TRC yaomba radhi kutokana na hitilafu ya umeme katika Treni ya SGR

TRC yaomba radhi kutokana na hitilafu ya umeme katika Treni ya SGR

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-08-02 at 16.20.08_168dbd2b.jpg

TAARIFA KWA UMMA HITILAFU YA TRENI YA KAWAIDA YA ABIRIA KUTOKA DODOMA KUELEKEA DAR ES SALAAM

Dar es Salaam, Tarehe 2 Agosti 2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kwa abiria waliosafiri kutoka Dodoma saa 2.15 usiku kuelekea Dar es Salaam Agosti 1, 2024 kwa treni ya mwendo kasi kuchelewa kuwasili kutokana na hitilafu ya kiufundi iliyotokea eneo la Mtaa wa Mshikamano Kata ya Kihonda mkoani Morogoro.

Hitilafu za kiufundi zilitokea majira ya saa 4.33 usiku na kushughulikiwa kwa muda wa takriban saa moja na kusababisha treni hiyo ya abiria kutoka Dodoma kuchelewa kuwasili Dar es Salaam kwa wakati uliopangwa.

Shirika la Reli Tanzania linatoa taarifa kuwa treni ya abiria iliyobeba viongozi na wananchi wengine waliotoka Dodoma saa 1 usiku baada ya kushiriki sherehe za uzinduzi wa SGR waliwasili Dar es Salaam kwa muda uliopangwa bila hitilafu yeyote.

TRC inazingatia usalama wa abiria kabla na wakati wa safari ili kuepusha madhara kwa watumiaji wa huduma za usafiri wa reli na linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
 
TAARIFA KWA UMMA HITILAFU YA TRENI YA KAWAIDA YA ABIRIA KUTOKA DODOMA KUELEKEA DAR ES SALAAM

Dar es Salaam, Tarehe 2 Agosti 2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaomba radhi kwa abiria waliosafiri kutoka Dodoma saa 2.15 usiku kuelekea Dar es Salaam Agosti 1, 2024 kwa treni ya mwendo kasi kuchelewa kuwasili kutokana na hitilafu ya kiufundi iliyotokea eneo la Mtaa wa Mshikamano Kata ya Kihonda mkoani Morogoro.

Hitilafu za kiufundi zilitokea majira ya saa 4.33 usiku na kushughulikiwa kwa muda wa takriban saa moja na kusababisha treni hiyo ya abiria kutoka Dodoma kuchelewa kuwasili Dar es Salaam kwa wakati uliopangwa.

Shirika la Reli Tanzania linatoa taarifa kuwa treni ya abiria iliyobeba viongozi na wananchi wengine waliotoka Dodoma saa 1 usiku baada ya kushiriki sherehe za uzinduzi wa SGR waliwasili Dar es Salaam kwa muda uliopangwa bila hitilafu yeyote.

TRC inazingatia usalama wa abiria kabla na wakati wa safari ili kuepusha madhara kwa watumiaji wa huduma za usafiri wa reli na linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

Jamila Mbarouk
MKUU WA KITENGO CHA UHUSIANO
Tunaomba majibu juu ya power bank za treni au wametutapeli wameleta ambazo hazina mfumo huo?
Ikiwa ndivyo wahusika wachukuliwe hatua kali.
 
Tunaomba majibu juu ya power bank za treni au wametutapeli wameleta ambazo hazina mfumo huo?
Ikiwa ndivyo wahusika wachukuliwe hatua kali.
Wa kuchukuwa hatua ni wananchi. Kama mmelala na mnategemea wezi wachukulie wezi wenzao hatua mtasubiri sana. Nyie kajazaneni tu viwanja vya mpira kwenye sijui Yanga na Simba day, siku mkija kumaka kwenye huo usingizi mtakuwa mmechelewa sana.
 
Back
Top Bottom