.
 
Kuna ile movie ya Runaway Train sema ile reli yake ilikuwa kamili sijui hii ikigoma kusimama na huko mbele hata hakuna madaraja.
 
Kwamba kuna siku umeme utakatika halafu friji iendelee kuwaka tu nyumbani
 
Duuh, Physics niliacha O level ila naamini umeme ukikatika itasimama tu haitatembea.
 
Treni la mtumba unategemea lisizime mara Kwa mara.Mimi kama mwana TRC nasema kuwa treni hii inasimama Kwa sababu ya uchakavu wake.Yaani haifai Tena Kwa matumizi ya binadamu
 
Sitaki kusema natabiri ila napenda kuwatadharisha shirika la reli wawe makini na SGR, hayo makosa madogo madogo ya hii train kusimama simama bila kuelewa sababu za msingi, mara wakati mwingine utasikia umeme umekatika, kuweni makini ipo siku hii train itakataa kusimama, sijui kitakachotokea hapo lakini tunaomba tusisikie kuwa kazi ya Mungu haina makosa.

Train imenunuliwa kwa pesa za watanzania, hatujui kama tumepigwa au hatujapigwa ila tumewakabidhi nyinyi TRC muhisimamie ilete matokeo tunayotarajia na ituletee heshima katika nyanja ya usafirishaji barani Afrika. Tumeanza kuona tukimwagiwa sifa na nchi za jirani kuwa tumepiga hatua, wanasema Tanzania sasa ni nchi ya kupigiwa mfano ila hichi kinachoendelea hapa kila siku train kuzimazima na kusimamasimama ni aibu.

Tunaanza kuaibishana sasa, mwisho wa siku maintenance itatushinda kama ilivotokea kwa mabasi ya mwendo kasi. Mabasi yananunuliwa kibao unayakuta yard mengine yamelala eti kisa bolt moja hakuna na anayetakiwa kusaini amesafiri mwezi mzima.

Mama Samia tunaomba utoe tamko lako la kiuongozi kwa watu wa TANESCO NA TRC, wasilete utani na SGR hii ni investment yetu kubwa na tunatakata ufanisi siyo blabla na excuse za kila siku.
Kweli kabisa mama awe mkali kiasi fulani
 
una maana gani kusema treni SGR itashindwa kusimama..kwani hiyo treni si iko automatic kwamba umeme ukikata na mifumo yote inayotumia umeme nayo inazima ni kama vile ww ukiwa unatizama TV pindi umeme ukikatika au ukiwa unaendesha gari likaishiwa mafuta linazima tu hakuna kinachoendelea basi na hilo SGR nayo ni hivyo itajizima tu ..labda useme litazimika gafla mita 100 karibu na stesheni wakati lipo kwenye speed uke mserereko baada ya kuzima ndo utabamiza dude ila huku njiani haina shida
 
una maana gani kusema treni SGR itashindwa kusimama..kwani hiyo treni si iko automatic kwamba umeme ukikata na mifumo yote inayotumia umeme nayo inazima ni kama vile ww ukiwa unatizama TV pindi umeme ukikatika au ukiwa unaendesha gari likaishiwa mafuta linazima tu hakuna kinachoendelea basi na hilo SGR nayo ni hivyo itajizima tu ..labda useme litazimika gafla mita 100 karibu na stesheni wakati lipo kwenye speed uke mserereko baada ya kuzima ndo utabamiza dude ila huku njiani haina shida
Mbona ile ya reli ya kati ilisimama kisha ghafla ikaanza kurudi kinyumenyume kwa kasi ya kuzidi sgr ikaishia kuanguka na kuua.
 
Duuh, Physics niliacha O level ila naamini umeme ukikatika itasimama tu haitatembea.
Si walisema lakini inauwezo wa kutunza umeme kwa masaa mawili hata kama umeme utakatika itaendelea kutembea
 
Sitaki kusema natabiri ila napenda kuwatadharisha shirika la reli wawe makini na SGR, hayo makosa madogo madogo ya hii train kusimama simama bila kuelewa sababu za msingi, mara wakati mwingine utasikia umeme umekatika, kuweni makini ipo siku hii train itakataa kusimama, sijui kitakachotokea hapo lakini tunaomba tusisikie kuwa kazi ya Mungu haina makosa.

Train imenunuliwa kwa pesa za watanzania, hatujui kama tumepigwa au hatujapigwa ila tumewakabidhi nyinyi TRC muhisimamie ilete matokeo tunayotarajia na ituletee heshima katika nyanja ya usafirishaji barani Afrika. Tumeanza kuona tukimwagiwa sifa na nchi za jirani kuwa tumepiga hatua, wanasema Tanzania sasa ni nchi ya kupigiwa mfano ila hichi kinachoendelea hapa kila siku train kuzimazima na kusimamasimama ni aibu.

Tunaanza kuaibishana sasa, mwisho wa siku maintenance itatushinda kama ilivotokea kwa mabasi ya mwendo kasi. Mabasi yananunuliwa kibao unayakuta yard mengine yamelala eti kisa bolt moja hakuna na anayetakiwa kusaini amesafiri mwezi mzima.

Mama Samia tunaomba utoe tamko lako la kiuongozi kwa watu wa TANESCO NA TRC, wasilete utani na SGR hii ni investment yetu kubwa na tunatakata ufanisi siyo blabla na excuse za kila siku.
Nimekuelewa sana!
 
Back
Top Bottom